Header Ads

NGUVU ILIYOMO KWENYE MAOMBI (..MWISHO)

 
BWANA ANAKUJA 
    
Baada ya kutazama vitu vitano muhimu wakati unapoamua kupeleka maombi yako juu ya madhabahu unayoitumia kuuufikia ulimwengu wa ROHO  katika hii sehemu ya tutaangalia sana ulimwengu wa nuru tu na ulimwengu wa giza hatutaugusa kabisaa lakini masomo yanayohusu jinsi ya kuushinda yatakuja kadri muumba atakavyonipa neema nawewe pia ukipewa neema yakusoma maana mpaka dakika hii sitaki mtu awaye mtu yeyote apotee kwa uzembe wangu bali kila atende kwa upande wake kwa bidii katika kumtafuta BWANA wa majeshi ili akaiponye nchi yake mwenyewe,familia yako, biashara yako, ndoa yako, na pia masomo yako. Vile vitano vya mwanzo ni vitu ambavyo mtu unaviishi lakini kuna vitu vitatu ambavyo vya kuwa navyo unavyoenda kuomba kwa mungu navyo vinapatikan katika 2nyakati 7:14 hapo unakuta vitu vitatu vya kuwa navyo ili kumwendea bwana ambavyo ni:-

basi tuitazame pia kujinyenyekeza inamaana ya kujishusha au kuiacha thamani yako na kuiona si kitu mbele za bwana muumba wako. Ambayo inakuwa imejengwa na mambo matatu nayo ni:-
  1.           kukubali kufundishika
  2.          kutii
  3.           kuwa na kicho(hofu)


hivi vitu vitatu mbele za bwana ni muhimu sana na vyote huanzia rohoni na kufikia kuviona nje kwa mtu ni baada ya moyo wake kuwa umejaa hivyo vitu nakuwa mmoja na vitu hivyoo ndio huyo mtu hata matunda ya roho unaweza kuyaona kwa wepesi kwake. Nje ya hapo utajijua wewe tu ukiwa unamtukia mungu bali watu wa nje hawawezi hata kulijua hilo. Hapa sizungumzii walokole nazungumzia mtu mwenye safari ya kwenda mbinguni kwamaana YESU alileta uzima wa milele ambao hakusema kuwa ni kuokoka bali ni kumjua MUNGU wa pekee na yesu kristo mwanaye aliyemtuma yohana 17:3.
                   Na pia haiishi hapo inatakiwa kujivika nila yake ili tuwe naye kweli lakini ili MUNGU asikuache inabidi kufanya yale yampendezayo kwamaana nyingine ili udumu katika uso wa bwana mungu wetu inabidi ufanye mda wote yampendezayo yeye. Ukisoma yohana 8:28-29 utakutana na neno wakati wa kufundisha yesu anasema neno siyo la kwake bali la kufundishwa na baba na akilisema au kulitenda naye baba anakuwepo mda wote naye ili kulilinda neno aliloagiza lisemwe au litendwe kwa jina lake. Unaweza usielewe kwa haraka lakini namaanisha mtazame YESU aliposema lolote muombalo kwa jina langu hilo nitalifanya. Lakini siyo kila mtu akitumia jina la yesu, yesu atatenda bali lazima uwe umeitwa kwa jina lake au umefanyika kuwa mwanafunzi wake . na ili akuhesabu hivyoo ataangalia ushikaji wako wa  maaagizo yake
           . Hapo ndipo njia mbaya nazo hutazamwa YESU aliweka kila kitu kiendacho kwa baba kipitie kwake yeye na hakuna njia nyingine na kama ukitumia jina jingine  kuomba kitu utakuwa unaomba kutoka kwa mungu wa ulimwemgu huu wala siyo mungu wa mbinguni aliyeumba mbingu na nchi 2wakorintho 4:4. Basi ndugu na rafiki yangu achana na njia zako mbaya naye MUNGU atakusikia na atakusamehe dhambi zako. Na ndipo macho yake yatafumbuka, na masikio yake yatasikiliza maombi yako 2nyakati 7:15&17. 
                    Kingine ni hofu ya kutenda dhambi inatakiwa itawale ndani yako maana utakuwa unaogopa kumkosea MUNGU na ndipo utaenenda vizuri. Na wala siyo kuogopa waumini wenzio maana hukumu nao ipo juu yao. Kwamaana kwa sheria wote tulihukumiwa kifo na mwanzo tulikuwa hapo wote. Bali ROHO alibatilisha kwa kutuhuisha kutoka uharibifu mpaka kutoharibika ambako ndiko kuwa na uzima wa milele. Basi pia tafuta kujazwa na ROHO WA MUNGU ndipo dhambi utaishinda na wala siyo kwa kushika sheria. Maana ashikaye sheria huyo ni mtumwa wa hiyo sheria bali sisi kwasasa ni watumwa wa YESU na malipo ni ROHO MTAKATIFU aletaye uzima wa milele ndani yetu.
MWISHO
MWANDISHI: MICHAEL BASA 0765279698 au+255 789 799 199

Hakuna maoni

Inaendeshwa na Blogger.