Header Ads

KUMPENDEZA MUNGU (PLEASING GOD)

PLEASE=cause to feel happy and satisfied (oxford 11th edit) kwa Kiswahili ninaweza kusema inamaana ya kufanya ahisi (awe na) furaha na kujitosheleza. Kumbe kumpendeza MUNGU inatakiwa umfanye MUNGU awe na furaha na kujitosheleza. Kwa hiyo mtu akiamua kumtumikia MUNGU inatakiwa kujitoa kwa mwili wake ili iwe dhabihu ya kumfanya MUNGU awe na furaha na wewe na aridhike na kile unachokitenda ndani ya mwili wako (jumba la roho/ROHO) warumi 12:1-2. Somo la mwili linapatikana tayari pitia hapa kulisoma  na ia somo la utatu wa binaadam pitia hapa kulisoma ili kujua kwanini MUNGU alikupata mwili na katika warumi 12 anasisitiza kuitoa miili yetu kama dhabihu iliyo hai. Ili kujua maana ya dhabihu pia pitia hapa kuiona na kwa upande wa kafara pia bofya hapa kulisoma. Katika smo leo tutajikita kwenye roho/ROHO ikiwa ndani ya mwili na jinsi MUNGU anavyotaka kutokea hapo.

JE MATENDO YAPI AMBAYO ROHO NDANI YA MWILI IKITENDA HUMPENDEZA MUNGU??
 Bila utumishi uliotukuka mbele za BWANA wetu kamwe hatuwezi kumendeza MUNGU maana mtu akiuhurumia mwili wake hawezi kujitoa kwa ajili ya MUNGU. Roho wa MUNGU anataka wewe ufunge kwa ajili ya BWANA halafu wewe katika maisha yako yote haujawahi kufunga kwahiyo cha kwanza kufikria ni mwili kukosa chakula chako cha kila siku. Na ndip shetani atakukumbusha juwa juna vidonda vya tumbo. 

Ndio maana inatakiwa kuona mwili kama vazi ambalo MUNGU kakupa ili umtumikie na siyo ushindwe kwaajili ya vazi maana yeye mwili wako umejaa uharibifu na nia yake ni uadi juu ya MUNGU. Kwa hiyo mtu akiacha kula kwaajili ya MUNGU huyo ndiyo MUNGU atapendezwa naye.
Warumi 14:11&18 ‘’Kwa kuwa yeye amtumikiaye Kristo katika mambo hayo humpendeza Mungu, tena hukubaliwa na wanadamu. Mkiwezeshwa kwa uwezo wote, kwa kadiri ya nguvu ya utukufu wake, mpate kuwa na saburi ya kila namna na uvumilivu pamoja na furaha’’

MATENDO YENYEWE NI:-

      1}KUJUA MAPENZI YA MUNGU
    Watu wengi tunashinddwwa kumpendeza MUNGU maana hatujui mapenzi yake wala ya mwanaye aliyemtuma. Maana mapenzi ya KRISTO ni kufa msalabani ili kila mtu aokolewa kupitia yeye. Naomba uelewe kitu kimoja kwamba MUNGU alichofanya msalabani ni kujitoa kwa kila mtu kupitia roho wake ili kila mmoja amjue yeye katika kweli yote na kumtii yeye kama bwana na mfalme wake. Basi hakikisha unajengwa katika imani moja roho mmoja na ubatizo mmoja. Ili mapenzi ya MUNGU YATIMIZWE NDANI YAKO. WARUMI 11:6 

    Lakini pasipo imani haiwezekani kumpendeza; kwa maana mtu amwendeaye Mungu lazima aamini kwamba yeye yuko, na kwamba huwapa thawabu wale  Na wala MUNGU hawezi kukuacha maana siku zote atakuwa pamoja nawe
yohana 8:29 Naye aliyenipeleka yu pamoja nami, hakuniacha peke yangu; kwa sababu nafanya sikuzote yale yampendezayo.

    2}  KUYATENDA MAPENZI YA MUNGU
Baada ya kuyajua maenzi ya MUNGU BABA kinachofuata ni ukamilifu wa imani ndani ya kristo. Ili kuikamilisha imani inatakiwa kuanza kuyatenda maenzi ya mungu maana imani bila matendo imekufa. James 2:26 Maana kama vile mwili pasipo roho umekufa, vivyo hivyo na imani pasipo matendo imekufa. Kingine ni ibaada katika roho na kweli Hebrews 12:28 Basi kwa kuwa tunapokea ufalme usioweza kutetemeshwa, na mwe na neema, ambayo kwa hiyo tumtolee Mungu ibada ya kumpendeza, pamoja na unyenyekevu na kicho;

 3} KUJIVIKA UTAKATIFU NA KUTENDA MAAGIZO YOTE YA BIBLIA
Utakatifu ni kama vazi kwa mkiristo yeyote ambaye anasafari ya kumuona MUNGU muumba mbingu na nchi. Maana pasi na utakatifu imani si kitu wala dini zetu si kitu . ndio maana watu wanaohubiri wengi husema dini haimpeleki mtu mbinguni wala haikufanyi wewe umuone MUNGU bali dini ni kusanyiko la watakatifu ambao kwa umoja wao kama ilivyo desturi hukutana ili kumtafuta MUNGU wa kweli na kujifunza kwa umoja wao ili kufaidiana na kuzidisha upendo ndani yao. Lakini kama huwezi kuwa kumtakatifu huwezi kumuona MUNGU. Wakolosai 2:10 mwenende kama ulivyo wajibu wenu kwa Bwana, mkimpendeza kabisa; mkizaa matunda kwa kila kazi njema, na kuzidi katika maarifa ya Mungu; 1Petro 1:15 bali kama yeye aliyewaita alivyo mtakatifu, ninyi nanyi iweni watakatifu katika mwenendo wenu wote; waebrania 12:14 Tafuteni kwa bidii kuwa na amani na watu wote, na huo utakatifu, ambao hapana mtu atakayemwona Bwana asipokuwa nao;

MATUNDA YA KUTENDA YALE YAMPENDEZAYO MUNGU
  •     Kujibiwa maombi yako  1yohana 3:21-22 na lo lote tuombalo, twalipokea kwake, kwa kuwa twazishika amri zake, na kuyatenda yapendezayo machoni pake
  •        Kuwa mwana wa MUNGU kweli
  •       Kumuona MUNGU waebrania 12:14
  •       Kuwa rafiki na ndugu wa YESU KRISTO mathayo 12:47-50
  •        Kuwa mrithi wa ufalme wa mbingu tito 3:7
Mwandishi MICHAEL BASA   0765 279 698,  +255 789 799 199

Hakuna maoni

Inaendeshwa na Blogger.