Header Ads

AINA ZA WAKRISTO NA TABIA ZAO

welcome to basa ministry
WAKRISTO Ni wafuasi au watu wanaomilikiwa na kristo Yesu ,yani wako ndani ya utawala wake,na kwa Mara ya kwanza neno wakristo lilitamkwa Antiokia  LAKINI hapo kwanza likiitwa kanisa/watakatifu
    matendo 11:26  ……Na wanafunzi waliitwa Wakristo kwanza hapo Antiokia
    yohana.   15:4
AINA ZA WAKRISTO
   Zipo aina tatu za wakristo nazo ni
         1.WA MWILINI          2.WACHANGA         3.WA ROHONI

TUANGALIE KWA UNDANI TUNAWEZA KUJIFUNZA KITU

1.WAKRISTO WA MWILINI
     Hawa ni wale waliookoka siku nyingi lakini maisha yao  hayabadiliki kutokana na uvivu wa kujifunza  waebrania 5:11-12
Huyu hata ukimhimiza kujifunza atakwambia"nilishayajua kabla hujazaliwa" lakini mtu mwwenye safari wa mbinguni hawezi kuwa hivyoo maaana hawezi kummaliza kumjua MUNGU wa kweli.
*SIFA ZAO*
1,anakuwa na sura mbili ya kanisani (utakatifu)na ya mitaani (kawaida) Tito 1:16
2,akikaa na watu wasio mjua Yesu ni vigum kumtofautisha 2timotheo 2:15
3,huona aibu kujitambulisha kama ameokoka  luka 22:54-60
4,ni mtu wa mizahaa
5,wakitukanwa hujirudishia
6,wepesi kukasirika wakolosai 3:8
7,hujisifu kwa miaka mingi walivyokaa wokovuni
8,hawapend kukemewa/ kuonywa wakikosea warumi 15:14, 1korintho 4:14,wakolosai 3:16
9,waongo sana  mith 26;19
10,ni kikwazo kwa wanaotaka kuokoka

2.WAKRISTO WACHANGA
     Hawa ni wale walio amin hiv karibun, hawa hupaswa kupewa maziwa yasiyoghoshiwa ili waukulie wokovu 1petro 2:1-2
*SIFA ZAO*
1,uwezo wa kupambanua JEMA na baya ni mdogo
2,chakula kigum hawakiwezi wanahitaj zaid kufundishwa kuhusu Yesu
3,hawana uwezo wa kujua kama majaribu ni kipimo cha imani (1korintho 3:1-2)
4,hawakosekani kukutwa na utu wa kale
5,hupenda kupewa kipaumbele na kutendewa
6,wokovu ni faida yake lkn hupenda kubembelezwa
7,kusoma neno na kuomba ni mpaka wakumbushwe

3.WAKRISTO WA ROHONI
     Hawa ni wakristo waliomwamini Yesu na hudum katika neno la MUNGU, likabadili maisha YAO nao wakafananana neno (Yesu) yohana 1:1-5   matendo 9:19-22
*SIFA ZAO*
1,Hujulikana kabla hawajajitambulisha yohana 19:38-42
2,Hakuna wanachokilinda zaidi   ufunuo 2:25 mithal. 4:23  yuda 1:3
3.Hakuna mzaha kwao  zabur 1:1-6
4,ni waaminifu katika yote
5,hawana roho ya kusengenya wala kunung'unika  wafilipi 2:14
6,hutoa kipaumbele kwa mambo ya MUNGU mathayo 6:33
7,huzaa matunda maana ndio kusudi la kuitwa kwao  mathayo 13:23
8,huongozwa na ROHO na wala hawamuhuzunishi  warumi 8:14 Galatia 5:16-26
9,biblia(neno)ni rafiki yao MKUU zabur 119:11
10,ni watetezi wa IMANI yao yuda 1:20  1petro 1:5-8
  
Yaani ukiona kuna maswali yanahusu imani yako na kuyajibu huwezi hadi aje mchungaji wako basi huna uwezo kwa nafasi hiyo  matendo 4:18-21 Marko.   5:25-32
Nategemea umejijua kuwa upo kundi gani kama la kwanza piga hatua ufike la tatu kama ni la pil pia piga hatua kufika la tatu  tunaujua kuwa kuna wali umepikwa kwa harufu yake maana wali unatabia ya kusambaza harufu
JICHUNGUZE TABIA ZAKO  NA  MUNGU AKUBARIKI

MWALIM DENISY 0759735473&0658316011

Mhariri Michael BASA 0765279698,+255789799

Hakuna maoni

Inaendeshwa na Blogger.