Header Ads

DHABIHU(sacrifice)

Defn
Nikitendo cha kutoa kitu chenye thamani kubwa kwa tegemeo la kupata kitu chenye thamani au umuhimu mkubwa kwako kama ishara ya ibada {Killing an animal or person and offering to GOD or gods} kutoka 10:25, 1wafalme 11:8,  zaburi 106:37. Pia katika somo letu la
NGUVU ILIYOMO KWENYE MAOMBI kipengele cha SADAKAAU KAFARA UNAYOTOA KWENYE HUO ULIMWENGU. Tulitazama kwa  upana hiki kipengele cha sadaka lakini kwenye hili tutazama kwenye ulimwengu wa nuru tu.  Unaweza kulipitia kwanza hicho kipengele ili Kupata mwanga kwanini tunatoa sadaka au dhabihu.

  •       Kwanini tunatoa dhabihu
  • ·         Kumuabudu MUNGU
  • ·         kutafuta amani na MUNGU kutoka 5:3,8:8 hesabu 7:19-25
  • ·         Kuvunja nadhiri numbers 15:3
  • ·         Kushukuru MUNGU 2nyakati 7:3&4,zaburi 50:14-23,zaburi56:12
  • ·         Kama sadaka mbele za MUNGU
  • ·     Kusafisha dhambi 1samuel 3:14 Zaburi 51:17 
Dhabihu za Mungu ni roho iliyovunjika; Moyo uliovunjika na kupondeka, Ee Mungu, hutaudharau.
        
KUNA AINA TATU ZA DHABIHU
  1.       YENYE NGUVU:-Ni ile ambayo mtu anatoa kilicho bora kutoka kwenye vile alivyo navyo
  2.      ILIYO SAFI:- Ni ile inayofuata sharia zote za biblia wakati wa kutoa dhabihu.
  3.     ILIYO HAI:- ni ile dhabihu ambayo kwa unayotoa ajili kufanya kazi ya MUNGU;hii hubaki inakushuhudia siku zote za uhai wako.

JE NI KWANINI LEO HATUTOI ZA DHABIHU ZA KUTEKETEZWA KAMA WANA WAISRAEL WALIVYOKUWA WANAFANYA???
Kwasasa hatutoi dhabihu kama wana waisrael walivyokuwa wanafanya ni kwasababu ya agano jipya ambalo mwana wa adam alikuja kuliacha.  waebrania 10:9-14,9:26
          Je kwasasa inatakiwa kutoa dhabihu za namna gani??
waebrania 13: 15 Basi, kwa njia yake yeye, na tumpe Mungu dhabihu ya sifa daima, yaani, tunda la midomo iliungamayo jina lake.
1petro 2: 5 Ninyi nanyi, kama mawe yaliyo hai, mmejengwa mwe nyumba ya Roho, ukuhani mtakatifu, mtoe dhabihu za roho, zinazokubaliwa na Mungu, kwa njia ya Yesu Kristo.


Mwandishi MICHAEL BASA   0765 279 698,  +255 789 799 199

Hakuna maoni

Inaendeshwa na Blogger.