Header Ads

KANISA LILILOPOTEA--2

      Kuna jinsi mbili za ambazo shetani hututmia kumtawala mtu mosi ni njia ya moja kwa moja. Katika hii njia mtu anakuwa anajuwa kuwa mimi ni washetani na hata sasa nikifa mimi nitaenda kuzimu lakini kwa sababu ya mambo fulani fulani siwezi kutoka huku mfano waabudu sanamu, wachawi n.k. Pili ni njia isiyo ya moja kwa moja hili kundi limegawanyika sehem mbili ya kwanza ni ile ambayo haiombi kabisa kwa MUNGU. na ya pili ni ile ambayo inaomba kwa MUNGU. Makundi yote unakuta yanamilikiwa na shetani pasipo na wao wahusika kujua. Watu katika kundi hili unaweza kuta mpaka ni viongozi wa kanisa lakini bado matendo ya mwili ni dhahiri kwao. Je hujawahi kukuta shehe kalawiti mtoto?.
         Je RC nayo amabayo watu wanaipigia kelele rome kila siku watoto wanaingiliwa kinyume na maumbile. Monoroviani ambao nao katika nchi za UK wameruhusu mashoga kufunga ndoa tena wanatumia biblia??. Je unafuu uko wapi PENTEKOSTE nako ambako ndoa zinafungwa huku binti tayari anamimba??. EAGT na TAG ambako mzee wa kanisa anakimada ndani ya kanisa lile lile?. Wamama wa makanisani nao wamejaa maseng'enyo unaachaje kusema hili ni kundi ambalo baya zaidi kuliko lile la kwanza. kwamaana hili ni kundi linaloodhifisha na kupoteza kanisa kuliko la wachawi na waabudu sanamu wala wajenzi huru.
          Kwamaana watu wengi wanashindwa kumfuata YESU katika ROHO na kweli kwasababu yenu ninyi viongozi na wachungaji vipofu. Injili zenu zimebaki kukemea wenzenu wa mafundisho fulani au waaina fulani tu. Mfano mzuri ni huu msitari waefeso 2:20{Mmejengwa juu ya msingi wa mitume na manabii, naye Kristo Yesu mwenyewe ni jiwe kuu la pembeni.}. Msingi wa kanisa lako umejengwa juu ya akina nani kama mafundisho yako wewe ni juu ya manabii tu na siyo kufundisha jinsi ya  kutofautisha nabii wa uongo na nabii wa ukweli?.
          Kuna mchungaji unamkuta mafundisho yake yote yanaongelea mafundhisha ya manabii wa uongo tu basi hebu anza kuliangalia hili andiko pia 1yohana 4:1{Wapenzi, msiiamini kila roho, bali zijaribuni hizo roho, kwamba zimetokana na Mungu; kwa sababu manabii wa uongo wengi wametokea duniani.}. Hebu anza kufundisha kanisa lako kutembea katika Roho uone kama atapotea hata mmoja kweli kwa maana umewafanya kila waumin wako kila siku kuwa ni watoto wadogo wakati kwenye kanisa lako ambalo halizidi hata huduma tatu. Na umekaa kimya tu na kuridhika kabisa je huduma zingine za ndani ya kanisa umeziweka wapi kama siyo kwamba umezikataa mwenyewe tu??.
        Naomba kwako leo ewe Mchungaji au Padri hebu jaribu kufufua karama zote na wafanye watu watembee katika Roho ndipo utaona ni kwanini watu wanahitaji kweli tu uongo utajitenga wenyewe. Pia naomba nieleweke kuwa sijakataa kuwa manabii wa uongo hawapo bali na makristo wa uongo wapo tena wengi kuliko hata manabii. Je kuna nyimbo ngapi za injili hazina utukufu katika uchezaji wake au uimbaji wake na hazimjengi mtu katika imani?. Basi kasome tena utakutwa imeandikwa katika 2wakorintho 1:21 {kuna mtia mafuta mmoja ambaye ni MUNGU} kisha kasome 1Yohana2:20-28 utajua ni kwanini natamani ujae ROHO Mtakatifu hata hutasumbuka na kuchukia mafundisho wala wafundishao bali utajua kusudi lako ni nini juu yao. Pia kuna roho ya ibilisi imekaribia kuanza kuingia makanisani na itakuwa na nguvu sana nayo ni KUJICHORA{TATTOO} nakuonya mapema anza kuikemea sasa na kufundisha kuwa kujichora ni dhambi na mtu akijichora atengwe kabisaa bila kujali cheo chake wala karama yake usije, nimekuonya mapema wewe na kundi lako.
     by MICHAEL BASA 0765 279 698

Hakuna maoni

Inaendeshwa na Blogger.