Header Ads

KANISA LILOPOTEA

 
   Makanisa ni sehem nzuri sana ya kusanyiko kuonyana, kuelekezana, kufundishana na kutiana moyo katika njia ya BWANA. Lakini kanisa hilo pia linaweza kupotoka na kuacha kuweka mkazo kwa washirika kwenye safari ya kwenda mbinguni na kurukia mambo ya kidunia. Kuna makanisa yanapinga injili za kufanikiwa sijui wanatumia biblia gani?? Hebu soma torati 28:1-22 lakini rudia tena kuusoma msitari wa  12{hasa hapa………nawe utakopesha mataifa mengi, wala hutakopa wewe.} fikria kwa kina huu msitari. Je ulishawahi kumuuliza ROHO mtakatifu kuhusu kanisa lako juu ya huu msitari. Naye alikujibu nini?? Je alikujibu kuwa na mali ni anasa na je matajiri wote hawataenda mbinguni??
       2wakorintho 8:9 { Maana mmejua neema ya Bwana wetu Yesu Kristo, jinsi alivyokuwa maskini kwa ajili yenu, ingawa alikuwa tajiri, ili kwamba ninyi mpate kuwa matajiri kwa umaskini wake.}. je huu nao haupo kwenye biblia yako mtumishi wa MUNGU aliye juu??. Haijalishi wewe ni nabii au mwinjilisti kwangu hakuna tofauti kwamaana biblia yasema kila mtu na atuhesabu hivi tu watenda kazi pamoja na KRISTO. 
         Lakini katika kutenda kazi pamoja na KRISTO kumbuka kumtumia ROHO wake ili kutengeneza mambo yaliyopo na yajayo kwa usahihi zaidi. Kwamaana watu makanisa yameacha injili kamili ya KRISTO na kujikita kwenye magomvi ambayo yanamuudhi ROHO wa BWANA na kumpa ibilisi utukufu. Na kuna mmoja ambaye alianza katika ROHO naye kamalizia katika mwili. Kaligawa kanisa kati ya wallio nacho na wasiokuwa nacho.
        Ewe mwana wa laana ni nani aliyekupa ruhusa ya kugawa mafungu watu wa aliye juu kwa tamaa zako mwenyewe. Basi BWANA amekutaa wewe na wana wako na nyumba yako omboleza kwa tumbo na kwa utungu anza sasa. Lia wewe uliye nyamaza naamu kesha mavumbini hata asubuhi maana BWANA hatakuacha salama.
          Kuna mwingine aliyepotea yeye na kanisa lake lote hata dhambi imekuwa kitu cha kawaida kanisani. Mchungaji anatafuta injili ya kutafuta watu waongezeke lakini hawapi nafasi ya kukutana na kumjua ROHO MTAKATIFU. Hii siyo injili ambayo YESU aliitaka ihubiriwe na watu wake ni injili ambayo cha kwanza kitakuwa ni kuingia YERUSALEM MPYA na siyo kuimiliki dunia.
By MICHAEL BASA 0765279698

Hakuna maoni

Inaendeshwa na Blogger.