Header Ads

NANI ASIMAME AKEMEE ???.


 Nami nimeuona uovu juu ya madhabahu maana dhambi ya kipindi kanisa linakuja kwasasa haikemewi tena. Nani kasema kuwa Yesu kabadilika au sheria zimetanguka, kama mwanzo tulikemea kunyoa DENGE na tukaamini kuwa ni uhuni na pia haufai kanisani leo kimetokea nini isiwe dhambi tena?. Soma walawi 19:27 {You shall not round the corners of the hair of your heads nor trim the corners of your beard [as some idolaters do] kutoka kwenye AMP}.  Hiyo style ya kunyoa ya denge ilikuwa inatumiwa na waabudu sanam na pia tatuu inatumiwa na waabudu sanam kama alama ya kujisogeza kwnye ibada.Mfano kwenye makanisa ya sasa tunatumia nyimbo za kuabudu ili kujiweka tayari mbele za Mungu. Sasa wewe unayenyoa au unayetamani ujichore tatuu je unajua kwamba mawazo yako yameanza kukutoa kwenye kumwabudu au kumtumikia Mungu wa kweli nakuanza kuielekea miungu ambayo haitakupeleka mbinguni bali kuzimu. 
     Tazama tena kwa mabinti zetu nguo walizovaa makahaba miaka 1970 leo ndio zinavaliwa na waimbaji wa makanisa yetu . Mtoto wa mchungaji akifanya dhambi ni nani wa kukemea huo uasi. Sikia mbinguni hatuingii kwa vyeo vyetu ndani ya kanisa wala huduma zetu ndani ya kanisa hakika nakuambia BASA MINISTRY haitanipeleka mbinguni bali UTAKATIFU ndio utanipa kibali cha kukutana na Bwana wangu. Waumini wameanza kuchagua mafundisho ya kushika wakati biblia ni moja wewe usiye na akili ni nani aliye kuroga wainjilisti wamesema wazi na kukemea wazi mbele zako nawewe ukainua kimdomo chako kumsema vibaya pole sana. Kwamaana wafanya vita na Bwana mwenyewe nawe hutaokoka kwa mawazo yako maovu wala kujihesabia haki kwako. 
   Ni nani kati ya mabinti zetu aliyetaka kununua kimini akaammua kufunga na kuomba kwaajili ya kupata maono na ruhusa ya Roho mtakatifu na baada ya kupata jibu akashirikisha mwingine zaidi kwenye kuomba maono kuwa Roho analionaje hilo vazi?. Vijana wa kanisa nao hawako nyuma kwa msemo wa modo zao nguo inabana kila sehem. Mwanzo wanawake walivaa kuamsha hisia{lust} za wanaume je kijana wa kiume unaamsha hisia za nani?. Je unajua madhara ya kutumika kwenye kitu ambacho mwanzilishi{author} wake siyo Mungu?. 
    Nakuambia acha kuiga iga vitu ovyo tamani kwanza kujazwa Roho mtakatifu kisha ipeleke injili kwa jinsi ulivyoitwa tamaa za mwili huwezi kuzikamilisha milele mpenzi wangu nikupendaye na pia shetani ni mdanganyifu sana wewe jisifu kwa Amani yenye mapengo mapengo na roho yako mwenyewe imechoka na haiwezi kumuona MUNGU. 

By MICHAEL BASA 0765 279 698

Hakuna maoni

Inaendeshwa na Blogger.