Header Ads

HUYU MUNGU NI BABA

Bwana wewe ni nguvu na ngome kwangu ahadi zako ni za milele kwangu umeniinua juu ya mataifa nawe umekuwa mji wa nguvu moyoni mwangu mataifa sikieni nanyi mkaweke ushuhuda mioyoni mwenu “Heri walio kamili njia zao, Waendao katika sheria ya Bwana”. Tena ni “Heri wazitiio shuhuda zake, Wamtafutao kwa moyo wote.Naam, hawakutenda ubatili, Wamekwenda katika njia zake”. Bwana Mungu wangu anawapenda watu hao nao kamwe hawatakuwa makapi mbele za adui zao maana Bwana yeye atawashindia vita na wao milele watakuwa washindi. Je wachamungu wametaabika mioyoni mwao na nyongeza zimeteka ufahamu wao sikieni leo niwakumbushe fadhili za Bwana zilizo za milele tena aliahidi hatakuacha enyi mtangao je hamkusoma imeandikwa “Msisumbuke, basi, mkisema, Tule nini? Au Tunywe nini? Au Tuvae nini?. Kwa maana hayo yote Mataifa huyatafuta; kwa sababu Baba yenu wa mbinguni anajua ya kuwa mnahitaji hayo yote. Bali utafuteni kwanza ufalme wake, na haki yake; na hayo yote mtazidishiwa.”. Je hamkuamini kwa neno la injili nalo ni hili yeye aketiye mahali palipoinuka ametuamru kuyashika mausia yake Ili sisi tuyatii sana. Neno langu naomba kibali mbele zako Bwana nalo ni hili “Ningependa njia zangu ziwe thabiti, Nizitii amri zako.Ndipo mimi sitaaibika, Nikiyaangalia maagizo yako yote.Nitakushukuru kwa unyofu wa moyo, Nikiisha kujifunza hukumu za haki yako”. Kwa maana Hakuna mtu aliyeacha nyumba, au ndugu waume, au ndugu wake, au mama, au baba, au watoto, au mashamba, kwa ajili ya Injili, akapata hasara bali atapewa mara mia sasa wakati huu, nyumba, na ndugu waume, na ndugu wake, na mama, na watoto, na mashamba, pamoja na udhia; na katika ulimwengu ujao uzima wa milele.

Hakuna maoni

Inaendeshwa na Blogger.