Header Ads

KWA KILA DINI

kwa kila dini
 Wote tunajua kua tumbo la mwanamke limeumbwa kiasi kwamba damu ya mama hai-ingiliani na damu ya mtoto aliye tumboni mwake. Hili ni jambo la kisayansi na ndio maana mama mwenye virusi vya ukimwi anaweza kuzaa mtoto asiye na virusi kama hakutatokea mchubuko kwa mtoto wakati wa kujifungua. Na wote tunajua kuwa MUNGU anajua mwanzo na mwisho wa kila kitu. Kwahiyo ni kweli MUNGU alijua kuna siku Adam atafanya uasi na kutenda dhambi.
Na MUNGU siku zote anaziheshimu sheria zake; Na katika uumbaji wake aliweka sheria ya urithi. Yaani kila binadamu anaezaliwa kwa muunganiko wa sperm cell na egg cell lazima arithi sifa za mama na baba (heredity). Kwahiyo kwa njia ya urithi, dhambi iliingia ulimwenguni kupitia kwa mtu mmoja yaani Adam. Na kupitia dhambi hii, mauti ikawafikia watu wote, kwani kwa njia ya urithi, wote wamefanya dhambi hata kama hawakutenda dhambi kama Adam.
Baada ya dhambi kuingia ulimwenguni… Siku ileile MUNGU alikuja na mpango mwingine akasema Mwanzo.3:15 “nitaweka uadui kati yako (shetani) na huyo mwanamke, na kati ya uzao wako na wake, huo atakuponda kichwa, nawe utamgonga kisigino. Na haya maneno ni ya kinabii ambayo Kwa tafsiri ya neno “kichwa”ni utawala na “kugonga kisigino” ni majaribu, mateso au taabu
Ukiangalia vizuri…mwanaume hajahusishwa kwenye huo mpango, bali ni mwanamke peke yake; Kwani MUNGU anasema, “nitaweka uadui kati yako (shetani) na huyo mwanamke”. Kwahiyo ni kwa uzao wa mwanamke tuu bila ya kuhusisha mwanaume. Na kwa njia hii lazima mwanamke awe bikira.
Lakini hata kisayansi yai pekee haliwezi kutunga mimba bila ya Sperm cell. Kwa njia hii pia hata yai halikuhusishwa kutunga mimba. Kwahiyo mwanamke anakuwa incubator tu; kwa ajili ya kukuza mtoto atakae-fanywa kwenye tumbo lake kwa nguvu za MUNGU. Na kwasababu damu ya mama na mtoto hazichangami… mtoto anaezaliwa anakua nje ya dhambi ya asili ya urithi (sinless).
Kwa njia hiyo mtoto anaezaliwa sio mtoto wa mwanadamu, kwani hajahusisha yai wala mbegu ya mwanadamu. Bali kwa uwezo wa Nguvu za MUNGU, mwili unafanyika kwenye tumbo la mwanamke, na mwanamke anakua incubator kwa huyo mtoto. Na kwasababu ni MUNGU ndiye aliefanya hivyo… basi mtoto anaezaliwa anaitwa “Mwana wa MUNGU”. Hata MUNGU alisibitisha akasema “Huyu ni Mwanangu mpendwa, ambaye ninapendezwa sana naye” mathayo.3:17’’ na tazama, sauti kutoka mbinguni ikisema, Huyu ni Mwanangu, mpendwa wangu, ninayependezwa naye.’’ Mtu kuzaliwa na bikra ndio ishara ambayo hakuna nabii au mtume kutoka dini yoyote aliyeishi hapa duniani alienayo. Nabii Isaya alitabiri; Bwana mwenyewe atawapa ishara: Bikira atachukua mimba, naye atamzaa mwana
Sasa kwakuwa dhambi iliingia ulimwenguni kupitia kwa mtu mmoja (Adam), na mauti ikawafikia watu wote, kwa sababu kwa njia ya urithi wote wametenda dhambi; Vivyo hivyo kwa kupitia mtu mwingine mmoja, ambaye yupo kama Adam kabla ya dhambi watu wote wanasamehewa dhambi zao na kupata uzima wa milele. (Warumi.8:12-21)
Kama vile dhambi ilivyoingia kwa Mwana wa MUNGU mmoja yaani Adam (Adam hakutokana na muunganiko egg na sperm cell), hatimae watu wote wa egg+sperm cell wakawa na dhambi na mauti… basi tena kwa kupitia mwana mwingine wa MUNGU yaani YESU, dhambi inaondolewa kwa hao watu wote na hivyo uzima wa milele (luka.3:23-38)
INAKUWAJE YESU MWENYE HAKI ASULUBIWE?
Kwamaana imeandikwa “Mtu mwenye haki huokolewa kutoka katika taabu, nayo huja kwa waovu badala yake(Mithali.11:8). Wote tunajua kua Kitendo cha mtu mwenye haki kuamua kupoteza kitu chake cha thamani kwa kupenda, kwa ajili ya kumuokoa yule asie na haki huitwa “sacrifice”.
Sasa sheria hiyo inatimizwa hivi; Huyu mtu mwenye haki (YESU), asiye na dhambi na ambae hawezi kufa kwasababu yuko nje ya dhambi ya Adam… anaitoa haki yake kwa hiari kwenda kwetu, tena alitupatia baraka zake, na kupokea unajisi, na laana zetu zote. Kwani kwenye torati imeandikwa “amelaaniwa yeye aangikwae juu ya mti” Na baada ya kua najisi, Roho wa MUNGU akamuacha hadi yeye akalia “MUNGU wangu MUNGU wangu mbona umeniacha?” kwa mabadilishano hayo… waovu (wengi) wakawa wenye haki, na mmoja mwenye haki akawa mwovu. Kwahiyo Watu (wengi) wenye haki huokolewa kutoka katika taabu (kusulubiwa/mauti), nayo hiyo taabu huja kwa mwovu mmoja (YESU) badala yao.


Mwandishi: IBRAHIM NZUNDA 0754 210 627

Hakuna maoni

Inaendeshwa na Blogger.