Header Ads

KANISA KAMA MAKABURI YALIYOPAMBWA KWA NJE NA WAKATI NDANI YAMEJAA MIFUPA NA VITU VILIVYOOZA.

welcome to basaministry
CHRIST’S GOSPEL INTERNATIONAL MINISTRIES..
    Hii si kumwabudu Mungu bali ni kujifariji, kukimbiza upepo, kujidanganya na kudanganyika kupoteza muda bilakujielewa na kutembea katika giza ndani ya nuru. “na hii ndiyo hukumu ya kuwa nuru imekuja ulimwenguni na watu wakapenda giza kuliko nuru kwa maana matendo yao yalikua maovu” Yoh 3:19.
     Nani kakudanganya kuwa kanisa ni jengo? Hivyo kuingia kwako katika majengo hayo nawe umekua sehemu ya kanisa!!! Kanisa ni mwili wa Kristo yaani wa YESU na hujengwa na watu watakatifu waingiao mahekaluni. Jiulize  je, wewe ni mtakatifu? Je wewe ni sehemu ya mwili wa Kristo? Au unaenda hekaluni kujaza viti na kuuza sura? “Naye ndiye kichwa cha mwili yaani cha kanisa….” Wakolosai 1:18-19.
     Hakuna kitu kibaya kama unafiki,umefika mbali sana maana hata Mungu unampaka mafuta kwa mgongo wa chupa? Kumuonyesha mchungaji kuwa muumini wake wakati wewe ni mtenda dhambi haina msaada kwa roho yako. Yesu mwenyewe anawachukia sana wanafiki kama wewe unayejidanganya kuwa mtu wa rohoni wakati wewe ni wa dhambini. “ole wenu waandishi na mafarisayo wanafiki! Kwa maana mmefanana na makaburi yaliyopakwa chokaa nayo kwa nje yanaonekana kuwa ….bali ndani yamejaa mifupa na uchafu wote” Mathayo 23:27-33. Mstari wa 33 “enyi nyoka wana wa majoka, mtaikimbiaje hukumu ya jehanamu?”
    Acha kuidanganya roho yako ubadilike kuanzia leo maana matendo unayofanya si ya ki MUNGU bali ya kishetani kabisa. Unaenda hekaluni kwa lengo la kujulikana tuu na si kwenda mbinguni, badilika sasa maana Yesu yu karibu kurudi “tubuni kwa kua ufalme wa Mungu umekaribia” Mathayo 3:2.
    Hayo uyafanyayo kwa siri ni matendo ya mwili na watu kama wewe wamewekwa akiba kwa ajili ya ziwa liwakalo moto yaani jehanamu pamoja na baba yao Shetani au Ibilisi. “basi matendo ya mwili ni dhahiri ndiyo haya uasherati, uchafu, ufisadi, ibada ya sanamu, uchawi, uadui, ugomvi, wivu, hasira, fitina, uzushi, husuda, ulevi, ulafi, na mambo yanayofana na hayo….ya kwamba watu watendao mambo ya jinsi hiyo hawataurithi ufalme wa mungu” Wagalatia 5:19-21. “bali waoga na wasioamini na wachukizao na wauaji na wazinzi na wachawi na hao waabudio sanamu na waongo wote, sehemu yao ni katika lile ziwa liwakalo moto na kiberiti….” Ufunuo 21:8.
    Sikia nikupe maarifa ya kiMungu haya yote unayafanya na unasema umeokoka muongo acha mara moja;
1.       Wewe ni mzinzi mpaka umekua kero kwenye nyumba za majirani zako. (UTAKUFA NA UKIMWI)
2.       Unavaa nguo za wadogo zako au zilizo kuruka hakuna anayependa kukuona ukiwa uchi  (UMEKUWA KAMA MDORI)
3.       Unavaa suruali kata kei(chini ya kiuno chako) kama hauna mgongo…………..Mmh
4.       Lugha yako si Kiswahili wala kiingereza bali ni matusi acha mambo hayo.
5.       Unaishi na wasiwasi kama unakufa kesho, si mpango wa MUNGU ni wa shetani huo.
      Hivyo ni baadhi ya vitu uvifanyavyo na bado unajiita MLOKOLE na unesema utafika mbinguni. Mbinguni si rahisi kuingia kama unavyodhani  badilika dada na kaka yangu.
Yesu anasema hakuja kwa ajili ya wachungaji, wainjilisti, mashemasi bali kwa ajili ya mwenye dhambi kama wewe “Sikuja kuwaita wenye haki bali wenye dhambi wapate kutubu” Luka 5:32. Nafasi ya kutubu na kusamehewa ipo kwa ajili yako “tazama nasimama mlangoni, nabisha,mtu akisikia sauti yangu na kufungua mlango nitaingia kwake nami nitakula pamoja naye na yeye pamoja nami.
       Kama unashindwa kuacha dhambi na unasumbuliwa na shida yoyote nitafute na YESU atakuweka huru mbali na dhambi kabisa.
TO THE LORD BE THE GLORY.
PRERARED BY FOUNDER  BUNGUBULIHO F.M Phone 0755285414 or 0716453335

WELCOME IN THE FAMILY OF JESUS CHRIST. Forwarded by BASA MINISTRY.

Hakuna maoni

Inaendeshwa na Blogger.