Header Ads

KUUSHINDA ULIMWENGU

kuushinda ulimwengu
Yesu kristo aliwahi kusemajuu ya kujipa moyo kwa mtazamo wa kuwa kila kitu cha ulimwengu ni wale wa ufuatao ulimwengu na tamaa zake nao huwapenda na kuwafurahia bali kwa wale wasioupenda au wanaoenda kinyume nao huwachukia na kutamani wasiwepo bali yesu anasema JIPENI MOYO kwamaana nyingine njia uliyoishika haiwezi kuwa katika wepesi wa maisha yako bali kwamaana yeye anayeenda kinyume na ulimwengu huu yeye anakuwa si wa ulimwengu huu yohana 8:23( Akawaambia, Ninyi ni wa chini, mimi ni wa juu; ninyi ni wa ulimwengu huu, mimi si wa ulimwengu huu.)kwa hiyo kama wewe si ulimwenguu huu hauwezi kuyatenda mapenzi ya ulimwengu huu ambayo dhahiri ni matendo ya mwili wala si ya ROHO ambayo yapo wagalatia 5:( 19 Basi matendo ya mwilinidhahiri, ndiyo haya, uasherati, uchafu, ufisadi,
 20 ibada ya sanamu, uchawi, uadui, ugomvi, wivu, hasira, fitina, faraka, uzushi,
 21 husuda, ulevi, ulafi, na mambo yanayofanana na hayo, katika hayo nawaambia mapema, kama nilivyokwisha kuwaambia, ya kwamba watu watendao mambo ya jinsi hiyo hawataurithi ufalme wa Mungu.)
 Ukiyasoma hayo matendo mengi yanapendwa na watu wa ulimwengu huu lakini ni matendo ambayo kwayo huwezi kuurithi ufalme wa mbinguni . hebu tazamo jinsi tunavyokaa sisi na marafiki zetu jinsi wanavyotushauri je ni mambo ambayo yanatupeleka mbinguni au ni yale ambayo yanatuondolea utakatifu.Na piindi ukiyakataa unaonekana mshamba usiyejua kitu au wa ajabu sana. Namimi nakushauri jipe moyo maana MUNGU aliyetupenda kwaajili yetu akamtoa mwanawe wa pekee ili afe na afanyike ondoleo la dhambi kwwetu yupo karibu zaidi na kwa upendo wake usiokoma. Sisi hatukumpenda yeye bali yeye ndo alitupenda sisi na hakika YESU alipoondoka hakutuacha  tutange tange(kama yatima)bali alituachia ROHO wa MUNGU akae na hao watakaopokea na kuamini INJILI yake yohana 14:( 16 Nami nitamwomba Baba, naye atawapa Msaidizi mwingine, ili akae nanyi hata milele;
 17 ndiye Roho wa kweli; ambaye ulimwengu hauwezi kumpokea, kwa kuwa haumwoni wala haumtambui; bali ninyi mnamtambua, maana anakaa kwenu, naye atakuwa ndani yenu.
 18 Sitawaacha ninyi yatima; naja kwenu.)
yohana 16:(33 Hayo nimewaambieni mpate kuwa na amani ndani yangu. Ulimwenguni mnayo dhiki; lakini jipeni moyo; mimi nimeushinda ulimwengu.)

Mwandishi MICHAEL BASA(0765 279 697,+255 789 799 199)

Hakuna maoni

Inaendeshwa na Blogger.