Header Ads

IJUE MILANGO YA KUVUKA KABLA HAUJAFA

1)KUIACHA DUNIA
Hii hutokea pindi mtu anapookoka ni kipindi ambacho mtu anatakiwa kuacha starehe za kidunia alizokuwa anafanya pindi ambapo hajamjua MUNGU (non believer) mf uvutaji sigara,ulevi , wizi, uasherati nk
 ufunuo 22: 15
 mathayo 25:17-25
 waolosai 3:5
husumbua sana kwasababu mtu anakuwa katika kipindi cha kugeuka ili kumwelekea MUNGU (translation period) ambayo bado loop yake inakuwa haijavunjika

CHA KUFANYA ILI KUMUOKOA/KUVUKA HUU KWENYE HUU MLANGO
• Kanisa kumuombea yakobo 5:15-16
• Kufanya juhudi katika kuomba wakolosai4:2
• Kusoma biblia kila siku zaburi 1:6
• Kushikamana na watakatifu na kukaa nao karibu

2)KUIKATALIA DUNIA KURUDI MOYONI MWAKO
mtu anakuwa kafanikiwa kuiacha dunia na mambo yake lakini watu awanaomzunguka wanakuwa bado wanamhitaji arudi kuziba pengo na hii huweza hata kusababisha mtu kutengwa na marafiki au hata kutengwa na ndugu
vitu vya kufanya ili kuuvuka huu mlango
• Kujitoa kwa ajili ya MUNGU mathayo16:24,luka9:23,marko 8:34
• Kujitahidi kusahau mabaya yote uliyowahi kutenda na kushikamana na makuu ya MUNGU tu zaburi 60:12, waefeso 2:4
• Kazana kupata zaidi karama za rohoni 1wakorinto 12
• Jaza neno kwa wingi na pia fundisha wengine luka8:39

3) KUITENDA KAZI YA MUNGU
Hili ni moja la eneo ambalo waumini wengi wamefungiwa ambalo uoga wa kutenda kazi ya MUNGU, aibu ya kusimama na kujitangaza kama mlokole pia watu huridhika na kuingia na kutoka makanisani na pia kuzidi kwa kujihesabia haki pasipo kuitenda wala kuitimiza mathayo3:15
Bila kusahau kuwa milango yote unaweza kuivuka lakini huu kuuvuka ni mpaka pale utakapokufa na hakuna kitu Zaidi ya kushikamana na haki ya MUNGU kujitoa kwa kazi ya MUNGU kwa kutangaza injili kwa kipaji ulichopewa na MUNGU marko16:15

JINSI YA KUDUMU NA MUNGU KATIKA HUU MLANGO
• Kudumu na ahadi za MUNGU
• Kufanya jitihada za kuwa na nguvu kwenye ufalme wa mbingu marko12:20 mathayo 11:112
• Kujitahidi kila siku kukuza karama yako 1petro 4:10
• Kujiepusha na makatazo yote pia kujitunza katika ukamilifu wa BWANA warumi 14:16 efeso5:3
• Kujizoeza kupata utauwa(exercising godliness)1timotheo 4:7
• Kushindana na roho za aibu,kukata tamaa,kinyongo,wivu ,majivuno ,na tamaa za aina zote titus 2:7 ufunuo 21:8
• Kuwaombea watakatifu wote walioko duniani wazidi katika Imani na utauwa Waefeso 6:18
• Kutoridhika na hatua uliyofikia wafilipi 3:12
• Kuyafanya maisha yako yawe ya mfano wa ki MUNGU 1petro 1:15 waefeso5:3
Mwandishi MICHAEL BASA 0765 279 698, +255 789 799 199

Hakuna maoni

Inaendeshwa na Blogger.