Header Ads

TUJUE KUUWEZA MWILI

Mtu ni roho inayomiliki nafsi. Na mtu huyu akiwekwa ndani ya nyumba ya udongo yaani mwili anakuwa nafsi hai. (mwanzo 2:7). Binadamu nae yupo katika utatu yaani roho, nafsi na mwili. Kama ilivyoandikwa katika 1wathesalonike 5:23 “Mungu wa amani mwenyewe awatakase kabisa; nanyi nafsi zenu na roho zenu na miili yenu mhifadhiwe mwe kamili”(UTATUWA MWANADAM PITIA HAPA)
Yaani kama vile mwili unavyomiliki  "kichwa" vivyo hivyo  roho nayo inamiliki "nafsi".  Kama vile kichwa chako na mwili vyote ni of the physical... vivyohivyo nafsi na roho vyote ni vya kiroho (ndio maana mtu akifa hajisahau yeye ni nani ingawa anaiacha "brain" yake kaburini).. (angalia luka.16:19-31)
Kwahiyo MWILI NI JUMBA LILOTENGENEZWA  KWA UDONGO ili KUTUNZA PUMZI YA UHAI (roho yako). Ndio maana mtu akifa maana yake ni kwamba roho yake inakuwa imeachana na mwili. Hivyo ukiomba mtu afufuke inamaana unairudisha roho yake katika mwili wake. Kama ilivyoandikwa “mwili pasipo roho umekufa (yakobo.2:26)”
Na kwakuwa mtu ni roho na sio mwili. Kinachoitwa “Mwana wa Mungu” sio mwili bali ni roho yako wewe. Na kwasababu roho yako haina asili ya kutenda dhambi imeandikwa “mtu aliyezaliwa na Mungu hatendi dhambi, kwa sababu uzao wake wakaa ndani yake; wala hawezi kutenda dhambi kwa sababu amezaliwa kutokana na Mungu (1yoh 3:9)”
Lakini kumbuka kuwa binadamu anazaliwa akiwa na asili ya dhambi katika roho na mwili wake. Sasa mtu anapookoka mwili wake huchukuliwa na kusulubiwa pamoja na Yesu pale msalabani. Kama ilivyoandikwa “hao walio wa Kristo Yesu wameusulibisha mwili pamoja na mawazo yake mabaya na tamaa zake(gala.5:24)”.
Sasa pamoja na kwamba mwili unakuwa umesulibiwa lakini asili yake ya dhambi haitolewi katika mwili ila unakuwa umesulubiwa tu pamoja na Yesu pale msalabani. Ndio maana bado miili hii inazeeka na inakufa kwasabu ya ile asili ya dhambi ndani yake iletayo mauti. Imeandikwa “nia ya mwili ni mauti; bali nia ya roho ni uzima na amani. Kwa kuwa ile nia ya mwili ni uadui juu ya Mungu, kwa maana haitii sheria ya Mungu, wala haiwezi kuitii”war8:6-7
 Kwa jinsi hii tunaona kuwa mwili waweza kutenda dhambi na hauwezi kutii sheria kwani bado unayo asili ya dhambi.  Na kwa muda huohuo roho yako haitaki kutenda dhambi kwani haiwezi kutenda dhambi kwasababu haina asili ya dhambi. Kama ilivyoandikwa “mwili hutamani ukishindana na roho, na roho kushindana na mwili; kwa maana hizi zimepingana, hata hamwezi kufanya mnayotaka (gal.5:17)” na tena imeandikwa “Wapenzi, nawasihi kama wapitaji na wasafiri, ziepukeni tamaa za mwili zipiganazo na roho.(1pet.2:11)
Kwa hiyo tamaa za mwili na matendo ya kimwili yako tofauti na  ya roho yako ndani yako
JE MATENDO YA MWILI NI YAPI SASA?
WAGALATIA 5:
19 Basi matendo ya mwili ni dhahiri, ndiyo haya, uasherati, uchafu, ufisadi,
 20 ibada ya sanamu, uchawi, uadui, ugomvi, wivu, hasira, fitina, faraka, uzushi,
 21 husuda, ulevi, ulafi, na mambo yanayofanana na hayo, katika hayo nawaambia mapema, kama nilivyokwisha kuwaambia, ya kwamba watu watendao mambo ya jinsi hiyo hawataurithi ufalme wa Mungu.
Na kwa upande wa roho ni
WAGALATIA 5:

Na matendo/tunda la roho ni lipi?
22 Lakini tunda la Roho ni upendo, furaha, amani, uvumilivu, utu wema, fadhili, uaminifu,
 23 upole, kiasi; juu ya mambo kama hayo hakuna sheria.

JE KUNA UHUSIANO WOWOTE KATI YA MWILI NA KUMTUMIKIA MUNGU????
NDIYO UPO
1WAKORINTHO 6:19; Au hamjui ya kuwa mwili wenu ni hekalu la Roho Mtakatifu aliye ndani yenu, mliyepewa na Mungu? Wala ninyi si mali yenu wenyewe
Kwa hiyo mwili ni hekalu la ROHO mtakatifu tuliyepewa na MUNGU lkn matendo ya mwili hayapo katika kumpendeza MUNGU
WARUMI 8:7.
8 Wale waufuatao mwili hawawezi kumpendeza Mungu.
Kumbe ili kumpendeza  MUNGU inabidi mtu asiiufuate mwili je njia zipi za kutoufuta mwili
KUMKIRI YESU
WAGALATIA 5; 24
WARUMI 8:10 Na Kristo akiwa ndani yenu, mwili wenu umekufa kwa sababu ya dhambi; bali roho yenu i hai, kwa sababu ya haki.

KUISHI KWA KUIFUATA roho/ROHO
WARUMI 8: 6 Kwa kuwa nia ya mwili ni mauti; bali nia ya roho ni uzima na amani.
9 Lakini ikiwa Roho wa Mungu anakaa ndani yenu, ninyi hamwufuati mwili; bali mwaifuata roho. Lakini mtu awaye yote asipokuwa na Roho wa Kristo, huyo si wake.
WAGALATIA 5;25 Tukiishi kwa Roho, na tuenende kwa Roho.
KUTOUFUATA MWILI
WARUMI 8:5 Kwa maana wale waufuatao mwili huyafikiri mambo ya mwili; bali wale waifuatao roho huyafikiri mambo ya roho.
1PETRO1: 24 Maana, Mwili wote ni kama majani, Na fahari yake yote ni kama ua la majani. Majani hukauka na ua lake huanguka;
2PETRO2: 9 basi, Bwana ajua kuwaokoa watauwa na majaribu, na kuwaweka wasio haki katika hali ya adhabu hata siku ya hukumu; 10 na hasa wale waufuatao mwili katika tamaa ya mambo machafu. na kudharau mamlaka.
KUJUA DHUMUNI LA MUNGU JUU YA MWANADAM
1WATHESALONIKE4: 3 Maana haya ndiyo mapenzi ya Mungu, kutakaswa kwenu, mwepukane na uasherati;
1WAKORINTHO 6: 20 maana mlinunuliwa kwa thamani. Sasa basi, mtukuzeni Mungu katika miili yenu.
KUJUA KUUWEZA MWILI
1WATHESALONIKE 4: 4 kila mmoja wenu ajue kuuweza mwili wake katika utakatifu na heshima; 5 si katika hali ya tamaa mbaya, kama Mataifa wasiomjua Mungu.

Mwandishi;  Michael BASA              0765 279 698, +255 789 799 199

Mhariri;       IBRAHIM J. NZUNDA  0754 210 627

Hakuna maoni

Inaendeshwa na Blogger.