Header Ads

NI NYAKATI ZA HATARI SANA!

Shalom:Ingawa watu wengi wanadharau suala hili la kweli; Lakini mjue jambo moja kama ilivyoandikwa “Wakati wasemapo, Kuna amani na salama, ndipo uharibifu uwajiapo kwa ghafula, kama vile utungu umjiavyo mwenye mimba, wala hakika hawataokolewa”. Tena ingawa hakuna ajuae SIKU wala SAA; lakini tumepewa uwezo wa kutambua majira na nyakati za kuja kwake. Kama Yesu alivyosema, “myaonapo mambo hayo yanaanza, tambueni ya kuwa yu karibu milangoni”. (marko.13:28-29)
Ndugu zangu Dunia inielekea mwishoni maana kila dalili na mambo yaliyoandikwa yanatimia sasa, Niajabu sana kuona kuwa watu wanaendelea kufanya mambo mabaya bila kufahamu kuwa dunia inarudi kipindi cha SODOMA NA GOMOLA INCHI ILE ILIYOCHOMWA MOTO NA KIBERITI (Mwanzo 19:24).
Nimaajabu makubwa kwamba wanyama wote wanatambua majira na nyakati chini ya jua lakini mwanadamu aliyeumbwa kwa mfano wa Mungu hatambui wala haelewi kinacho-endelea chini ya jua. “Ng'ombe amjua bwana wake, Na punda ajua kibanda cha bwana wake; Bali Israeli hajui, watu wangu hawafikiri” (Isaya 1:3).
Sikia haya yanayofanyika duniani leo na mengine hata wewe huenda unayafanya,, Wasomi watembea nusu utupu na kupigapicha za utupu, Ndoa za jinsia moja zimehalalishwa, wadada kutoa mimba kanakwamba wanatoa taka mwilini, Mauwaji ya kutisha na ugaidi kila kona,dhuruma na ufisadi mkubwa sana, Usaganaji, ushoga na ufilaji mchafu, mziki na ngoma za uchi maeneo mbalimbali. TUSIJIFANYE HATUNA AKILI, HAYA YOTE YAMETAJWA KWENYE BIBLIA NA NDIO DALILI ZENYEWE
ufahamu neno hili, ya kuwa siku za mwisho kutakuwako nyakati za hatari. Maana imeandikwa “watu watakuwa wenye kujipenda wenyewe, wenye kupenda fedha, wenye kujisifu, wenye kiburi, wenye kutukana, wasiotii wazazi wao, wasio na shukrani, wasio safi, wasiowapenda wa kwao, wasiotaka kufanya suluhu, wasingiziaji, wasiojizuia, wakali, wasiopenda mema, wasaliti, wakaidi, wenye kujivuna, wapendao anasa kuliko kumpenda Mungu; wenye mfano wa utauwa, lakini wakikana nguvu zake;...” (2Timotheo 3:1).
Jiulize maswali yafuatayo:
 Toka umeanza kufanya UZINZI umepata nini cha kumwonesha YESU atakaporudi?
 Kwa nini huwapendi watu wanaomwabudu Mungu katika roho na kweli! Shituka ndugu
 JE ukifa bila kumwamini Yesu mwenye uzima wa milele, UKAMKUTA HUKO utaweza kuvumilia Moto wa JEHANAMU? GEUKA Mwanadamu
 Pamoja na dini yako umeweza kuacha dhambi na hasa hasa dhambi ya kizazi hiki ya UZINZI na UCHAWI?
 JE unajua kuwa wewe ni mtumwa wa dhambi na hivyo imekupa kibali cha kuwa mtoto wa SHETANI na hivyo ukifa bila kumwamini YESU unakwenda MOTONI?
 JE wewe uliye jificha kwenye nyumba za ibada unazani MUNGU hakuoni!!!!!!!!!!!!!!! YESU amekuona ACHA LEO YESU AKUSAMEHEEEEEEE....
 Je wewe ni shoga mbona unavaa Nguo zilizo legezwaaa? na we MSICHA mbona hizo nguo zimekuluka? acha kuzizaa unajiabisha halafu zinaonesha KUWA UNA MAPEPO YA UZINZI NA UMALAYA.
Ukiyajua haya, niheli uachane na njia yako mbaya ya UZINZI,UMALAYA, ushilikina, matusi NA MENGINE, na kumpokea YESU ili awe Bwana na Mwokozi wa maisha yako. Bwana asema “Amwaminiye yeye hahukumiwi; asiyeamini amekwisha kuhukumiwa...” tena imeandikwa “ukimkiri Yesu kwa kinywa chako ya kuwa ni Bwana, na kuamini moyoni mwako ya kuwa Mungu alimfufua katika wafu, utaokoka. Kwa maana kwa moyo mtu huamini hata kupata haki, na kwa kinywa hukiri hata kupata wokovu. (Warumi 9:9-10).
 pakua pdf hapa

PREPARED BY BUNGUBULIHO M. FREDRICK , 0755-285-414

Hakuna maoni

Inaendeshwa na Blogger.