Header Ads

JE, YESU NI MUNGU?

Ndugu Msomaji habari!.

Tunajuwa kuwa MWANGA una asili mbili (dual nature) kwa pamoja ambazo haziingiliani na wala hazitengani. 

"Mwanga ni wave na vilevile ni particle." Na wave ni immaterial lakini particle ni material. 

Na mwanga unazo sifa zote za wave yaani diffraction, refraction, interference n.k. Pia mwanga anazo sifa zote kama particle na tuna-utumia kutengeneza umeme wa Jua (sola power). (kumbuka de Broglie wave-particle duality).

Sasa Yesu amesema kuwa yeye ni MWANGA (LIGHT).
Alikuja duniani katika umbo la binadamu na akawa binadamu kamili (i.e. particle) na sifa zote, wala hakuwa fake, kwani Mungu hatengenezi fake. Ndiyo maana Yesu anasema “hakuna mtu ye yote aliye mwema ila Mungu peke yake” na alilia “Mungu wangu Mungu wangu, mbona umeniacha?” (KUHUSU U-MUNGU NIMEANDIKA AYA ZA CHINI).


Ndio maana imeandikwa “Kwa maana ikiwa kutokana na kosa la mtu mmoja, mauti ilitawala kupitia huyo mtu mmoja, zaidi sana wale wanaopokea wingi wa neema ya Mungu na karama Yake ya kuhesabiwa haki, watatawala katika uzima kwa njia ya huyo mtu mmoja, yaani, Yesu Kristo”(warumi.5:12-19, 1korintho.15:20-22).

LAKINI kwa sababu ana-asili mbili… yote haya hayamfanyi Yesu asiwe Mungu. 

Yesu alipoulizwa “Bwana, tuonyeshe Baba yako yatosha”…Yesu akajibu “Filipo, nimekaa nanyi muda huu wote hata usinijue?” (yohana.14:9-10). 

Huyu ndiye Yesu ambea pia ni Mungu na aliyesema

“tazama, naja upesi, na ujira wangu u pamoja nami, kumlipa kila mtu kama kazi yake ilivyo. Mimi ni Alfa na Omega, mwanzo na mwisho, wa kwanza na wa mwisho.(ufunuo.22:12-13)

Pia imeandikwa
“kwa ajili yetu mtoto amezaliwa, tumepewa mtoto mwanamume, nao utawala utakuwa mabegani mwake. Naye ataitwa: Mshauri wa Ajabu, Mungu Mwenye Nguvu, Baba wa Milele, Mfalme wa Amani (Isaya.9:6). 

Na pengine imeandikwa 
“Hapo mwanzo, alikuwako Neno, Huyo Neno alikuwa pamoja na Mungu, naye Neno alikuwa Mungu” 
na inamalizia kwa kusema
“Neno alifanyika mwili, akakaa miongoni mwetu, nasi takauona utukufu Wake. (yohana.1:1-14, 17:4-5, wafilipi.2:6-11). 

Bwana akubariki sana. AMEN

Imeandikwa na IBRAHIM J. NZUNDA (0754 210 627)

 – kupata softcopy Ya Somo Hili Bonyeza Hapa || Kupata SoftCopy Zote Bonyeza Hapa

Hakuna maoni

Inaendeshwa na Blogger.