Header Ads

NINI CHA KUFANYA BAADA YA KUANGUKA?

kumbuka kwamba BWANA ni mwingi wa hasira na hakuna hata mmoja awezaye kusimama hata sekunde moja kuikabili hasira yake, naye ni mwenye nguvu nyingi na utukufu. Pia ni mwepesi wa kusamehe ndo maana mpaka leo unaona ni kwa neema tu watu tunaishi
ukisoma Yoeli 2:12-13; BWANA wa majeshi anaonesha ni jinsi gani ambavyo anaitunza hasira yake juu yako na anasema umrudie kwa:

1. MOYO WAKO WOTE - MUNGU ni roho, na imetupasa tumwabudu katika roho na kweli (Yohana 4:24). Kwa maana nyingine naweza sema kwamba BWANA wetu anataka mioyo yote mda wote ikae ikimwelekea yeye kwa kumuwaza na neno lake ndo lijaze mioyo yetu (Mithali 4:23)

2. KWA KUFUNGA- Na kwa jinsi hii unaua tamaa za mwili na kuiacha njia mbaya uliyoiendea ili ukadumu katika uwepo wake siku zote. Kambuka hata YESU alifunga siku 40. Tazama pia waninawi ambao walijivika magunia na kufunga ambapo mpaka mifugo haikutoka zizini mpaka pale waliposamehewa

3. KWA KULIA- Juta kwa kile ulichokifanya mpaka kikakutoa mbele ya uso wake ili ukatubu maana hauwezi kutubu kama hujui kosa. BWANA anasema “kumbuka ni wapi ulikoanguka; ukatubu, ukayafanye matendo ya kwanza. Lakini, usipofanya hivyo, naja kwako, nami nitakiondoa kinara chako katika mahali pake, usipotubu. (ufunuo.2:5)
pili unashauriwa kwenda kicho mbele za BWANA au kwa maana nyingine kwa kujinyenyekeza jiweke mbele yake kwa mda mrefu huku ukiiombolezea nafsi yako kwa kosa ililotenda na MUNGU atakusamehe baada ya kujuta kwa nafsi yako.
ndipo tukutane katika somo jingine la jinsi kudumu katika uwepo wa BWANA maisha yako yote na BWANA akubariki kwa kusoma hiki kipande.
Mwandishi; Michael Basanorare (0765 279 698)

Hakuna maoni

Inaendeshwa na Blogger.