Header Ads

NDANI YA DINI YANGU----5


MATENDO YAKE HUMTANGAZA KRISTO{kusoma utangulizi bofya hapa}

"Usiangalie matendo yangu bali sikia nasema nini kwako au fuata ninachosema" moja ya hoja maarufu sana kwa wakristo wengi wasiojua kwanini wanamfuata KRISTO. Ni kweli Mungu huichunguza mioyo kama biblia inavyosema kwenye mstari wa 1 Samuel 16:7…Bwana haangalii kama binadamu aangaliavyo; maana wanadamu huitazama sura ya nje, bali Bwana huutazama moyo. Subiri nikuambie kitu kimoja ambacho unatakiwa ukielewe kutoka kwangu na si kwamwingine biblia ni kitabu kitakatifu huwa kinachanganya kama usipoweza kufunuliwa kwa Roho mtakatifu. Kuna wachungaji kwa kutojua maana halisi ya neno au msitari huitafasiri vibaya na huenda nawewe ulichukua kwake. 
             Wengine huitafasiri kwaajili ya kuficha udhaifu wao na hao ndio laana imekaa kwao na ndio waalim wa uongo walionenwa ujihadhari nao mapema nakuonya pia. Kuna siku nilikuwa nafundisha nakumbuka nikataka kutoa mfano nikaonya mapema natumia tafsiri isiyo takiwa kuitumia kwenye kila mazingira bali ni kwa mazingira ya mfano huu tu. Sasa kama nisingetoa hiyo kuna watu wangechukua kama ni tafsiri ya kijumla na kuna mazingira ingepingana na wao wenyewe kutumika. Swali la msingi JE NI KWELI MUNGU HUANGALIA MOYO TU? KAMA NDIO KWANINI NIANDIKE MATENDO? KAMA HAPANA JE HUO MSITARI NI WAUONGO?. Nikutoe hofu kwanza kama umeshaanza kuwaza nitajibuje kwenye hayo maswali mawili hapo juu. Kwa msitari huo hauna tatizo kabisaa kama ukiutumia kumuonya mtu ambaye kwa nje ni msafi au unasisitiza usafi ndipo unasema Bwana haangalii nje bali huangalia mioyo na kuvichunguza viuno yeremia 17:10{Mimi, Bwana, nauchunguza moyo, navijaribu viuno, hata kumpa kila mtu kiasi cha njia zake, kiasi cha matunda ya matendo yake}.
         Je unakumbuka kuwa dhambi huanzia ndani ya mtu na siyo nje kama wengi wanavyodhani soma tena mwanzo 4:7{Usipotenda vyema dhambi iko, inakuotea mlangoni, nayo inakutamani wewe, walakini yapasa uishinde.}jiulize sasa hapo mlango ni upi?. Soma tena ayubu{Job 38:17 Je! Umefunuliwa malango ya mauti, Au umeyaona malango ya kuzimu?}. Uone kitu kingine kipya kabisaa ndipo ujue kuwa biblia haishii hapo wewe unapoona kwa upeo wako wala kwa maandiko ya BASA tu. Pia maandiko siyo ulokole na wala siyo UKRISTO kwamaana UKRISTO ni kuwa ndani ya KRISTO na ULOKOLE ni kumiminwa ndani ya ROHO MTAKATIFU. Ukitaka kuwa MKRISTO kweli jifunze msalabani sana na ukubali na kutii kila andiko kama lilivyo bila kusema mtumishi fulani alisema hivi au vile. Kuna mtu mmoja alifundishwa na watu wawili tofauti mtu wa kwanza alifundisha kutopenda kumpa mkono kila mtu na hakuelezea kwanini na kwa mazingira gani?. Mtu wa pili akafundisha kuwapenda wale wa nje na kuwasalimia kwa kupeana mikono na kama ni jinsia moja unaweza kuwakumbatia kabisaa. Swali likaja kwangu sasa je amfuate nani kwamaana wote ni wachungaji na anawaamini sana na hahisi kama kuna mmoja kasema uongo. Mimi nikacheka kisha nikamfundisha chimbuko la mafundisho yote mawili na kwanini yapo hivyo na kwenye ulimwengu wa roho yanachukuliwaje kisha na yeye afuate lipi?. Lakini nilichogundua kwa huyu mtu hajazama ndani ya Roho mtakatifu vizuri ndio maana hakuelewa ashike lipi sasa?. 
       Ndio maana nasema kwamba matendo yako yote yanatakiwa yamhubiri KRISTO, watu waduniani wanaangalia porn na wewe mkristo unaangalia halafu unataka uione mbingu sahau tu. Mungu siyo wa mzaha kiasi hicho aisee tena pole sana. Watu wanajitesa kwa kufunga na kuomba na kukesha wewe unakula siku 365 kwa mwaka na kulala masaa yote. Kuomba dakika tano nyingi halafu unataka eti ufunuliwe kwenye ulimwengu wa roho sahau tu. Mtu unatembea uchi halafu unataka Yesu aonekane kwako au ajidhihirushe labda utumie pepo aisee. Hakika Mtu ambaye roho yake inamwabudu Mungu kweli au moyo wake unakicho cha Bwana halafu kwa nje anachotoa ni uongo, uasherati, wizi, uuaji, chuki, uchonganishi, ufiraji, kuchora tattoo, huombi, husomi neno, disko umo, sehem za laana hukosi. Wasioamini wanassema kabisaa kama nawewe ukiingia mbinguni basi mimi nitakuwa malaika {mathayo 5:20}halafu unajibu utaona Mungu anaangalia moyo wa mtu haangalii matendo pumbavu kabisaa mwana wa laana wewe. 
       Wewe ndio unafanya injili inakuwa ngumu kwa watu kuipokea na kuitii kwamaana haoni tofauti yako wewe ambaye ni mfuasi wa KRISTO na yeye ambaye bado anaabudu miungu mingine. Basi tuangalie matendo yako kama Mungu anayatazama kama moyo au vyote viwili. Tito 1:16 Wanakiri ya kwamba wanamjua Mungu, bali kwa matendo yao wanamkana; ni wenye machukizo, waasi, wala kwa kila tendo jema hawafai. Huyo siyo mimi bali ni walaka kwa tito ambao mwandishi anaonesha kitu kidogo kwamba kuna matendo ambayo ukiyafanya unakuwa unamkataa Mungu kabisaa. Mkirsto mwenzangu hujui kwamba mdomo wako unaweza kuwa unamkubali Mungu kweli lakini mwili wako unafanya ibada za miungu kila siku. Badilika wewe mkristo mwenzangu hakikisha matendo yako yanatoa kile kilichoko ndani ya moyo wako ambacho Yesu mwenyewe alifundisha. Hatuna kipimo kingine cha utakatifu isipokuwa matunda ya ROHO MTAKATIFU.

Mwandishi: MICHAEL BASA 0765279698/+255789799199

Hakuna maoni

Inaendeshwa na Blogger.