Header Ads

MTAZAMO WANGU

Usimkosee Mungu kwa vitu vitatu naam kwa vitu vinne hautakiwi kuikosa mbingu
  1. TUMBO
  2. MAVAZI
  3. UPAKO
  4. NDOA

1.    Hakuna kitu kizuri kama kula na kunywa mbele za Bwana maana nayo ni karama aisee {mhubiri 3:13 Tena ni karama ya Mungu kila mtu apate kula na kunywa, na kujiburudisha kwa mema katika kazi yake yote.} hata mimi napenda kula na kunywa sana na kufurahia kila chakula na kinywaji changu. Lakini kuna kitu cha kuchunga kila karama ina mipaka yake hata karama ya kulihudumia tumbo inamipaka yake tena mikubwa. Mwanzo 2:16-17{Bwana Mungu akamwagiza huyo mtu, akisema, Matunda ya kila mti wa bustani waweza kula,walakini matunda ya mti wa ujuzi wa mema na mabaya usile, kwa maana siku utakapokula matunda ya mti huo utakufa hakika}. Umepewa kula na kunywa na kufurahi lakini yakumbuke masharti ya kula na kunywa n siyo kujiendea kama usiye na akili. Huo mwili unaohitaji chakula inatakiwa upate nguvu na afya siyo kufa ndio maana adam akaewa angalizo mappema kabisaa. Naamini katika biblia sheria ya kwanza ilihusu chakula kwa mwanadam na ndio agizo la kwanza kabisaa. Kuna watu wanahisi kila kitu ni chakula na kunywa tu huku afya zao au uzima ndani yao unatetereka kila siku na magonjwa ya ajabu ajabu yanaongezeka. Wataalam wa afya wanadai kuwa ulaji mbaya umefanya magonjwa yasoyoambukiza kuongezeka. 
                   Kwenye angalizo la kwanza lilikuwa ni kula chakula ulichoewa mwenyewe na ambacho unauwezo wa kuamua ule nini na nini usile?. Basi tumbo hutamani kila kitu kwa mda wote bali roho hutafuta ibada kwa kila jambo hapa nasemea mtu aliyempokea KRISTO nasivinginevyo. Kuna watu siyo Amani ya KRISTO ndani yao bali ni mazoea yao ndio huamua ndani yao. Ni kweli andiko lasema wazi kuleni vyote kwaajili ya dhamiri lakini kumbuka siyo kila chakula chafaa kuliwa na mwandam na si kila kinywaji cha chafaa kwa afya yako anza sasa kula na kunywa kwaajili ya roho yako mwenyewe na kwaajili ya uzima wako ndani ya KRISTO. Kula kwaajili ya kufurahia hii karama lakini uwe na KIASI katika kula kwako na kunywa kwako. Kuna watu wamejaa ubatili kwaajili ua kula tu na kunywa. Nawaonya mapema isafisheni mikono yenu na muzitakase nia zenu ili roho zimrudie YEYE aliye juu na yote na juu ya vyote ni Bwana wa vyote pia na ndie aliye mmiliki wa vyote Mungu wa enzi na miliki zote. Kwamaana wokovu wafaa sana kwake yeye aliye nao na Roho wa ahadi afaa kwa vyote na yote pia. Kuna watu walimfuta Yesu kwasababu tu walikula mikate waksahau kuwa hawajanywa maji ya uzima, je wewe tumbo lako limeokoka na vyakula vya laana na makao ya kuzimu yako nje ya viuongo vyako. Mkate usikutoe kwa Yesu kwamaana 1wakolintho 6:13 Vyakula ni kwa tumbo, na tumbo ni kwa vyakula; lakini Mungu atavitowesha vyote viwili, tumbo na vyakula. Lakini mwili si kwa zinaa, bali ni kwa Bwana, naye Bwana ni kwa mwili. 
       Utapata hasara kama uliwekeza kwa tumbo kwamaana hakuna kitakachobaki kwako siku ya hukumu lakini wewe basi jifariji kwa hii yohana 6:51 Mimi ndimi chakula chenye uzima kilichoshuka kutoka mbinguni; mtu akila chakula hiki, ataishi milele. Na chakula nitakachotoa mimi ni mwili wangu, kwa ajili ya uzima wa ulimwengu. Hakikisha tumbo lako limejaa hiki chakula kila siku za Maisha yako 
           Mandishi MICHAEL BASA 0765279698

Hakuna maoni

Inaendeshwa na Blogger.