Header Ads

MUDA GANI MUNGU ANAFUNDISHA???

kujibu hili swali ni bora kwanza tukawa na uhakika kuwa MUNGU wetu anasema na watu wake aliowaumba kwa mfano wake. Tazama huu msitari .......Akiwapo nabii kati yenu,Mimi, Bwana, nitajifunua kwake katika maono,Nitasema naye katika ndoto {hesabu 12:6 }. Hapa kuna kitu cha kujua kuwa BWANA husema kwa njia anayoichagua mwenyewe kwa maana kwa mananbii wa jamii hiyo kachagua njia ya ndoto. Kwa kuwa Mungu hunena mara moja, Naam, hata mara ya pili, ajapokuwa mtu hajali{ayubu 33:14}. 
     
 Basi kupitia maandiko hayo tunaamini kwamba MUNGU hunena na watu wake kama yeye vile apendavyo. Naam sasa ni bora tuangalie njia ambazo BWANA anaweza tumia kunena na mtu mmoja mmoja au na kanisa kwa ujumla.anbazo ni:- 
  1. Wazo jipya
  2. Kutumia watu wa kawaida
  3. Kusema naww moja kwa moja
  4. Mafunuo
  5. Ndoto
  6. Manabii
 Hizo ndizo njia ambazo MUNGU amezitumia kwenye biblia kunena na watu wake sana.
     Manabii wametumika kipindi kikubwa cha agano jipya na pia mpaka leo bado wanatumika kwa kutoa mwongozo na wakati mwingine maonyo kwa kanisa na pia kutoa majibu ya maombi yao.  

    Ukisoma ayubu 33:14--16 utajua ni kwanini kwawewe ni lazima uwe unaota ndoto na pia ni lazima uzikumbuke ndoto unazoota na uzijue ndoto zinazojirudia. Maana ndoto ikijirudia inamaana kwamba MUNGU mwenyewe amelidhibitisha kwako neno lake mwanzo 41:32. 

     Pia wazo jipya linaweza kukujia tu kichwani hiyo ppia ni njia ambayo Bwana huitumia kujifunua na kutoa majibu juu ya maombi. 
         Moja ya tatizo kubwa ambalo watu wengi tunakutana nalo ni kuchagua watu wa kusema nao na ppengine hata wa kuwasikiliza. Lakini watu hao hao wanaweza kutumiwa na Bwana kama vyombo vya wewe kusema naye na kuisikia sauti yake kwa upana sana kwa hiyo Bwana anaweza kusema nawewe na wala usijali. 
   Watu ambao wako vizuri kiroho au ambao wamepakwa mafuta hawa huweza kumsikia ROHO akinena wazi wazi kwao mfano wake ni MUSA. MUNGU anaamuaa kunena kwa ishara na watu wengine wote bali kwa MUSA anaamua kusema naye uso kwa uso. kwa hiyo mafuta aliyopakwa musa yalikuwa tofauti na aliyopakwa haruni. Pia mafunuo huja kwa mtu ambayo BWANA hutumia kutoa majibu au kusema na watu wake. 
  
by MICHAEL BASA. 

Hakuna maoni

Inaendeshwa na Blogger.