Header Ads

BARAKA ZAKO ZIKUJIAPO

MUNGU ni mfano wa mwanadam uliojificha wenye sifa na maamuzi na hisia kama mwanadam uliozungukwa nautukufu pande zote. Tofauti kubwa kati ya mwanadam na MUNGU ni ibada na dhambi. Mwanadam hutafuta kitu chenye uwezo mkubwa na kukipa sifa ya MUNGU{maana mungu ni cheo tu na siyo jina ni kama kusema raisi hi hutegemea na nchi yako na mtu aliyepo madarakani na siyo mtu fulani} na chenyewe hakiwezi kukipeleka hiyo sifa sehem nyingine. Ndio maana mwanadam humwabudu mungu na wala mungu hamwabudu mwanadam. Ukikuta mungu ana mungu wake kuna sifa ya kiungu hupungua kwake mfano mungumtu. Basi ukikuta mungu wako ana mungu mwingine ujue huyo yupo kwa kazi fulani na kuna anashindwa kutenda mpaka umjue mungu mkuu wake maana yeye ndio anampa mungu wako nguvu za kujibu  maombi yako. Kingine ni dhambi, haya ni matendo au fikra ambazo mungu unayemtumikia anazipinga kwenye ufalme wake au kwenye ibada zake. Mfano wake ni MUNGU-YESU kutamani uasherati na mfanya uasherati wote ni wamefanya zinaa katika ullimwengu wake. Basi tujikite kwa MUNGU muumba mbingu na nchi na aliyeandikwa kwenye biblia tu maana sitajikita kwa miungu wengine waliobaki nje ya huyo.
        Baraka ni mafuta au nguvu anayopokea mtu kwaajili ya kumiliki kitu vitu au eneo pamoja na vilivyomo ndani yake. Basi MUNGU akikubariki kwenye kazi fulani amekupa kila kitu kinachohusiana na hiyo kazi kinachobaki ni wewe tu kujua nguvu ipi itumike wakati gani?. Mfano mzuri maarifa yapi yatumike wapi na kwa wakati gani?, busara itumike kwa mtu gani na kwanini??, watu wa jinsi fulani uwamiliki vp?, pia nguvu ya maono ya kazi unayofanya utaweza kujua kipi ni muhimu kwa majira  na nyakati zake. Lakini ili MUNGU akubariki inakubidi ujitahidi kugusa moyo wake maana bila hivyo huwezi kufanikiwa katika baraka atakayoiachia kwako. Ukisoma torati 28 utakuta baraka nyingi sana ameahidi MUNGU kukupa lakini baraka zote hizo zimegeuka laana kwa maana msitari wa kwanza wa torati 28 unasema kwamba ''Itakuwa utakaposikia sauti ya Bwana, Mungu wako, kwa bidii, kutunza kuyafanya maagizo yake yote nikuagizayo leo, ndipo Bwana, Mungu wako, atakapokutukuza juu ya mataifa yote ya duniani;''. Baraka zote ulizoahidiwa zinaweza kukupata kama nguvu ya yakufanikiwa au nguvu yakukurudisha nyuma{laana} kwasababu ya sautu ya MUNGU. Kuna vitu vitatu katika msitari huu ambavyo ni muhimu sana navyo ni:-
  1. Itakuwa utakaposikia sauti ya Bwana, Mungu wako,
  2. kwa bidii,
  3. kutunza
  4. kuyafanya maagizo yake yote nikuagizayo leo,

        Kuna kitu muhim cha kuelewa hapo nacho ni kusikia ssauti ya MUNGU. Hii inaonesha MUNGU anasema nawewe baada na kabla ya kukupa hiyo nguvu. Pili usisikie tu kwa jinsi ya kawaida lakini uwe mtu wakujitaabisha kwaajili ya kusema na MUNGU wako ndio maana kuna neno  bidii hapo. Tatu baada ya kuisikia ni lazima kutunza kwa maana nyingine ROHO ananiambia hapa ni kuchambua ili kuvijua {mtumie ROHO tu hapa ili uwe vizuri zaidi katika kipande hiki}. Baada ya kuvichambua na kuvijua vyote chukua ambayo ni maagizo ndiyo ukayafanye kwama alivyoagiza MUNGU mwenyewe katika kusema kwake. Usitende kwa jinsi ya kibinadam maana itahesabika kama uasi mbele za MUNGU. 
         imeandikwa na MICHAEL BASA 

Hakuna maoni

Inaendeshwa na Blogger.