Header Ads

NEEMA ILIYOZIDI SHARIA

 


   Neema {grace the free and unearned favour of God, a divinely given talent or blessing} ni hali ya kupata kitu ambacho hukustahili kupata kwa matendo,elimu,uwezo au muonekano wako. Kwa mkristo ni neema imeelezwa ni haki kuupata wana wa Mungu. Kwamaana baada ya Yesu kufa msalabani kwaajili ya dhambi za watu wengine kwahiyo yeye{YESU} anateswa hali mwenyewe hajafanya tendo lolote lipasalo kufa. Maana yake ni hii mtu atendaye dhambi asitahili kifo tena cha aibu kilichojaa mateso. Mwanadam alikuwa na dhambi na alihesabiwa kifo waefeso 2:1 Nanyi mlikuwa wafu kwa sababu ya makosa na dhambi zenu; Yesu mwenyewe akajitoa kufa kwaajili ya kuichukua hiyo hatia na huyu mwanadam ambaye hakustahili mwanzo apate kibali cha kuwa mwana na kupaingia patakatifu pa Mungu.

 

Sharia ni taratibu ambazo huwekwa kwa ajili ya kuongoza,kulinda au kuweka usawa kwenye kundi husika. Hizi huwekwa kwa makusudi ya kumtia mtu hatia na siyo kumwokoa. Kabla ya Kristo kuja sharia zilikuja kwa mkono wa musa. Ziliwekwa ili watu wajue kuna Mungu wa baba yao Ibrahim, Isaka na Yakobo ambaye anapaswa kuabudiwa ndio maana ukisoma torati ya Musa utakuja kuona ni kiasi tendo la dhambi lilihukumiwa kwa kifo mda wote ndani ya kundi.

 

    Yesu alikuja na second chance ya dhambi badala ya kifo ndio maana ukisoma (marko 8:1-11). Sharia ipo kwaajili ya kuonesha makosa na siyo kusahihisha na pia haina nguvu ya kusaidia mtu asitende kosa husika. Bali husimamia hukumu juu ya mwanadamu. Napenda msomaji unielewe hivi kwasababu ya sharia ya dhambi, mauti(kifo) ilipata nguvu na kwasababu ya neema uzima unapata nguvu ya kuishinda dhambi.

   Basi neema ilikuja ulimwenguni na kuifanya sharia kuwa kivuli cha mambo yanayotakiwa kutendwa. Yaani namaanisha kule kusema usile wala kunywa ni kwa sharia. Bali kwa neema kula vyote na kunywa vyote katika Bwana. Kwamaana bwana mwenyewe ataandika njia zake katika mioyo yetu kama ilivyo ahadi(Ezekiel 36:26-27). Ndiyo iliyokuja kutimizwa kwenye efeso 8:9&10.

          Tamaa yangu ni wote tujue hili neno katika Roho 1timotheo 1:8-10 Lakini twajua ya kuwa sheria ni njema, kama mtu akiitumia kwa njia iliyo halali; akilifahamu neno hili, ya kuwa sheria haimhusu mtu wa haki, bali waasi, na wasio wataratibu, na makafiri, na wenye dhambi, na wanajisi, na wasiomcha Mungu, na wapigao baba zao, na wapigao mama zao, na wauaji,na wazinifu, na wafiraji, na waibao watu, na waongo, nao waapao kwa uongo; na likiwapo neno lo lote linginelo lisilopatana na mafundisho yenye uzima;.

Basi neema ni Zaidi ya sharia kwamaana huwaelekeza na kuwakalisha watu katika uzima na uchaji Mungu. Ile neema ya kuweka{kuandika} sharia za Mungu katika mioyo ya watu wote wanaolikili neno la neema ya kuwa Yesu ni Mwana wake kamili. Hakika na wote walioijiliwa na neno la mwana wake walifanyika kuwa wana wa Mungu. Tena ikaandikwa mimi leo nimekuzaa. Neno hilo halikuwa kwaajili ya malaika wa mbinguni bali ni wale kwa uchaji wao hufanyika miungu. Basi naijulikane hivi Maana neema ya Mungu iwaokoayo wanadamu wote imefunuliwa [tito 2:11]. Tena neema hii huokoa watu wote na haiwaweki chini ya kongwa la utumwa bali huwaweka huru. Kule kusema wote ni nini basi? Kwamaana kwa neema wote waliokili na kubatizwa hakika hao ndio walio katika neema hii. Tena wakaandikiwa wote kwa njia ya wokovu kama ilivyoandikwa kwenye mariko 16:16, rumi 10:12-17.

Prop,Mwal: Michael Basanorare 0765 279 698, +255 737 919 561

 

 

JINA LA BWANA LIBARIKIWE

Hakuna maoni

Inaendeshwa na Blogger.