Jumapili, 2 Oktoba 2016

SOMO: HATUA ZA KUINGIA KWENYE MAOMBI----1

kuomba ni moja ya nguzo muhimu sana katika kuuendea ufalme wa mbinguni. Bali watu wengi tumekuwa tunaona maombi ni sehem ya kutimiza wajibu bali kiukweli ni sehem ya kuongea na BABA yetu ambaye kwa imani katuzaa kupitia kifo cha mwanaye YESU KRISTO. Ili maombi yako yawe ni manufaa kwako unaweza pitia kwanza somo la NGUVU ILIYOMO KWENYE MAOMBI ndani ya BASA MINISTRY. Ndio uje kwenye hiki kipande cha hatua za kuingia kwenye maombi ambazo ni:
1}KUSUDI LA MAOMBI YAKO
Watu wengi tunaamini kuomba kwa masaa mengi ndio kipimo cha maombi au maneno kuwa mengi ndio MUNGU atusikia na kutenda unaweza kuta kuwa maombi ya dakika kumi za mwanzo yamejibiwa na yale ya masaa mawili yote hayajajibiwa hata moja. Ukisoma mathayo 6:7&8 YESU alielezea vizuri sana hili jambo ingawa watu wengi hatuelewi alimaanisha nini? Bali ukweli wake siyo kwamba kutoomba kwa sauti wala kurudia jambo wakati wakati wa maombi (mathayo 26:39-44). Bali kuomba kwa mpangilio ulio mzuri na yawe na mtiririko mzuri hata mtu mwingine akisikiliza unaomba ajue unaombea nini kwa mda na umeombea vitu gani. kwahiyo kusudi la kwenda kufanya hayo maombi ni muhimu pia unaweza liandika kwenye karatasi na kuliainisha kwa vipengele kwamba nitaanza na hiki na nitaishia na hiki kipengele.
2}MAHALI 
mazingira yakufanyia maombi yako ni muhimu sana kuliko unavyoweza kuwaza au kulichukulia. Ukisoma mark 6:46 unaona YESU anajitenga na wanafunzi wake ili akaombe lakini anaenda sehemu ambayo hata makutano hawawezi kumuona kwa mda huo ili akaombe tu. Pia ukisoma mark 1:35 unaweza ona YESU KRISTO anaenda sehemu isiyokuwa na watu akaombe tena alfajiri na mapema. Kwahiyo unapochagua sehem ya kufanyia maombi yako chagua iwe ni sehem ambayo hakutakuwa na ususmbufu wowote. Usumbufu ambao utakutoa kuzama kwenye maombi yako kwa mda huo.
3} MUDA WA KUOMBA
Hii imegawanyika mara mbili
  1.              KUNA MDA WA KUKAA KWENYE MAOMBI hapa ninachoongelea ni kwa mda gani utakaa kwenye maombi yako. Ukisoma mathayo 26:39-44 kwenye msitari wa 40 utaona YESU anauliza Je! Hamkuweza kukesha pamoja nami hata saa moja?. Kwamaana nyingine mda ambao YESU aliuona unawafaa hawa watu kukaa kwenye maombi kwa uchache ni saa moja. Je wewe kwenye maombi yako unakaa kwa mda gani rafiki na ndugu yangu katika IMANI?. Mimi nakushauri fanya mda kidogo zaidi ya wewe kukaa kwenye maombi uwe ni dakika 30 lakini usikae hapo ukalizika nenda mpaka ufikie angalau masaa mawili kwenye maombi yako.
  2.           MDA WA KUINGIA KWENYE MAOMBI YAKO. Muda wa kuingia kwenye maombi hakikisha ni muda ambao wewe umemaliza kazi zako au uko huru inamaana hakuna wazo lakuingilia maombi yako akili yako yote iwe kwenye hayo maombi na siyo uwe na nia mbili [double minded]. Kuna mda ambao kibiblia unasiri kubwa ukiufuata nao ni

  •        ALFAJIRI=mda huu unasiri ya jinsi ya kipekee sana kwasababu ni muda pekee ambao daudi aliamsha utukufu wa BWANA juu yake zaburi 57:7—9. Pia Ayubu alikuwa anawatakasa wanaye asubuhi na mapema ayubu 1:5. Natamani nawewe uanze kuutumia huu mda kwaajili ya kuumba siku yako unayoiendea kwako na kwa familia yako yote.
  •            Saa tatu
  •             Saa sita
  •           Saa tisa
  •            JIONI AU MDA WA KUPUNGA JUA= huu ni mda wa ibaada ya shukrani kwa mda wa siku nzima ambao BWANA amekufanikisha. Pia ni mda wako mzuri wa kutafakari mambo yote aliyokutendea BWANA pia ni mda wa wewe kujitafakari umefanya nini kuhusu BWANA?. Kujitafakari ni njia nzuri zaidi ya kujipanga kwaajili ya BWANA juu ya siku ijayo ppia kuungama kwaajili ya makosa ambayo hukuyatambua mda wote wa mchana.


Lakini kumbuka unapochagua mda wa kuingia na kukaa kukaa kwenye maombi hakikisha kuwa ni mda ambao unakuweka katika hali ya msawazo[relaxation]  wa kiakili na mwili ili uweze kujitoa katika Roho na kuzama kwa kumwita BWANA kwenye roho yako


Mtum: Prop: Mwalim: MICHAEL BASA

Jumapili, 4 Septemba 2016

UBATIZO WA WATOTO WADOGO

KUTOKEA KWENYE SOMO LETU LA UBATIZO{kulisoma bofya hapa} Taratibu za kubatiza watoto kwa kunyunyizia maji zilianza mwishoni mwa karne ya 2 B.K, lakini hazikupata ukubali wa wengi mpaka miaka ya 354-430 B.K. Hapo ndipo watu walioasi walipoanza kufundisha kuwa watoto wanarithi dhambi za Adam na Hawa na kwa hivyo wanazaliwa wakiwa na dhambi ya asili na hivyo wanapaswa kubatizwa baada ya kuzaliwa.

Hayo Yalikuwa Ni Mawazo Yao Waliyotunga Na Siyo Fundisho La Biblia.

BIBLIA iNASEMA WATOTO WANAPASWA KUBARIKIWA NA SIYO KUBATIZWA, BIBLIA INASEMA.
"Basi wakamletea watoto wadogo ili awaguse; wanafunzi wake wakawakemea. Ila Yesu alipoona alichukizwa sana, akawaambia, Waacheni watoto wadogo waje kwangu, msiwazuie; kwa maana watoto kama hawa ufalme wa Mungu ni wao.Amin, nawaambieni, Ye yote asiyeukubali ufalme wa Mungu kama mtoto mdogo hatauingia kabisa.Akawakumbatia, akaweka mikono yake juu yao, akawabarikia."(Marko 10:13-16).

KUNA HATUA AMBAZO INABIDI MTU AZIPITIE KABLA YA KUBATIZWA..

HATUA YA KWANZA.
Kabla ya kubatizwa lazima mtu mwenyewe bila kulazimishwa Aamini. Biblia Inasema. "Wakawa wakiendelea njiani, wakafika mahali penye maji; yule towashi akasema, Tazama, maji haya; ni nini kinachonizuia nisibatizwe? [Filipo akasema, Ukiamini kwa moyo wako wote, inawezekana. Akajibu, akanena, Naamini ya kwamba Yesu Kristo ndiye Mwana wa Mungu.]
Akaamuru lile gari lisimame; wakatelemka wote wawili majini, Filipo na yule towashi; naye akambatiza." (Matendo 8:36-38). Tena hapa anayebatizwa aliamini mwenyewe, Tena hakuna aliyesema kwa niaba yake.

HATUA YA PILI.
Mtu mwenyewe anatakiwa atubu dhambi zake, Tena kutubu dhambi, sharti kuwepo kujutia dhambi yako. Biblia Inasema. "Walipoyasikia haya wakachomwa mioyo yao, wakamwambia Petro na mitume wengine, Tutendeje, ndugu zetu? Petro akawaambia, Tubuni mkabatizwe kila mmoja kwa jina lake Yesu Kristo, mpate ondoleo la dhambi zenu, nanyi mtapokea kipawa cha Roho Mtakatifu." (Matendo 2:37-38).

SASA TUMEONA KUWA KABLA MTOTO HAJABATIZWA SHARTI AAMINI KWA MOYO WAKE WOTE.Maswali ya Kujiuliza:-
      1.  watoto wanaamini wenyewe Tena Moyo wote ? Au wanaaminishwa?
      2. Je kitoto kichanga ambacho hakiongei kinaweza kuamini?
      3. Lakini hatua ya pili Sharti mtoto atubu. Swali Je mtoto mdogo, kichanga kinaweza kutubu?
      4. Mtoto mdogo anaweza kujutia dhambi yake?

Yawezekana unapanga kumbatiza mtoto wako ubatizo wa kunyunyizia, Yawezekana ulibatizwa ubatizo wa kunyunyizia Tena ukiwa mtoto bila hiari yako, Tena Yawezekana umekuta una cheti cha ubatizo Lakini ulipobatizwa haukumbuki. Rafiki yangu nataka nikuambie kuwa huo ni uongo wa Shetani, ulio kinyume na Maandiko, maana kazi ya Ibilisi ni kuudanganya ulimwenguni. Biblia Inasema "Yule joka akatupwa, yule mkubwa, nyoka wa zamani, aitwaye Ibilisi na Shetani, audanganyaye ulimwengu wote." (Ufunuo 12:9).
Mpokee Yesu na Kubatizwa ubatizo sahihi wa biblia Tena wa KUZAMISHWA NDANI YA MAJI MENGI , Tena iwe ni baada ya kuamini Bila kuaminishwa.

Jumatano, 31 Agosti 2016

UBATIZO

Kwanini nibatizwe? Ubatizo upi ni sahihi kibilia?. Ni wakati upi na nani anatakiwa kubatizwa? Je, ni kabla ya kupokea wokovu au baada? Faida zake ni zipi? .

Kwanza kabisa; kuna batizo zitokazo kwa wanadamu na pia upo ubatizo unaotoka kwa Mungu. Tunajua hili kutokana na Yesu alipowauliza makuhani na wazee wa Israel kwa Kusema “Nitawauliza neno moja, nanyi mnijibu, kisha nitawaambia ni kwa mamlaka gani nayatenda haya. Ubatizo wa Yohana ulitoka mbinguni, au kwa wanadamu? Nijibuni” (Mk.11:30-32).

Kutoka hapo tunajuwa kumbe ubatizo ule wa Yohana ulitoka Mbinguni. Pia kabla ya Yohana Mbatizaji, kulikuwa na aina mbalimbali za batizo ambazo hazikuwa kama ubatizo wa yohana. Hii ni kutokana na swali ambalo watu kadhaa waliulizwa na mtume Paulo kwa kusema “Basi mlibatizwa kwa ubatizo gani? Wakasema, Kwa ubatizo wa Yohana” (matendo,19:3). Hivyo kutoka hapo pia tunajua kumbe hata wakati wa mitume kulikuwa na batizo aina mbalimbali zilizoletwa na wanadamu
Kabla Yesu hajaondoka duniani, naye alikuwa anabatiza watu kupitia wanafunzi wake. Na aina ya Ubatizo aliokuwa anautumia ulikuwa ni ule uliotoka Mbinguni ulioletwa kwa mkono wa Yohana. Kama ilivyoandikwa “Baada ya hayo Yesu na wanafunzi wake walikwenda mpaka nchi ya Uyahudi; akashinda huko pamoja nao, akabatiza” (yoh.3:22,10:40). Na huu ndiyo ubatizo sahihi kibibilia ambao Yesu aliowaachia wanafunzi wake mpaka leo.

Sasa Ubatizo wa Maji Mengi huu wa Yohana Mbatizaji Mungu ameuweka ili kwa Njia hiyo nawewe ushiriki kifo cha Yesu kwa kufa pamoja naye na kufufuka pamoja naye kwa njia ya kuzamishwa na kuinuliwa katika maji. Kama ilivyoandikwa “sisi sote tuliobatizwa katika Kristo Yesu tulibatizwa katika mauti yake” na tena “tulizikwa pamoja naye kwa njia ya ubatizo katika mauti yake, kusudi kama Kristo alivyofufuka katika wafu kwa njia ya utukufu wa Baba, vivyo hivyo na sisi tuenende katika upya wa uzima”. na tena “Mkazikwa pamoja naye katika ubatizo; na katika huo mkafufuliwa pamoja naye” (Rum.6:3-6, Col.2:12). Hivyo tunaona kumbe unapobatizwa, mambo halisi hufanyika wala sio ishara tu.

Siku unayo-batizwa kwa maji mengi ndiyo siku ambayo 1) unakufa pamoja na Kristo msalabani. 2) unafufuka pamoja na Yesu mautini. 3). Unapokea Uwezo wa kuenenda katika hali ya “upya wa uzima” alionao Yesu sasa. 4) unakuwa umetimiza haki yote. Maana imeandikwa “mshahara wa dhambi ni mauti”. Na kwasabu wewe hapo mwanzo ulikuwa mdhambi… Unahukumiwa mauti pamoja na Yesu kwa njia ya msalaba na mauti yake. Hivyo hutahukumiwa mauti ile siku ya kuuhukumu ulimwengu wote (yohana.5:24)

Tunajuwa kuwa Yesu aliposulubiwa msalabani hakufa muda uleule; bali alisulubiwa saa tatu lakini akafa saa tisa (Mk. 15:24,34). Vivyohivyo Kuokoka maana Yake ni kuzaliwa mala ya pili kunako ambatana na kupokea utakaso wa dhambi zote na kunyweshwa ua kumpokea Roho Mtakatifu ndani yako aishi nawe milele. Na kwasababu hiyo wewe unakuwa kiumbe Kipya uliye Mwana wa Mungu, uliye mtakatifu na uzima wa Milele unakuwa ndani yako. Kama ilivyoandikwa “alituokoa;…, kwa kuoshwa kwa kuzaliwa kwa mara ya pili na kufanywa upya na Roho Mtakatifu”, na tena “Yeye aliye naye Mwana, anao huo uzima; asiye naye Mwana wa Mungu hana huo uzima “(tito.3:4-7, 1yoh.5:12).

Kwahiyo mtu huyu alie-okoka anakuwa amezaliwa mara ya pili na amesulubiwa msalabani pasipo kuzikwa utu wake wa kale na kufufuka pamoja na Yesu. Kama ilivyoandikwa “hao walio wa Kristo Yesu wameusulibisha mwili pamoja na mawazo yake mabaya na tamaa zake” (gal.5:24). Hivyo utu wake wa kale unakuwa bado haujazikwa, kwasababu utu wa kale huzikwa katika ubatizo wa maji mengi.Kwahiyo kama hujabatizwa atakuwa kwenye vita kali daima kati ya roho yako na mwili wako mpaka pale atakapouzika huo utu wako katika ubatizo.

Hivyo haijalishi wewe umeokoka miaka mingi kiasi gani. Lakini pasipo ubatizo wa maji Mengi bado haujakamilika. Hauja-itimiza haki yote. Kwani kumbukumbu za wewe kufa na kufufuka pamoja na Kristo hazipo mbele za Mungu mpaka utakapo kubali kubatizwa kwa ubatizo wa Maji mengi. Usitegemee ubatizo wa kunyunyizia kichwani kwani kwa huo haiwezekani kushiriki mauti na ufufuo wa Yesu Kristo. Kama inavyosema “Mkazikwa pamoja naye katika ubatizo; na katika huo mkafufuliwa pamoja naye”.

Siku unayobatizwa ndiyo siku unayozika utu wako wa kale na kuhukumiwa mauti pamoja na Yesu msalabani ili siku ile ya hukumu usije ukahukumiwa mauti kama wengine ambao wao watahukumiwa mauti. Maana imeandikwa “tumehukumu hivi, ya kwamba mmoja alikufa kwa ajili ya wote, basi walikufa wote” (2Kor.5:14). Kwahiyo huo ubatizo wa Kuzamishwa kwenye maji ni ili uunganishwe na Yesu katika mauti na uzima wake. Ukibatizwa unafanya “final separation from the world”.
Mtu anatakiwa kubatizwa baada ya kupokea wokovu kwanza na sio kabla ya kuamini (Mk.16:16). Maana sababu nyingine ya kubatizwa ni matokeo ya utii yathibitishayo kuwa dhamiri zako zimefanywa upya. Kama ilivyoandikwa “ubatizo, unaowaokoa ninyi pia siku hizi; .., jibu la dhamiri safi mbele za Mungu, kwa kufufuka kwake Yesu Kristo” (1pet.3:21). Sasa jibu la dhamiri haliwezi kuwepo kwa mtoto mchanga kimwili, kwasababu mtu anapo-okoka (born again) ndipo anatakaswa dhamiri zake na kuanza kuzichukia dhambi alizokuwa anazitenda kabla, na roho yake huanza kuumia akiziona dhambi (ebr.9:14, 2pet.2:8)

“utashiriki vipi mauti ya Mwanangu Yesu kwa kunyunyiziwa maji kichwani? Niambie, Je, kwa kunyunyiziwa maji utatimizaje neno langu lisemalo “Mkazikwa pamoja naye katika ubatizo; na katika huo mkafufuliwa pamoja naye”?. “kama vile ambavyo haikuwezekana Mwanangu afe bila kwenda ndani ya nchi chini; vivyohivyo nawewe haiwezekani kushiriki mauti ya Mwanangu pasipo kwenda ndani ya maji”. kwa kubatizwa Yesu ndani ya maji, akatia mhuri na kutangaza mauti na ufufuo wake jinsi utakavyokuwa. Hivyo nawewe imekupasa kuenenda kwa jinsi hiyohiyo.
Laana na magonjwa ya kurithi hukaa na hupata kibali kutokana na wewe kuwa na utu wa kale. Lakini unapobatizwa hayo yote huzikwa na hayawi na mamlaka tena kwani unakuwa “katika upya wa uzima” (rum.6:4). Baada ya kuokoka nilikuwa nabisha sana. Hadi Mungu mwenyewe aliposema na mimi. Na baaada ya kufunuliwa tu bila kuchelewa nilienda nikabatizwa kwa maji mengi. Hivyo hata wewe unaweza ukaenda ukabatizwa bila kuhama hilo dhehebu lako. Nenda Kabatizwe usifungwe na udhehebu ukakosa ufalme.

Sio dhambi, na sio ukosefu wa imani kuamua kubatizwa kwa mala nyingine kama ukigundua ubatizo wa kwanza huakuwa kama neno linavyotaka. Hata mimi nilitumia hoja kama hiyo kukataa kubatizwa kwa maji mengi kwa kusema “nilibatizwa tayari tangu mtoto”. Lakini Bwana akasema “mbona kwenye Matendo 19:2-5 mtume Paulo aliwabatiza mala ya pili watu kadhaa waliokuwa wamebatizwa na yohana mbatizaji?”.

Hautakiwi kubatizwa kama hujapokea wokovu kwanza. Kibiblia mtu haokoki kwa kubatizwa kwa maji. Unapokea wokovu kwanza ndipo unaenda kubatizwa. Mtu asikudanganye kwa kusema siku unayobatizwa ndiyo unayozaliwa mala ya pili- Huo ni uongo. Ukibatizwa kabla ya wokovu ni sawa na mtu anae-oga tu.

Kama kweli wewe ni mteule wa Mungu; Jambo hili la ubatizo hutakuwa na amani nalo mpaka utakapokubali na kutii kwa kwenda kubatizwa. Ndipo moyo wako utakapotulia. Maana Mungu hawezi kumtumia mtu “to the full” kama bado hujabatizwa. Yesu anasema “Amin, amin, nakuambia, Mtu asipozaliwa kwa maji na kwa Roho, hawezi kuuingia ufalme wa Mungu”(Yohana.3:5). AMINA.
Mwandishi: NZUNDA Ibrahim (0754 210 627)

Jumamosi, 27 Agosti 2016

MWONGO NI NANI?

Wengi wanasema; “haijalishi kama wewe ni dini gani, au unafuata njia gani… Mungu ni mmoja… kwahiyo kama unamwabudu Mungu halisi na unatenda mambo mema huko uliko… siku ya mwisho hautahukumiwa”. Je, hii ni kweli au uongo?

Imeandikwa “Je, mwongo ni nani? Mwongo ni mtu yule asemaye kwamba Yesu si Kristo. Mtu wa namna hiyo ndiye MPINGA KRISTO, yaani, yeye humkana Baba na Mwana. Hakuna yeyote amkanaye Mwana aliye na Baba.” (1yohana.2:22-23). Pia Kristo anasema “Mimi ndimi njia na kweli na uzima. Mtu hawezi kuja kwa Baba isipokuwa kwa kupitia Kwangu” (Yohana.14:6). Kwahiyo njia ni moja tu, na imani ni moja tu, yaani Yesu basi. Njia nyingine zote ni za upotevuni (njia pana).

Hii pia ni kwa kila mtu anaetumia majina mengine ili kupata msamaha wa dhambi kutoka kwa Mungu. Yesu anasema “Nanyi mkiomba lo lote kwa Jina Langu, hilo nitalifanya, ili Baba apate kutukuzwa katika Mwana. Kama mkiniomba lo lote kwa Jina Langu nitalifanya” (Yohana.14:13-14, 15:16, 16:23-28) Pia imesisitizwa kuwa; “kama mtu yeyote akitenda dhambi, tunaye Mwombezi kwa Baba, Yesu Kristo Mwenye haki. Yeye ndiye dhabihu ya upatanisho kwa ajili ya dhambi zetu, wala si kwa ajili ya dhambi zetu tu, bali pia kwa ajili ya dhambi za ulimwengu wote” (1yohana.2:1-2).

 Hatuna dhabihu wala mwenye haki zaidi ya Yesu kwahiyo nikisema “Mt. Petro au Maria utuombee sisi wakosefu” badala ya “Yesu utuombee sisi wakosefu”; ninakuwa nimepotea kabisa na hiyo ni ibada ya mizimu, kwani wapagani wote hutegemea wafu badala ya Yesu aliye hai.(Isaya.8:19). Sisi ni makuhani(ufunuo.1.5-6), na Kristo ndiye Kuhani wetu Mkuu(waebrania.5.1-10). Sasa ni upotevu ulioje kwa kuhani kumwacha kuhani Mkuu aliye hai na kwenda kwa wafu?

  Pia wote wanaosema “hakuna wokovu duniani” wanatenda dhambi ya kumfanya Mungu mwongo na kwamba hakumleta mwanae ili atuokoe (1yohana.5:9-10). Imeandikwa “tazama,wakati uliokubalika ndiyo sasa; tazama siku ya wokovu ni sasa” (2korintho.6:2) Vile vile; Dini au dhehebu au mtu yeyote anaehubiri injili nyingine zaidi ya injili ya Kristo, yeye amelaaniwa kabisa (wagalatia.1:8-9, 1korintho.16:22).

Ndio maana Mungu alisema “Enendeni ulimwenguni mwote, mkaihubiri Injili kwa kila kiumbe. Yeyote aaminiye na kubatizwa ataokoka. Lakini ye yote asiyeamini atahukumiwa.”(Marko.16:15). Kwahiyo kila mwanfunzi wa Kristo lazima ahubiri injili hata kwa matendo inatosha… la sivyo mtu huyo anachangia kupoteza wenzake.
Mwandishi: IBRAHIM J. NZUNDA 0754 210 627

Jumatano, 17 Agosti 2016

AINA ZA WAKRISTO NA TABIA ZAO

welcome to basa ministry
WAKRISTO Ni wafuasi au watu wanaomilikiwa na kristo Yesu ,yani wako ndani ya utawala wake,na kwa Mara ya kwanza neno wakristo lilitamkwa Antiokia  LAKINI hapo kwanza likiitwa kanisa/watakatifu
    matendo 11:26  ……Na wanafunzi waliitwa Wakristo kwanza hapo Antiokia
    yohana.   15:4
AINA ZA WAKRISTO
   Zipo aina tatu za wakristo nazo ni
         1.WA MWILINI          2.WACHANGA         3.WA ROHONI

TUANGALIE KWA UNDANI TUNAWEZA KUJIFUNZA KITU

1.WAKRISTO WA MWILINI
     Hawa ni wale waliookoka siku nyingi lakini maisha yao  hayabadiliki kutokana na uvivu wa kujifunza  waebrania 5:11-12
Huyu hata ukimhimiza kujifunza atakwambia"nilishayajua kabla hujazaliwa" lakini mtu mwwenye safari wa mbinguni hawezi kuwa hivyoo maaana hawezi kummaliza kumjua MUNGU wa kweli.
*SIFA ZAO*
1,anakuwa na sura mbili ya kanisani (utakatifu)na ya mitaani (kawaida) Tito 1:16
2,akikaa na watu wasio mjua Yesu ni vigum kumtofautisha 2timotheo 2:15
3,huona aibu kujitambulisha kama ameokoka  luka 22:54-60
4,ni mtu wa mizahaa
5,wakitukanwa hujirudishia
6,wepesi kukasirika wakolosai 3:8
7,hujisifu kwa miaka mingi walivyokaa wokovuni
8,hawapend kukemewa/ kuonywa wakikosea warumi 15:14, 1korintho 4:14,wakolosai 3:16
9,waongo sana  mith 26;19
10,ni kikwazo kwa wanaotaka kuokoka

2.WAKRISTO WACHANGA
     Hawa ni wale walio amin hiv karibun, hawa hupaswa kupewa maziwa yasiyoghoshiwa ili waukulie wokovu 1petro 2:1-2
*SIFA ZAO*
1,uwezo wa kupambanua JEMA na baya ni mdogo
2,chakula kigum hawakiwezi wanahitaj zaid kufundishwa kuhusu Yesu
3,hawana uwezo wa kujua kama majaribu ni kipimo cha imani (1korintho 3:1-2)
4,hawakosekani kukutwa na utu wa kale
5,hupenda kupewa kipaumbele na kutendewa
6,wokovu ni faida yake lkn hupenda kubembelezwa
7,kusoma neno na kuomba ni mpaka wakumbushwe

3.WAKRISTO WA ROHONI
     Hawa ni wakristo waliomwamini Yesu na hudum katika neno la MUNGU, likabadili maisha YAO nao wakafananana neno (Yesu) yohana 1:1-5   matendo 9:19-22
*SIFA ZAO*
1,Hujulikana kabla hawajajitambulisha yohana 19:38-42
2,Hakuna wanachokilinda zaidi   ufunuo 2:25 mithal. 4:23  yuda 1:3
3.Hakuna mzaha kwao  zabur 1:1-6
4,ni waaminifu katika yote
5,hawana roho ya kusengenya wala kunung'unika  wafilipi 2:14
6,hutoa kipaumbele kwa mambo ya MUNGU mathayo 6:33
7,huzaa matunda maana ndio kusudi la kuitwa kwao  mathayo 13:23
8,huongozwa na ROHO na wala hawamuhuzunishi  warumi 8:14 Galatia 5:16-26
9,biblia(neno)ni rafiki yao MKUU zabur 119:11
10,ni watetezi wa IMANI yao yuda 1:20  1petro 1:5-8
  
Yaani ukiona kuna maswali yanahusu imani yako na kuyajibu huwezi hadi aje mchungaji wako basi huna uwezo kwa nafasi hiyo  matendo 4:18-21 Marko.   5:25-32
Nategemea umejijua kuwa upo kundi gani kama la kwanza piga hatua ufike la tatu kama ni la pil pia piga hatua kufika la tatu  tunaujua kuwa kuna wali umepikwa kwa harufu yake maana wali unatabia ya kusambaza harufu
JICHUNGUZE TABIA ZAKO  NA  MUNGU AKUBARIKI

MWALIM DENISY 0759735473&0658316011

Mhariri Michael BASA 0765279698,+255789799

Jumapili, 14 Agosti 2016

KUMPENDEZA MUNGU (PLEASING GOD)

PLEASE=cause to feel happy and satisfied (oxford 11th edit) kwa Kiswahili ninaweza kusema inamaana ya kufanya ahisi (awe na) furaha na kujitosheleza. Kumbe kumpendeza MUNGU inatakiwa umfanye MUNGU awe na furaha na kujitosheleza. Kwa hiyo mtu akiamua kumtumikia MUNGU inatakiwa kujitoa kwa mwili wake ili iwe dhabihu ya kumfanya MUNGU awe na furaha na wewe na aridhike na kile unachokitenda ndani ya mwili wako (jumba la roho/ROHO) warumi 12:1-2. Somo la mwili linapatikana tayari pitia hapa kulisoma  na ia somo la utatu wa binaadam pitia hapa kulisoma ili kujua kwanini MUNGU alikupata mwili na katika warumi 12 anasisitiza kuitoa miili yetu kama dhabihu iliyo hai. Ili kujua maana ya dhabihu pia pitia hapa kuiona na kwa upande wa kafara pia bofya hapa kulisoma. Katika smo leo tutajikita kwenye roho/ROHO ikiwa ndani ya mwili na jinsi MUNGU anavyotaka kutokea hapo.

JE MATENDO YAPI AMBAYO ROHO NDANI YA MWILI IKITENDA HUMPENDEZA MUNGU??
 Bila utumishi uliotukuka mbele za BWANA wetu kamwe hatuwezi kumendeza MUNGU maana mtu akiuhurumia mwili wake hawezi kujitoa kwa ajili ya MUNGU. Roho wa MUNGU anataka wewe ufunge kwa ajili ya BWANA halafu wewe katika maisha yako yote haujawahi kufunga kwahiyo cha kwanza kufikria ni mwili kukosa chakula chako cha kila siku. Na ndip shetani atakukumbusha juwa juna vidonda vya tumbo. 

Ndio maana inatakiwa kuona mwili kama vazi ambalo MUNGU kakupa ili umtumikie na siyo ushindwe kwaajili ya vazi maana yeye mwili wako umejaa uharibifu na nia yake ni uadi juu ya MUNGU. Kwa hiyo mtu akiacha kula kwaajili ya MUNGU huyo ndiyo MUNGU atapendezwa naye.
Warumi 14:11&18 ‘’Kwa kuwa yeye amtumikiaye Kristo katika mambo hayo humpendeza Mungu, tena hukubaliwa na wanadamu. Mkiwezeshwa kwa uwezo wote, kwa kadiri ya nguvu ya utukufu wake, mpate kuwa na saburi ya kila namna na uvumilivu pamoja na furaha’’

MATENDO YENYEWE NI:-

      1}KUJUA MAPENZI YA MUNGU
    Watu wengi tunashinddwwa kumpendeza MUNGU maana hatujui mapenzi yake wala ya mwanaye aliyemtuma. Maana mapenzi ya KRISTO ni kufa msalabani ili kila mtu aokolewa kupitia yeye. Naomba uelewe kitu kimoja kwamba MUNGU alichofanya msalabani ni kujitoa kwa kila mtu kupitia roho wake ili kila mmoja amjue yeye katika kweli yote na kumtii yeye kama bwana na mfalme wake. Basi hakikisha unajengwa katika imani moja roho mmoja na ubatizo mmoja. Ili mapenzi ya MUNGU YATIMIZWE NDANI YAKO. WARUMI 11:6 

    Lakini pasipo imani haiwezekani kumpendeza; kwa maana mtu amwendeaye Mungu lazima aamini kwamba yeye yuko, na kwamba huwapa thawabu wale  Na wala MUNGU hawezi kukuacha maana siku zote atakuwa pamoja nawe
yohana 8:29 Naye aliyenipeleka yu pamoja nami, hakuniacha peke yangu; kwa sababu nafanya sikuzote yale yampendezayo.

    2}  KUYATENDA MAPENZI YA MUNGU
Baada ya kuyajua maenzi ya MUNGU BABA kinachofuata ni ukamilifu wa imani ndani ya kristo. Ili kuikamilisha imani inatakiwa kuanza kuyatenda maenzi ya mungu maana imani bila matendo imekufa. James 2:26 Maana kama vile mwili pasipo roho umekufa, vivyo hivyo na imani pasipo matendo imekufa. Kingine ni ibaada katika roho na kweli Hebrews 12:28 Basi kwa kuwa tunapokea ufalme usioweza kutetemeshwa, na mwe na neema, ambayo kwa hiyo tumtolee Mungu ibada ya kumpendeza, pamoja na unyenyekevu na kicho;

 3} KUJIVIKA UTAKATIFU NA KUTENDA MAAGIZO YOTE YA BIBLIA
Utakatifu ni kama vazi kwa mkiristo yeyote ambaye anasafari ya kumuona MUNGU muumba mbingu na nchi. Maana pasi na utakatifu imani si kitu wala dini zetu si kitu . ndio maana watu wanaohubiri wengi husema dini haimpeleki mtu mbinguni wala haikufanyi wewe umuone MUNGU bali dini ni kusanyiko la watakatifu ambao kwa umoja wao kama ilivyo desturi hukutana ili kumtafuta MUNGU wa kweli na kujifunza kwa umoja wao ili kufaidiana na kuzidisha upendo ndani yao. Lakini kama huwezi kuwa kumtakatifu huwezi kumuona MUNGU. Wakolosai 2:10 mwenende kama ulivyo wajibu wenu kwa Bwana, mkimpendeza kabisa; mkizaa matunda kwa kila kazi njema, na kuzidi katika maarifa ya Mungu; 1Petro 1:15 bali kama yeye aliyewaita alivyo mtakatifu, ninyi nanyi iweni watakatifu katika mwenendo wenu wote; waebrania 12:14 Tafuteni kwa bidii kuwa na amani na watu wote, na huo utakatifu, ambao hapana mtu atakayemwona Bwana asipokuwa nao;

MATUNDA YA KUTENDA YALE YAMPENDEZAYO MUNGU
  •     Kujibiwa maombi yako  1yohana 3:21-22 na lo lote tuombalo, twalipokea kwake, kwa kuwa twazishika amri zake, na kuyatenda yapendezayo machoni pake
  •        Kuwa mwana wa MUNGU kweli
  •       Kumuona MUNGU waebrania 12:14
  •       Kuwa rafiki na ndugu wa YESU KRISTO mathayo 12:47-50
  •        Kuwa mrithi wa ufalme wa mbingu tito 3:7
Mwandishi MICHAEL BASA   0765 279 698,  +255 789 799 199

Alhamisi, 11 Agosti 2016

DHABIHU(sacrifice)

Defn
Nikitendo cha kutoa kitu chenye thamani kubwa kwa tegemeo la kupata kitu chenye thamani au umuhimu mkubwa kwako kama ishara ya ibada {Killing an animal or person and offering to GOD or gods} kutoka 10:25, 1wafalme 11:8,  zaburi 106:37. Pia katika somo letu la
NGUVU ILIYOMO KWENYE MAOMBI kipengele cha SADAKAAU KAFARA UNAYOTOA KWENYE HUO ULIMWENGU. Tulitazama kwa  upana hiki kipengele cha sadaka lakini kwenye hili tutazama kwenye ulimwengu wa nuru tu.  Unaweza kulipitia kwanza hicho kipengele ili Kupata mwanga kwanini tunatoa sadaka au dhabihu.

  •       Kwanini tunatoa dhabihu
  • ·         Kumuabudu MUNGU
  • ·         kutafuta amani na MUNGU kutoka 5:3,8:8 hesabu 7:19-25
  • ·         Kuvunja nadhiri numbers 15:3
  • ·         Kushukuru MUNGU 2nyakati 7:3&4,zaburi 50:14-23,zaburi56:12
  • ·         Kama sadaka mbele za MUNGU
  • ·     Kusafisha dhambi 1samuel 3:14 Zaburi 51:17 
Dhabihu za Mungu ni roho iliyovunjika; Moyo uliovunjika na kupondeka, Ee Mungu, hutaudharau.
        
KUNA AINA TATU ZA DHABIHU
  1.       YENYE NGUVU:-Ni ile ambayo mtu anatoa kilicho bora kutoka kwenye vile alivyo navyo
  2.      ILIYO SAFI:- Ni ile inayofuata sharia zote za biblia wakati wa kutoa dhabihu.
  3.     ILIYO HAI:- ni ile dhabihu ambayo kwa unayotoa ajili kufanya kazi ya MUNGU;hii hubaki inakushuhudia siku zote za uhai wako.

JE NI KWANINI LEO HATUTOI ZA DHABIHU ZA KUTEKETEZWA KAMA WANA WAISRAEL WALIVYOKUWA WANAFANYA???
Kwasasa hatutoi dhabihu kama wana waisrael walivyokuwa wanafanya ni kwasababu ya agano jipya ambalo mwana wa adam alikuja kuliacha.  waebrania 10:9-14,9:26
          Je kwasasa inatakiwa kutoa dhabihu za namna gani??
waebrania 13: 15 Basi, kwa njia yake yeye, na tumpe Mungu dhabihu ya sifa daima, yaani, tunda la midomo iliungamayo jina lake.
1petro 2: 5 Ninyi nanyi, kama mawe yaliyo hai, mmejengwa mwe nyumba ya Roho, ukuhani mtakatifu, mtoe dhabihu za roho, zinazokubaliwa na Mungu, kwa njia ya Yesu Kristo.


Mwandishi MICHAEL BASA   0765 279 698,  +255 789 799 199

Jumatatu, 8 Agosti 2016

NGUVU ILIYOMO KWENYE MAOMBI (..MWISHO)

 
BWANA ANAKUJA 
    
Baada ya kutazama vitu vitano muhimu wakati unapoamua kupeleka maombi yako juu ya madhabahu unayoitumia kuuufikia ulimwengu wa ROHO  katika hii sehemu ya tutaangalia sana ulimwengu wa nuru tu na ulimwengu wa giza hatutaugusa kabisaa lakini masomo yanayohusu jinsi ya kuushinda yatakuja kadri muumba atakavyonipa neema nawewe pia ukipewa neema yakusoma maana mpaka dakika hii sitaki mtu awaye mtu yeyote apotee kwa uzembe wangu bali kila atende kwa upande wake kwa bidii katika kumtafuta BWANA wa majeshi ili akaiponye nchi yake mwenyewe,familia yako, biashara yako, ndoa yako, na pia masomo yako. Vile vitano vya mwanzo ni vitu ambavyo mtu unaviishi lakini kuna vitu vitatu ambavyo vya kuwa navyo unavyoenda kuomba kwa mungu navyo vinapatikan katika 2nyakati 7:14 hapo unakuta vitu vitatu vya kuwa navyo ili kumwendea bwana ambavyo ni:-

basi tuitazame pia kujinyenyekeza inamaana ya kujishusha au kuiacha thamani yako na kuiona si kitu mbele za bwana muumba wako. Ambayo inakuwa imejengwa na mambo matatu nayo ni:-
  1.           kukubali kufundishika
  2.          kutii
  3.           kuwa na kicho(hofu)


hivi vitu vitatu mbele za bwana ni muhimu sana na vyote huanzia rohoni na kufikia kuviona nje kwa mtu ni baada ya moyo wake kuwa umejaa hivyo vitu nakuwa mmoja na vitu hivyoo ndio huyo mtu hata matunda ya roho unaweza kuyaona kwa wepesi kwake. Nje ya hapo utajijua wewe tu ukiwa unamtukia mungu bali watu wa nje hawawezi hata kulijua hilo. Hapa sizungumzii walokole nazungumzia mtu mwenye safari ya kwenda mbinguni kwamaana YESU alileta uzima wa milele ambao hakusema kuwa ni kuokoka bali ni kumjua MUNGU wa pekee na yesu kristo mwanaye aliyemtuma yohana 17:3.
                   Na pia haiishi hapo inatakiwa kujivika nila yake ili tuwe naye kweli lakini ili MUNGU asikuache inabidi kufanya yale yampendezayo kwamaana nyingine ili udumu katika uso wa bwana mungu wetu inabidi ufanye mda wote yampendezayo yeye. Ukisoma yohana 8:28-29 utakutana na neno wakati wa kufundisha yesu anasema neno siyo la kwake bali la kufundishwa na baba na akilisema au kulitenda naye baba anakuwepo mda wote naye ili kulilinda neno aliloagiza lisemwe au litendwe kwa jina lake. Unaweza usielewe kwa haraka lakini namaanisha mtazame YESU aliposema lolote muombalo kwa jina langu hilo nitalifanya. Lakini siyo kila mtu akitumia jina la yesu, yesu atatenda bali lazima uwe umeitwa kwa jina lake au umefanyika kuwa mwanafunzi wake . na ili akuhesabu hivyoo ataangalia ushikaji wako wa  maaagizo yake
           . Hapo ndipo njia mbaya nazo hutazamwa YESU aliweka kila kitu kiendacho kwa baba kipitie kwake yeye na hakuna njia nyingine na kama ukitumia jina jingine  kuomba kitu utakuwa unaomba kutoka kwa mungu wa ulimwemgu huu wala siyo mungu wa mbinguni aliyeumba mbingu na nchi 2wakorintho 4:4. Basi ndugu na rafiki yangu achana na njia zako mbaya naye MUNGU atakusikia na atakusamehe dhambi zako. Na ndipo macho yake yatafumbuka, na masikio yake yatasikiliza maombi yako 2nyakati 7:15&17. 
                    Kingine ni hofu ya kutenda dhambi inatakiwa itawale ndani yako maana utakuwa unaogopa kumkosea MUNGU na ndipo utaenenda vizuri. Na wala siyo kuogopa waumini wenzio maana hukumu nao ipo juu yao. Kwamaana kwa sheria wote tulihukumiwa kifo na mwanzo tulikuwa hapo wote. Bali ROHO alibatilisha kwa kutuhuisha kutoka uharibifu mpaka kutoharibika ambako ndiko kuwa na uzima wa milele. Basi pia tafuta kujazwa na ROHO WA MUNGU ndipo dhambi utaishinda na wala siyo kwa kushika sheria. Maana ashikaye sheria huyo ni mtumwa wa hiyo sheria bali sisi kwasasa ni watumwa wa YESU na malipo ni ROHO MTAKATIFU aletaye uzima wa milele ndani yetu.
MWISHO
MWANDISHI: MICHAEL BASA 0765279698 au+255 789 799 199

Alhamisi, 4 Agosti 2016

NGUVU ILIYOMO KWENYE MAOMBI(..mwendelezo)

IMANI YAKO JUU YA HUO ULIMWENGU.
Kila mtu anahitaji kuaminiwaau kuwafanya wengine kuwa na imani juu yake. Inaweza kuwa juu ya jambo Fulani analo weza kulifanya kwa usahihi. Watu huhitaji kuaminiwa na watu wanawaowazunguka ili:-
  1.        Aweze kufanya kitu pasi na kuingiliwa kimaamuzi
  2.       Amani ya kufanya kile anachowaza juu ya hao wamwaminio pasi na kuomba ruhusa.
  3.          Kuwa na amani juu ya hao wamwaminio.
  4.       Kuelezea kile alichofanya juu ya hao watu pasi na hofu ya kuwa inawezekana kukosea.

Mtu akiaminiwa anaweza kufanya vizuri kuliko akifanya huku anahofia kukosea. Kwasababu mtu akiaminiwa huwa anatumia kipaji chake cha ndani ambacho si rahisi kukiona bila kumpa nafasi na uhuru wa mawazo hapo ndipo imani juu ya huyo inatakiwa kuonekana. Imani huanza kidogo kidogo na baadaye hukua kutokana na matendo au faida anazopata kutoka kwa aamaniye.


Siyo ulimwengu wa nyama hata ulimwengu wa roho nao uko vivyo hivyo ndiomaana ukisoma Luka 17:6 Bwana akasema, Kama mngekuwa na imani (trust and confidence in GOD) kiasi cha chembe ya haradali, mngeuambia mkuyu (mulberry tree) huu, Ng'oka, ukapandwe baharini, nao ungewatii. Hata MUNGU mwenyewe ili afanye kazi kwako inatakiwa imani yako kumwelekea yeye iwepo na imani huwa haina shaka (kusita-sita) ndani. waebrania 10:38 Lakini mwenye haki wangu ataishi kwa imani; Naye akisita-sita, roho yangu haina furaha naye.

Kwa hiyo  Imani ni hakika ya mambo yatarajiwayo na nibayana ya mambo yasiyoonekana  waebrania 11:1. imani hujengwa na mda mwingine huharibiwa pia hubomolewa. Kwahiyo imani nikama kitu ambacho kinanguvu juu ya mtu yuda 1:20 Bali ninyi, wapenzi, mkijijenga juu ya imani yenu iliyo takatifu sana…. Iman Humjenga mtu kwa mitazamo, kiutendaji na kimazungumzo maana imani ya mtu ndio huujaza moyo wa mtu na kiujazacho moyo ndicho mtu hukitoa au hukisema. yakobo 2:26 Maana kama vile mwili pasipo roho umekufa, vivyo hivyo na imani pasipo matendo imekufa.

Imani hukua baada ya jambo ambalo lilikuwa ni tatizo kwa mtu/watu kutatuliwa kwa mfano imani ya watu wa karibu na YESU ilikuwa baada ya watu kumuona anatatua matatizo yao yanayowazunguka mfano. Kutoa pepo, kuponywa wagonjwa na kufufua wafu kwa kipindi hicho hakukuwa na watu wa kufanya hivyo. Ndiomaana mtu anafikia kutaka neno tu kwa YESU kwamaana kwa imani yake alijua hata akisema neno tu kitafanyika mathayo 15:25. 

Ili imani ikue inahitaji kuanzishwa au kujengwa. Imani hujengwa juu msingi nayo misingi ambayo imani imejengwa imetofautiana na ndizo hutofautisha kuamini kwetu. Kwamaana kuna imani juu msingi ambao ni kristo, waganga wa kienyeji, wachawi, mizimu, juu ya watu,juu ya kitu asichokijua. Imani inaweza kupimwa ndio maana mtu husema imani yangu ni ndogo juu ya hiki kitu.bas kama ndiyo hivyo bassi amini nami kuwa kipimo cha iamni kipo nacho ni AMANI. Imani hujengwa juu ya misingi bali vifuatavyo huisimamisha na kuikuza imani yako. Navyo ni elimu,mazingira, uzoefu juu ya jambo Fulani, utamaduni n.k . 

MWANDISHI: MICHAEL BASA 0765279698 au+255 789 799 199

Jumapili, 24 Julai 2016

NGUVU ILIYOMO KWENYE MAOMBI(..mwendelezo)

  
USHIKAJI WAKO WA MAAGIZO YA HUO ULIMWENGU.
Kama tulivyokwisha tazama kwenye MUUNGANO WAKO NA HUO ULIMWENGU KWA KILA SIKU tuliona kuna maagizo ya kila ulimwengu ambayo yanaujenga huo ulimwengu na kwa mtu anayeutumikia lazima ayashike hayo maagizo ili ukue katika huo ulimwengu unaotumika kwahiyo mtu yeyote anayepewa masharti ya ulimwengu inapaswa ayashike bila kuyatafutia sababu kwa ulimwengu wa ROHO maagizo yake yamegawanyka sehemu mbili nazo ni  ‘’ten bible commandments (sheria kumi za MUNGU’’ and ‘’bible instructions(maagizo)’’ sheria kumi alipewa musa pale mlima Sinai bali maagizo ya MUNGU yalikuja kwa mdomo wa nabii,kuhani na waonyaji mbalimbali waliomo kwenye biblia. Maagizo yote yanakuja ili kuikamilisha ile sheria iliyopewa musa ndio maana YESU hakuja kuitangua sheria bali kuitimiliza sheria ya musa kwamaana nyingine hakuja kuifuta ile sheria waliyoachiwa na musa bali kuielezea kwanini MUNGU BABA alitoa zile sharia kwa kipindi kile  na maana kamili ni  nini na mambo yapi amabyo kwa mdomo wa musa  au yoshua au suleimani waliyapokea bali sasa siyo maagizo tena ya kuyashika bali kwenda kwa jinsi mpya ambayo mungu anaitazamia kwao Mathayo19:8 Akawaambia, Musa, kwa sababu ya ugumu wa mioyo yenu, aliwapa ruhusa kuwaacha wake zenu; lakini tangu mwanzo haikuwa hivi. Marko 10: 5-6 Yesu akawaambia, Kwa sababu ya ugumu wa mioyo yenu aliwaandikia amri hii. Lakini tangu mwanzo wa kuumbwa ulimwengu, aliwafanya mume na mke. Ukisoma utaona kuwa alichokuwa akikisema yesu hakikuwa kwenye amri kumi bali ilikuwa ni ruhusa ya kumwacha mke. Bali tokea mwanzo haikuwa hivyo bali kwa ugumu wa mioyo yenu ndio maana mkapewa hiyo sheria. Hapa yesu anathibitisha kuwa kabisa kwa kipindi cha musa ilikuwa ni halali. Bali sasa kwenye utimilifu wa sheria agizo ni kutoachana. Hapo ndio unaweza sema kuwa sheria ya bwana haibadiliki na maagizo yake alikuja kutimilizwa na yesu kristo kwa kumuacha ROHO mtakatifu kama chombo pekee cha kukupa kile ambacho yesu hakukisema kwa kipindi hicho na baadhi ya mambo ambayo MUNGU aliyatoa au kuyasema kwa ufupi. Unapoenda kwenye madhabahu ya MUNGU wako maagizo yake anayaangalia kujua ukaribu wako nayeye. Chukuliana namimi huu mfano kwenye biblia imeandikwa waziwazi kuwa kitu pekee cha kukufanya umuone MUNGU ni utakatifu bali njia ya kumfikia MUNGU ni yesu kristo.n kwahapo hata kama ukiwa na yesu kwa vipimo vyote kama huna utakatifu huwezi kumuona MUNGU lakini pia ukiwa na utakatifu ukawa huna yesu wewe huwezi kumfikia MUNGU. Hiyo haipo kwenye amri kumi bali ipo kwenye maagizo.
MWANDISHI: MICHAEL BASA 0765279698/ +255 789 799 199

Jumapili, 3 Julai 2016

NGUVU ILIYOMO KWENYE MAOMBI(..mwendelezo)

BASA MINISTRY
MUUNGANO WAKO NA HUO ULIMWENGU KWA KILA SIKU.
Muungano wako na ulimwengu unaotumika ni muhimu sana kama unataka maombi yako yajibiwe haraka. Maana kukaa kwa mda mrefu huku ukiwa umeungwa kiroho (spiritually connected) bila kujali nini kinakukabili kwenye ulimwengu wa nyama inamaana kubwa sana.
Hebu tazama tumekuwa wadhaifu kutii baadhi ya sheria za kimungu kwasababu muda mrefu tunakuwa tumeungwa na mihangaiko ya dunia hii. Malaika hawawezi kusumbuka kushika sheria za kimungu kwasababu ni sehemu ya maisha yao. Kwa hiyo hawawezi kuuona ugumu maana asilimia mia moja wako wameungwa na ulimwengu mwingine.
Mwanadamu mwili wake ni sehemu ya dunia nao uko umeungwa na dunia, na hii ndiyo maana kama dunia ilivyo kinyume na mapenzi ya mungu ndivyo ilivyo kwa mwili wa mwanadamu. Ndio maana unaoshwa na kafara ili kuutoa kwenye maunganisho na dunia hii, na kuunga na ulimwengu mwingine wa kiroho.
Tazama yesu msalabani alifanyika kafara kwa ajili ya dhambi ikaliayo mwili  wako na kuielemea roho yako kushika maagizo ya mungu muumba wako. Kama ukisoma kwenye UTATU WA MWANADAMU utaelewa zaidi ninachokisema hapa kwa ufupi.
Ukisoma kwenye biblia YESU alimwambia mtu mmoja kuwa ukitaka kunifuata jikane kwanza mwenyewe kisha unifuate. Kwamaana nyingine achana na mahangaiko ya dunia hii kisha ujitoe kwaajili ya BWANA MUNGU WAKO. Maana  bila kukataa kuwa na mawazo mengine (double minded, spiritually you will never grow to extent that the Holy Ghost needs you to reach). Kiroho hauwezi kukua sana kwa kiwango ambacho ROHO MTAKATIFU anataka wewe ufikie .
Basi kama ndiyo hivyo tunatakiwa kupenda kuwa mbele za mungu wetu muda wote. Maana kuwa mbele za Bwana au kukaa kwenye madhabahu yake kwa muda mrefu unakuwa umeunganishwa kiroho na madhabahu ile na akili yako, roho yako na mwili wako kwa umoja wao vinakuwa mbele za Bwana. Hii ndiyo njia ya kuomba mbele ya Bwana inayotakiwa kama ilivyoandikwa kwenye mathayo 22:37.
Mwili unapaswa kunyenyekea mbele za BWANA, maana unakuwa unaonesha ishara ya utii kwenye mamlaka nyingine. Pia ni niya ya kuonesha utii wa kiroho, kwa maana ya kupondeka kwa roho huhesabika kwa matendo ya mwili isaya 66:2.
Basi kama ndivyo hivyo mwili wako ulio hekalu la ROHO na utiishwe chini ya madhabahu ya BWANA kama ROHO mwenyewe alivyoutiisha mwili wa KRISTO; hata mauti na ndipo wokovu ukaja. Hivyo hata kwako fanya nawewe utaona kama neema za bwana hazitakuzukia.

Roho yatakiwa kushika au kukumbuka maagizo na kulia mbele za bwana huku ukijitahidi sana kuufanya mwili ushike sheria za Bwana muda wote. Na nafsi yako na ijae mamlaka ya Bwana Mungu juu ya mwili wako. Na bwana wa mbinguni atakuwa nawe wala hatakuacha kama alivyokuwa na mtumishi wake YESU KRISTO.  

Wiki ijayo tutaangalie moja kati ya zile zilizosalia. MUNGU muumba mbingu na nchi akubariki sana  

Mwandishi: MICHAEL BASA 0765 279 698 , +255 789 799 199

Jumapili, 26 Juni 2016

NGUVU ILIYOMO KWENYE MAOMBI(..mwendelezo)


maombi yangu
MWENENDO WAKO KATIKA HUO ULIMWENGU UNAOPELEKA MAOMBI YAKO.
Kila ufalme unajengwa kwa mila desturi ,masharti na sheria ili uweze kusimama. Ulimwengu wa giza una-miiko yake, pia na ulimwengu wa nuru pia una-miiko yake katika ufanyaji kazi na hivyo ndivyo ulivyojengwa. Ili uenende kwenye ulimwengu kuna masharti ya kiujumla au sharia, na pia kuna masharti ya jamii moja na jamii nyingine.
Mfano jamii ya waganga wa kienyeji iko tofauti na jamii ya wachawi ingawa ni wamoja. Lakini kazi zao zinawafanya wawe tofauti kimiiko ya kiutendaji. Vivyo hivyo mitume na waalim na wao pia wanamiiko ya kiutendaji, haimaniishi kuwa kazi zake mtume haziwezi kufanana na mwalimu au mchawi hawezi kufanana na mganga, hapana hata kidogo.

Kwa maana ufanano wa kazi unajengwa na nguvu inayoshuka kwenye madhabahu wanayotumia kwenye maombi. Wasipoweka miiko huo ufalme utafitinika. Kama ilivyoandikwa “Kila ufalme ukifitinika juu ya nafsi yake, hufanyika ukiwa; tena mji au nyumba yo yote ikifitinika juu ya nafsi yake, haitasimama. Na Shetani akimtoa Shetani, amefitinika juu ya nafsi yake; basi ufalme wake utasimamaje?” (mathayo12: 24-27).

Kwahiyo ili uwe na nguvu kwenye ulimwengu wa roho inatakiwa kushika vizuri masharti ya huo ufalme unaotumika. Mfano ulimwengu wa NURU  ukitumia madhabahu ya walokole unakuta kuna kunena kwa lugha. Mtu anayenena kwa lugha hawezi kufanana kwa nguvu wakati wa kuomba na ambaye haneni kwa lugha.
Au mfano mwingine mchawi hapandi cheo pasi na kuvuka baadhi ya mitihani na pia kuna vyeo kupewa kwenye ulimwengu wa giza mpaka uwe wamekuamini sana. Halikadhallika na kwenye taasisi zetu za kawaida kwenye ulimwengu wa nyama kawaida.

Kwa ulimwengu wa nuru kwenye madhabahu ya wakristo sheria ziko wazi kwenye biblia na msharti yako ndani pia. Ukitaka uwe na nguvu zaidi mda wa kuomba inatakiwa uombe mda mrefu tena kwa mpangilio na siyo kuomba tu. Pia omba kwa kunukuu vifungu vya biblia kwenye aina ya maombi yako kama tulivyokishwa jifunza kwenye   CHRISTIAN  CULTURE.

kwa maana kutoka kwenye utangulizi wa hili somo tuliona kwamba kuna prayers na requests sasa unapopeleka “requests” hakikisha ziko kwenye mpangilio(definite) ili zikubaliwe la sivyo utakuwa unapayuka(speaking in vain). Soma AMPLIFIED BIBLE philipians 4:6 na mathew 6:7

Pia inatakiwa uache uovu  wote, kama ilivyoandikwa “Kila alitajaye jina la Bwana na auache uovu” (2Timotheo 2:19). Kwamaana uovu hautakiwi kutajwa kwako waefeso 5:3 Lakini uasherati usitajwe kwenu kamwe, wala uchafu wo wote wa kutamani, kama iwastahilivyo watakatifu;. Pia anza kufanya kazi ya MUNGU(JEHOVA YIRE). Kama tulivyokwisha ona kwenye MILANGO YA KUVUKA KABLA HUJAFA.

Hapo ndipo nguvu zako na mwenendo wako kwenye huu  ulimwengu utakapokubaliwa na kuwa mwenye nguvu na maombi yako ndivyo yatakavyokuwa yanajibiwa upesi zaidi. Maana “tangu siku za Yohana Mbatizaji hata sasa ufalme wa mbinguni hupatikana kwa nguvu, nao wenye nguvu wauteka”( mathayo11:12).  

Wiki ijayo tutaangalie moja kati ya zile zilizosalia. MUNGU muumba mbingu na nchi akubariki sana  

Mwandishi: MICHAEL BASA 0765 279 698 , +255 789 799 199
Inaendeshwa na Blogger.