Jumapili, 24 Julai 2016

NGUVU ILIYOMO KWENYE MAOMBI(..mwendelezo)

  
USHIKAJI WAKO WA MAAGIZO YA HUO ULIMWENGU.
Kama tulivyokwisha tazama kwenye MUUNGANO WAKO NA HUO ULIMWENGU KWA KILA SIKU tuliona kuna maagizo ya kila ulimwengu ambayo yanaujenga huo ulimwengu na kwa mtu anayeutumikia lazima ayashike hayo maagizo ili ukue katika huo ulimwengu unaotumika kwahiyo mtu yeyote anayepewa masharti ya ulimwengu inapaswa ayashike bila kuyatafutia sababu kwa ulimwengu wa ROHO maagizo yake yamegawanyka sehemu mbili nazo ni  ‘’ten bible commandments (sheria kumi za MUNGU’’ and ‘’bible instructions(maagizo)’’ sheria kumi alipewa musa pale mlima Sinai bali maagizo ya MUNGU yalikuja kwa mdomo wa nabii,kuhani na waonyaji mbalimbali waliomo kwenye biblia. Maagizo yote yanakuja ili kuikamilisha ile sheria iliyopewa musa ndio maana YESU hakuja kuitangua sheria bali kuitimiliza sheria ya musa kwamaana nyingine hakuja kuifuta ile sheria waliyoachiwa na musa bali kuielezea kwanini MUNGU BABA alitoa zile sharia kwa kipindi kile  na maana kamili ni  nini na mambo yapi amabyo kwa mdomo wa musa  au yoshua au suleimani waliyapokea bali sasa siyo maagizo tena ya kuyashika bali kwenda kwa jinsi mpya ambayo mungu anaitazamia kwao Mathayo19:8 Akawaambia, Musa, kwa sababu ya ugumu wa mioyo yenu, aliwapa ruhusa kuwaacha wake zenu; lakini tangu mwanzo haikuwa hivi. Marko 10: 5-6 Yesu akawaambia, Kwa sababu ya ugumu wa mioyo yenu aliwaandikia amri hii. Lakini tangu mwanzo wa kuumbwa ulimwengu, aliwafanya mume na mke. Ukisoma utaona kuwa alichokuwa akikisema yesu hakikuwa kwenye amri kumi bali ilikuwa ni ruhusa ya kumwacha mke. Bali tokea mwanzo haikuwa hivyo bali kwa ugumu wa mioyo yenu ndio maana mkapewa hiyo sheria. Hapa yesu anathibitisha kuwa kabisa kwa kipindi cha musa ilikuwa ni halali. Bali sasa kwenye utimilifu wa sheria agizo ni kutoachana. Hapo ndio unaweza sema kuwa sheria ya bwana haibadiliki na maagizo yake alikuja kutimilizwa na yesu kristo kwa kumuacha ROHO mtakatifu kama chombo pekee cha kukupa kile ambacho yesu hakukisema kwa kipindi hicho na baadhi ya mambo ambayo MUNGU aliyatoa au kuyasema kwa ufupi. Unapoenda kwenye madhabahu ya MUNGU wako maagizo yake anayaangalia kujua ukaribu wako nayeye. Chukuliana namimi huu mfano kwenye biblia imeandikwa waziwazi kuwa kitu pekee cha kukufanya umuone MUNGU ni utakatifu bali njia ya kumfikia MUNGU ni yesu kristo.n kwahapo hata kama ukiwa na yesu kwa vipimo vyote kama huna utakatifu huwezi kumuona MUNGU lakini pia ukiwa na utakatifu ukawa huna yesu wewe huwezi kumfikia MUNGU. Hiyo haipo kwenye amri kumi bali ipo kwenye maagizo.
MWANDISHI: MICHAEL BASA 0765279698/ +255 789 799 199

Jumapili, 3 Julai 2016

NGUVU ILIYOMO KWENYE MAOMBI(..mwendelezo)

BASA MINISTRY
MUUNGANO WAKO NA HUO ULIMWENGU KWA KILA SIKU.
Muungano wako na ulimwengu unaotumika ni muhimu sana kama unataka maombi yako yajibiwe haraka. Maana kukaa kwa mda mrefu huku ukiwa umeungwa kiroho (spiritually connected) bila kujali nini kinakukabili kwenye ulimwengu wa nyama inamaana kubwa sana.
Hebu tazama tumekuwa wadhaifu kutii baadhi ya sheria za kimungu kwasababu muda mrefu tunakuwa tumeungwa na mihangaiko ya dunia hii. Malaika hawawezi kusumbuka kushika sheria za kimungu kwasababu ni sehemu ya maisha yao. Kwa hiyo hawawezi kuuona ugumu maana asilimia mia moja wako wameungwa na ulimwengu mwingine.
Mwanadamu mwili wake ni sehemu ya dunia nao uko umeungwa na dunia, na hii ndiyo maana kama dunia ilivyo kinyume na mapenzi ya mungu ndivyo ilivyo kwa mwili wa mwanadamu. Ndio maana unaoshwa na kafara ili kuutoa kwenye maunganisho na dunia hii, na kuunga na ulimwengu mwingine wa kiroho.
Tazama yesu msalabani alifanyika kafara kwa ajili ya dhambi ikaliayo mwili  wako na kuielemea roho yako kushika maagizo ya mungu muumba wako. Kama ukisoma kwenye UTATU WA MWANADAMU utaelewa zaidi ninachokisema hapa kwa ufupi.
Ukisoma kwenye biblia YESU alimwambia mtu mmoja kuwa ukitaka kunifuata jikane kwanza mwenyewe kisha unifuate. Kwamaana nyingine achana na mahangaiko ya dunia hii kisha ujitoe kwaajili ya BWANA MUNGU WAKO. Maana  bila kukataa kuwa na mawazo mengine (double minded, spiritually you will never grow to extent that the Holy Ghost needs you to reach). Kiroho hauwezi kukua sana kwa kiwango ambacho ROHO MTAKATIFU anataka wewe ufikie .
Basi kama ndiyo hivyo tunatakiwa kupenda kuwa mbele za mungu wetu muda wote. Maana kuwa mbele za Bwana au kukaa kwenye madhabahu yake kwa muda mrefu unakuwa umeunganishwa kiroho na madhabahu ile na akili yako, roho yako na mwili wako kwa umoja wao vinakuwa mbele za Bwana. Hii ndiyo njia ya kuomba mbele ya Bwana inayotakiwa kama ilivyoandikwa kwenye mathayo 22:37.
Mwili unapaswa kunyenyekea mbele za BWANA, maana unakuwa unaonesha ishara ya utii kwenye mamlaka nyingine. Pia ni niya ya kuonesha utii wa kiroho, kwa maana ya kupondeka kwa roho huhesabika kwa matendo ya mwili isaya 66:2.
Basi kama ndivyo hivyo mwili wako ulio hekalu la ROHO na utiishwe chini ya madhabahu ya BWANA kama ROHO mwenyewe alivyoutiisha mwili wa KRISTO; hata mauti na ndipo wokovu ukaja. Hivyo hata kwako fanya nawewe utaona kama neema za bwana hazitakuzukia.

Roho yatakiwa kushika au kukumbuka maagizo na kulia mbele za bwana huku ukijitahidi sana kuufanya mwili ushike sheria za Bwana muda wote. Na nafsi yako na ijae mamlaka ya Bwana Mungu juu ya mwili wako. Na bwana wa mbinguni atakuwa nawe wala hatakuacha kama alivyokuwa na mtumishi wake YESU KRISTO.  

Wiki ijayo tutaangalie moja kati ya zile zilizosalia. MUNGU muumba mbingu na nchi akubariki sana  

Mwandishi: MICHAEL BASA 0765 279 698 , +255 789 799 199
Inaendeshwa na Blogger.