Jumatatu, 13 Novemba 2017

NJIA SABA ZA KUKUSAIDIA KUIACHA DHAMBI INAYOKUSUMBUA.

BWANA YESU atukuzwe ndugu yangu. Karibu tujifunze Neno la MUNGU aliye hai.
Dhambi ni kosa la kwenda kinyume na utaratibu wa MUNGU.
Dhambi ni uasi kwa MUNGU.
Dhambi ni kulikataa kusudi la MUNGU.
Dhambi ni matendo maovu yote atendayo mwanadamu mbele za MUNGU.

Warumi 6:12 '' Basi, dhambi isitawale ndani ya miili yenu ipatikanayo na mauti, hata mkazitii tamaa zake;''mKama kuna kitu cha kwanza ambacho mwanadamu anatakiwa kushughulika nacho basi ni kuacha dhambi ili kuishi maisha matakatifu.

Kwanini tunajifunza njia hizi saba za kukusaidia kuacha dhambi?

Ni kwa sababu hakuna siri kwa MUNGU.Mithali 15:3 ''Macho ya BWANA yako kila mahali; Yakimchunguza mbaya na mwema.'' Kwa MUNGU matendo yetu yote yako wazi mbele zake.
Na kama mtu asipoacha dhambi na asipotubu maana yake matendo yake yataendelea kukaa, na siku ya mwisho kama matendo yake yalivyokuwa angali alipokuwa duniani ndivyo atakavyolipwa siku ya mwisho.Obadia 1:15 ''Kwa maana hiyo siku ya BWANA i karibu juu ya mataifa yote; kama ulivyotenda, ndivyo utakavyotendwa; malipo yako yatakurudia juu ya kichwa chako mwenyewe.''
Waliotenda mema katika KRISTO wataupata uzima wa milele na waliotenda mabaya wote watapokelewa na ziwa la moto. Ni muhimu sana kuacha dhambi. Ni Muhimu sana kutafuta njia za kuiacha hiyo dhambi inayokusumbua. 1Timotheo 1:15 ''Ni neno la kuaminiwa, tena lastahili kukubalika kabisa, ya kwamba KRISTO YESU alikuja ulimwenguni awaokoe wenye dhambi; ambao wa kwanza wao ni mimi.'' Kumbuka kuwa ukimpokea YESU na ukatubu kwake hakika dhambi zako zote zitafuta na MUNGU hatazikumbuka tena. Lakini usipotubu na kuokoka hakika uovu wako utadumu hadi siku unaondoka duniani maana hukutubu na kuacha uovu huo. Kuna watu hudhani kwamba hawawezi kuacha dhambi lakini ukweli ni kwamba huo ni uongo tu wa shetani kuhakikisha mwanadamu huyo haendi uzima wa milele. Kama kuna dhambi inakutesa na hujui jinsi ya kuiacha nakuomba jifunze ujumbe huu na uuhamishie katika matendo utashinda.

NJIA SABA ZA KUKUSAIDIA KUIACHA DHAMBI INAYOKUSUMBUA.

1. Kumtii MUNGU kupitia Neno lake Biblia.
Yakobo 4:7-10 '' Basi mtiini MUNGU. Mpingeni Shetani, naye atawakimbia. Mkaribieni MUNGU,naye atawakaribia ninyi. Itakaseni mikono yenu, enyi wenye dhambi, na kuisafisha mioyo yenu, enyi wenye nia mbili. Huzunikeni na kuomboleza na kulia. Kucheka kwenu na kugeuzwe kuwa kuomboleza, na furaha yenu kuwa hamu. Jidhilini mbele za BWANA, naye atawakuza. ''
·        Njia muhimu za kumtii MUNGU ni kumpinga shetani.
·        Ni kujitenga na kila jambo la kishetani.
·        Kumtii MUNGU ni kumwabudu katika Roho na kweli.
Kama kuna dhambi inakutesa ni kwa sababu tu hujaamua kumtii MUNGU. Kumtii MUNGU ni kuiacha dhambi hiyo kwa nguvu kisha kuhamishia nguvu zako kwa MUNGU. Ndugu anza kuanzia leo kumtii MUNGU na Neno lake utashinda.

2. Kuishi maisha matakatifu.
1 Petro 1:15 '' bali kama yeye aliyewaita alivyo mtakatifu, ninyi nanyi iweni watakatifu katika mwenendo wenu wote;'' Mtakatifu kinyume chake ni mtenda dhambi. Kama unataka kushinda dhambi basi acha dhambi na kuanza kutenda mema, huo ndio utakatifu. Anza tu kuipenda mbingu kwa kuamua kuishi maisha matakatifu. Jitenge na kila vishawishi vilivyokufanya uingie dhambini. Jitenge na marafiki wabaya wote. Acha tabia zako zote ambazo ni za dhambi. Acha ulevi, uzinzi, uongo na kila dhambi. Amua tu kumpendeza MUNGU kwa kuanza kuishi maisha matakatifu kila siku. Kama ukiamua hakika utaona nguvu ya MUNGU ya kukusaidia kuishi maisha matakatifu. Kumbuka huwezi kuishi maisha matakatifu kama uko mbali na MUNGU, uko mbali na Neno la MUNGU, Uko mbali na watakatifu wengine ambao watakusaidia kusonga mbele vyema, ndio maana ni muhimu sana wewe ukaokoka na kuanza kuwa mhudhuliaji wa vipindi kanisani ili ukue kiroho na ukikua kiroho itakuwa rahisi sana kwako kushinda dhambi.

3. Kuokoka.
Yohana 3:16-21 ''Kwa maana jinsi hii MUNGU aliupenda ulimwengu, hata akamtoa Mwanawe pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele. Maana MUNGU hakumtuma Mwana ulimwenguni ili auhukumu ulimwengu, bali ulimwengu uokolewe katika yeye. Amwaminiye yeye hahukumiwi; asiyeamini amekwisha kuhukumiwa; kwa sababu hakuliamini jina la Mwana pekee wa MUNGU. Na hii ndiyo hukumu; ya kuwa nuru imekuja ulimwenguni, na watu wakapenda giza kuliko nuru; kwa maana matendo yao yalikuwa maovu. Maana kila mtu atendaye mabaya huichukia nuru, wala haji kwenye nuru, matendo yake yasije yakakemewa. Bali yeye aitendaye kweli huja kwenye nuru, ili matendo yake yaonekane wazi ya kuwa yametendwa katika MUNGU. '' Kuokoka ni jambo la muhimu sana kama unataka kuzishinda dhambi. Kuokoka ndio mwanzo wa mwanadamu kumwabudu MUNGU katika Roho na kweli. Kuokoka ni kumpokea BWANA YESU kama Mwokozi wako. Hakuja jambo zuri na muhimu kwa kila mwanadamu kama kumpokea YESU na kuanza kuishi maisha matakatifu. Kama unataka kuishinda hiyo dhambi nakuomba okoka na uwe mhudhiliaji wa ibada, huko kanisani utapata maarifa sahihi ya kukusaidia kushinda dhambi na mambo ya ulimwengu.

4. Kujitenga na dhambi.
Warumi 6:23 '' Kwa maana mshahara wa dhambi ni mauti; bali karama ya Mungu ni uzima wa milele katika Kristo Yesu Bwana wetu.'' Biblia iko wazi sana ikisema kwamba dhambi ina matokeo mabaya sana. Dhambi ina mshahara na huo mshahara unaitwa mauti yaani kutengwa na MUNGU. Na mauti hiyo kama Mwanadamu huyo hatatubu maana yake mauti hiyo ya dhambi itazaa jehanamu. Kama unataka kushinda dhambi hakikisha unajitenga na kila dhambi. Kila kisababishi cha dhambi hakikisha unakaa mbali nacho. Kama ni wanadamu ndio hukushawishi kuingia dhambini nakuomba leo amua kuwa karibu na YESU mwenye uzima wako. tii Neno la MUNGU utashinda. Kama unaweza kuacha kula chakula fulani ulichokatazwa kula na daktari, basi mimi naamini kabisa kwa njia kama hiyo hiyo unaweza kuamua kuacha dhambi zote, maana ukitenda dhambi kuna madhara kama ambavyo ukila chakula kile ulichokatazwa na daktari. Ndugu, amua tu kutoka moyoni mwako kuacha dhambi zote na utabarikiwa rohoni na mwilini.

5. Kuutumia muda wako wote vizuri na kwa malengo mema.
Waefeso 5:15-17 ''Basi angalieni sana jinsi mnavyoenenda; si kama watu wasio na hekima bali kama watu wenye hekima; mkiukomboa wakati kwa maana zamani hizi ni za uovu. Kwa sababu hiyo msiwe wajinga, bali mfahamu ni nini yaliyo mapenzi ya BWANA.'' Biblia inakushauri kuukomboa wakati maana nyakati hizi ni nyakati za maovu mengi. Muda ambao unautumia disko ungeutumia kwa MUNGU ungeziepuka dhambi. Muda ambao unautumia kuzini ungeutumia katika maombi ungeepuka dhambi. Dhambi unaweza ukaishinda kwa kuamua tu kuutumia muda wako vizuri. Kama rafiki yako anakuita ili mkafanye mabaya hakikisha muda huo wewe utumie kwa MUNGU. Hudhuria semina za Neno la MUNGU. Hudhuria mikutano ya injili. Nenda kanisani na utumie muda wako mwingi katika mabo ya MUNGU utashinda
.
6. Kufunga na kuomba.
Mathayo 17:21 ''Lakini namna hii haitoki ila kwa kusali na kufunga.'' Kazi mojawapo ya maombi ni kuutiisha mwili ili tamaa mbaya zisiinuke. Kazi mojawapo ya maombi ya kufunga ni kuifanya roho yako iutawale mwili na sio mwili kuitawala roho. Kama huwa huwezi kupata muda wa kuomba ni ngumu kushinda ya dunia. Kama huwa huwezi kupata muda wa kufunga na kuomba ni ngumu kushinda dhambi. Nakushauri kuanzia leo uwe na muda wa kuomba na kufunga itakusaidia. Sio yale maombi ya kuombea chakula tu na wewe unajiita muombaji, wala sio yale maombi ya kabla ya kulala unaomba dakika moja na wewe unajiita muombaji bali maombi ya kudumu na ya muda mrefu. Sio yale maombi ya kukariri na wewe ujaiita muombaji, bali ni maombi yanayotoka katika moyo wako kwa imani sio kukariri.
Ø Tafuta ushindi wako katika maombi.
Ø Ita utakatifu kupitia maombi yako.
Ø Ita nguvu za kuishinda dhambi kupitia maombi.
Ø Utiishe mwili wako kupitia maombi na kufunga.
Hakika ukizingatia utashinda.

7. Kuenenda kwa ROHO MTAKATIFU.
Wagalatia 5:16 ''Basi nasema, Enendeni kwa ROHO, wala hamtazitimiza kamwe tamaa za mwili.'' Kazi mojawapo ya ROHO wa MUNGU ndani yetu ni kutusaidia kushinda mambo yote ya ulimwengu. Changamoto ya wanadamu ni jinsi ya kumpata huyo ROHO MTAKATIFU maana yeye hachangamani na uovu, yeye ni mtakatifu na akiingia ndani yako atakusaidia kuishi maisha matakatifu ila kama tu ukimtii. Mambo mengi yanayokuja mbele yako ni mapando ya giza ili kukufanya utende dhambi, lakini akiwapo ROHO wa MUNGU atakusaidia jinsi ya kuepuka dhambi. Unaweza kukuta Binti unaitwa na rafiki yako, yule rafiki yako anakuwa amepanga akupe madawa ya kulevya kisha atembee na wewe, Kama una ROHO wa MUNGU ni lazima tu atakukataza kwenda maana yeye anajua jambo kabla hata halijatokea. ukimtii ROHO wa MUNGU utashinda.

Asante kama unanielewa ndugu yangu.
BWANA YESU Amekaribia Kurudi.
Je, Umejiandaaje?
Je, Unaendeleza Dhambi Ili Siku Ile Uachwe Na BWANA YESU? Je, Umeshika Wokovu Na Utakatifu Hata Unyakuliwe Siku Ile Kwa Ajili Ya Kwenda Uzima Wa Milele?
Majibu Sahihi Yako Moyoni Mwako Ila Nakusihi Mpokee BWANA YESU Kama Hujampokea Na Nakusihi Ishi Maisha Matakatifu Ukiwa Ndani Ya Wokovu. Vya Dunia Tulivikuta Na Tutaviacha. Ndugu, Vya Dunia Visikupotezee Muda Wako Hata Ukasahau Kuokoka. Vya Dunia Visikupotezee Muda Wako Hata Ukasahau Wokovu Wa BWANA YESU Kwako.
Ni mimi ndugu yako Peter M Mabula.
Mtenda kazi katika shamba la BWANA YESU. 0714252292.
mabula1986@gmail.com
Ubarikiwe sana kwa kusoma somo hili.

Jumapili, 12 Novemba 2017

MTAZAMO WANGU

Usimkosee Mungu kwa vitu vitatu naam kwa vitu vinne hautakiwi kuikosa mbingu
  1. TUMBO
  2. MAVAZI
  3. UPAKO
  4. NDOA

1.    Hakuna kitu kizuri kama kula na kunywa mbele za Bwana maana nayo ni karama aisee {mhubiri 3:13 Tena ni karama ya Mungu kila mtu apate kula na kunywa, na kujiburudisha kwa mema katika kazi yake yote.} hata mimi napenda kula na kunywa sana na kufurahia kila chakula na kinywaji changu. Lakini kuna kitu cha kuchunga kila karama ina mipaka yake hata karama ya kulihudumia tumbo inamipaka yake tena mikubwa. Mwanzo 2:16-17{Bwana Mungu akamwagiza huyo mtu, akisema, Matunda ya kila mti wa bustani waweza kula,walakini matunda ya mti wa ujuzi wa mema na mabaya usile, kwa maana siku utakapokula matunda ya mti huo utakufa hakika}. Umepewa kula na kunywa na kufurahi lakini yakumbuke masharti ya kula na kunywa n siyo kujiendea kama usiye na akili. Huo mwili unaohitaji chakula inatakiwa upate nguvu na afya siyo kufa ndio maana adam akaewa angalizo mappema kabisaa. Naamini katika biblia sheria ya kwanza ilihusu chakula kwa mwanadam na ndio agizo la kwanza kabisaa. Kuna watu wanahisi kila kitu ni chakula na kunywa tu huku afya zao au uzima ndani yao unatetereka kila siku na magonjwa ya ajabu ajabu yanaongezeka. Wataalam wa afya wanadai kuwa ulaji mbaya umefanya magonjwa yasoyoambukiza kuongezeka. 
                   Kwenye angalizo la kwanza lilikuwa ni kula chakula ulichoewa mwenyewe na ambacho unauwezo wa kuamua ule nini na nini usile?. Basi tumbo hutamani kila kitu kwa mda wote bali roho hutafuta ibada kwa kila jambo hapa nasemea mtu aliyempokea KRISTO nasivinginevyo. Kuna watu siyo Amani ya KRISTO ndani yao bali ni mazoea yao ndio huamua ndani yao. Ni kweli andiko lasema wazi kuleni vyote kwaajili ya dhamiri lakini kumbuka siyo kila chakula chafaa kuliwa na mwandam na si kila kinywaji cha chafaa kwa afya yako anza sasa kula na kunywa kwaajili ya roho yako mwenyewe na kwaajili ya uzima wako ndani ya KRISTO. Kula kwaajili ya kufurahia hii karama lakini uwe na KIASI katika kula kwako na kunywa kwako. Kuna watu wamejaa ubatili kwaajili ua kula tu na kunywa. Nawaonya mapema isafisheni mikono yenu na muzitakase nia zenu ili roho zimrudie YEYE aliye juu na yote na juu ya vyote ni Bwana wa vyote pia na ndie aliye mmiliki wa vyote Mungu wa enzi na miliki zote. Kwamaana wokovu wafaa sana kwake yeye aliye nao na Roho wa ahadi afaa kwa vyote na yote pia. Kuna watu walimfuta Yesu kwasababu tu walikula mikate waksahau kuwa hawajanywa maji ya uzima, je wewe tumbo lako limeokoka na vyakula vya laana na makao ya kuzimu yako nje ya viuongo vyako. Mkate usikutoe kwa Yesu kwamaana 1wakolintho 6:13 Vyakula ni kwa tumbo, na tumbo ni kwa vyakula; lakini Mungu atavitowesha vyote viwili, tumbo na vyakula. Lakini mwili si kwa zinaa, bali ni kwa Bwana, naye Bwana ni kwa mwili. 
       Utapata hasara kama uliwekeza kwa tumbo kwamaana hakuna kitakachobaki kwako siku ya hukumu lakini wewe basi jifariji kwa hii yohana 6:51 Mimi ndimi chakula chenye uzima kilichoshuka kutoka mbinguni; mtu akila chakula hiki, ataishi milele. Na chakula nitakachotoa mimi ni mwili wangu, kwa ajili ya uzima wa ulimwengu. Hakikisha tumbo lako limejaa hiki chakula kila siku za Maisha yako 
           Mandishi MICHAEL BASA 0765279698

Alhamisi, 9 Novemba 2017

CHURCH GIRLS AND CHURCH BOYS

Siku moja nilikuwa engineering pale SUA najisomea mara akapita msichana mmoja kavaa tisheti imeandikwa church girl. Nilishangaa kwa mda kisha nikajiuliza huyu ni nani? mbona mavazi yake na mwonekano wake hayana hilo neno?. Nikagundua kuwa ni mkristo mmojawapo katika makanisa ya kikristo. Kwa mtazamo wa nje linaonekana ni neno zuri lakini kwa mtazamo wa ndani halina maana yoyote. Subiri nikuambie kitu mwana wa mungu aliye hai. Kinachotakiwa kumtangaza kristo ni matendo  yako siyo maandishi ya kwenye nguo. Kristo aliyekufa msalabani na kwakufuata maagizo yake huwa hakuna mwana kanisa fulaani kwamaana kwake sisi kwa umoja wetu ni mwili mmoja. Hautakiwi hata mara moja kuwa church girl wala church boy. Kwa maana hilo ni mojawapo la tendo la mwilini kwamaana kanisa ni hali ya kupatanishwa kwa mwili na siyo roho. Soma biblia tena uone kama kuna sehem yoyote ambayo yesu anaongelea kujazwa mwili. Bali roho yako ndio inayopaswa kukaa kwa YESU na ukijazwa ROHO kamwe hauwezi kuwa wa mwilini tena bali utakuwa mtu wa kuishinda dhambi. Tazama church boys na church girls wengi. Utaona maisha yao ya kiroho ni machanga kwa maana upendo wao hauko kwa kristo bali kwa jengo na jina la dhehebu analotumika. Lakini kristo ambaye kwa pendo lake ndio tunapaswa kuliishi na kulitangaza ni uzima wa milele tu. Na uzima wa milele ndio huu wakujue wewe Mungu mmoja wa kweli na wapekee na Yesu kristo uliyemtuma. Kuna wengine wameenda mbali zaidi kwa kuanzisha mijadala kuhusu dhehebu Fulani ni bora kuliko dhehebu Fulani. Sikiliza nikuambie huo siyo upendo wa kristo kwa maana vipimo vya ubora vipo katika maarifa ya kujua Mungu anataka nini kwa mda huo juu yako. Soma tena biblia uone kama pendo la kristo ndilo hilo unalotangaza wewe kwenye mijadala yako. Yesu alikufa msalabani kwaajili ya watu wote na siyo baadhi ya watu tu. Hakuna ubora wa dhehebu ndani ya KRISTO mwenyewe bali kuna ubora wa mtu atendaye mema ndani ya KRISTO. Kwahiyo hayo majengo yanayowachanganya mpaka mkaanza kujifunza historia ya dhehebu lenu ili ukitembea ujisifu kwa wengine ni upuuzi na kujilisha upepo. Soma neno ujazwe Roho mtakatifu uone kama utabaki mtu wa kuwaza chini ya viwango vya kiroho kiasi hicho. Unamkuta mtu  kajiandika I LOVE JESUS lakini maisha yako hayaakisi hata kidogo hilo neno hata mawazo yako tu hayajui kama kweli kuna YESU ndani yako. Badilika ndugu mpende YESU kwa moyo wako wote, roho yako yote, matendo yako yote, nafsi yako yote na akili zako zote. Ili yeye aliye Bwana wa rehema na neema akutakase mwili wako, nafsi yako na roho yako siku zote za maisha yako. Biblia inasema wazi kabisaa kuwa utatambuliliwa kwa matunda yako mathayo 7:20. wala siyo kwa maandishi kwenye mashati yenu wala siyo kwa kuwa church girl and church boy ambao ni ushetani mkubwa ndani ya kanisa.  

Jumatatu, 6 Novemba 2017

NDANI YA DINI YANGU----5


MATENDO YAKE HUMTANGAZA KRISTO{kusoma utangulizi bofya hapa}

"Usiangalie matendo yangu bali sikia nasema nini kwako au fuata ninachosema" moja ya hoja maarufu sana kwa wakristo wengi wasiojua kwanini wanamfuata KRISTO. Ni kweli Mungu huichunguza mioyo kama biblia inavyosema kwenye mstari wa 1 Samuel 16:7…Bwana haangalii kama binadamu aangaliavyo; maana wanadamu huitazama sura ya nje, bali Bwana huutazama moyo. Subiri nikuambie kitu kimoja ambacho unatakiwa ukielewe kutoka kwangu na si kwamwingine biblia ni kitabu kitakatifu huwa kinachanganya kama usipoweza kufunuliwa kwa Roho mtakatifu. Kuna wachungaji kwa kutojua maana halisi ya neno au msitari huitafasiri vibaya na huenda nawewe ulichukua kwake. 
             Wengine huitafasiri kwaajili ya kuficha udhaifu wao na hao ndio laana imekaa kwao na ndio waalim wa uongo walionenwa ujihadhari nao mapema nakuonya pia. Kuna siku nilikuwa nafundisha nakumbuka nikataka kutoa mfano nikaonya mapema natumia tafsiri isiyo takiwa kuitumia kwenye kila mazingira bali ni kwa mazingira ya mfano huu tu. Sasa kama nisingetoa hiyo kuna watu wangechukua kama ni tafsiri ya kijumla na kuna mazingira ingepingana na wao wenyewe kutumika. Swali la msingi JE NI KWELI MUNGU HUANGALIA MOYO TU? KAMA NDIO KWANINI NIANDIKE MATENDO? KAMA HAPANA JE HUO MSITARI NI WAUONGO?. Nikutoe hofu kwanza kama umeshaanza kuwaza nitajibuje kwenye hayo maswali mawili hapo juu. Kwa msitari huo hauna tatizo kabisaa kama ukiutumia kumuonya mtu ambaye kwa nje ni msafi au unasisitiza usafi ndipo unasema Bwana haangalii nje bali huangalia mioyo na kuvichunguza viuno yeremia 17:10{Mimi, Bwana, nauchunguza moyo, navijaribu viuno, hata kumpa kila mtu kiasi cha njia zake, kiasi cha matunda ya matendo yake}.
         Je unakumbuka kuwa dhambi huanzia ndani ya mtu na siyo nje kama wengi wanavyodhani soma tena mwanzo 4:7{Usipotenda vyema dhambi iko, inakuotea mlangoni, nayo inakutamani wewe, walakini yapasa uishinde.}jiulize sasa hapo mlango ni upi?. Soma tena ayubu{Job 38:17 Je! Umefunuliwa malango ya mauti, Au umeyaona malango ya kuzimu?}. Uone kitu kingine kipya kabisaa ndipo ujue kuwa biblia haishii hapo wewe unapoona kwa upeo wako wala kwa maandiko ya BASA tu. Pia maandiko siyo ulokole na wala siyo UKRISTO kwamaana UKRISTO ni kuwa ndani ya KRISTO na ULOKOLE ni kumiminwa ndani ya ROHO MTAKATIFU. Ukitaka kuwa MKRISTO kweli jifunze msalabani sana na ukubali na kutii kila andiko kama lilivyo bila kusema mtumishi fulani alisema hivi au vile. Kuna mtu mmoja alifundishwa na watu wawili tofauti mtu wa kwanza alifundisha kutopenda kumpa mkono kila mtu na hakuelezea kwanini na kwa mazingira gani?. Mtu wa pili akafundisha kuwapenda wale wa nje na kuwasalimia kwa kupeana mikono na kama ni jinsia moja unaweza kuwakumbatia kabisaa. Swali likaja kwangu sasa je amfuate nani kwamaana wote ni wachungaji na anawaamini sana na hahisi kama kuna mmoja kasema uongo. Mimi nikacheka kisha nikamfundisha chimbuko la mafundisho yote mawili na kwanini yapo hivyo na kwenye ulimwengu wa roho yanachukuliwaje kisha na yeye afuate lipi?. Lakini nilichogundua kwa huyu mtu hajazama ndani ya Roho mtakatifu vizuri ndio maana hakuelewa ashike lipi sasa?. 
       Ndio maana nasema kwamba matendo yako yote yanatakiwa yamhubiri KRISTO, watu waduniani wanaangalia porn na wewe mkristo unaangalia halafu unataka uione mbingu sahau tu. Mungu siyo wa mzaha kiasi hicho aisee tena pole sana. Watu wanajitesa kwa kufunga na kuomba na kukesha wewe unakula siku 365 kwa mwaka na kulala masaa yote. Kuomba dakika tano nyingi halafu unataka eti ufunuliwe kwenye ulimwengu wa roho sahau tu. Mtu unatembea uchi halafu unataka Yesu aonekane kwako au ajidhihirushe labda utumie pepo aisee. Hakika Mtu ambaye roho yake inamwabudu Mungu kweli au moyo wake unakicho cha Bwana halafu kwa nje anachotoa ni uongo, uasherati, wizi, uuaji, chuki, uchonganishi, ufiraji, kuchora tattoo, huombi, husomi neno, disko umo, sehem za laana hukosi. Wasioamini wanassema kabisaa kama nawewe ukiingia mbinguni basi mimi nitakuwa malaika {mathayo 5:20}halafu unajibu utaona Mungu anaangalia moyo wa mtu haangalii matendo pumbavu kabisaa mwana wa laana wewe. 
       Wewe ndio unafanya injili inakuwa ngumu kwa watu kuipokea na kuitii kwamaana haoni tofauti yako wewe ambaye ni mfuasi wa KRISTO na yeye ambaye bado anaabudu miungu mingine. Basi tuangalie matendo yako kama Mungu anayatazama kama moyo au vyote viwili. Tito 1:16 Wanakiri ya kwamba wanamjua Mungu, bali kwa matendo yao wanamkana; ni wenye machukizo, waasi, wala kwa kila tendo jema hawafai. Huyo siyo mimi bali ni walaka kwa tito ambao mwandishi anaonesha kitu kidogo kwamba kuna matendo ambayo ukiyafanya unakuwa unamkataa Mungu kabisaa. Mkirsto mwenzangu hujui kwamba mdomo wako unaweza kuwa unamkubali Mungu kweli lakini mwili wako unafanya ibada za miungu kila siku. Badilika wewe mkristo mwenzangu hakikisha matendo yako yanatoa kile kilichoko ndani ya moyo wako ambacho Yesu mwenyewe alifundisha. Hatuna kipimo kingine cha utakatifu isipokuwa matunda ya ROHO MTAKATIFU.

Mwandishi: MICHAEL BASA 0765279698/+255789799199

Alhamisi, 2 Novemba 2017

NDANI YA DINI YANGU---4

AMEJAZWA ROHO MTAKATIFU (KUSOMA UTANGULIZI BOFYA HAPA)
      Kuna Rafiki zangu wa dhehebu Fulani Roho kwao ni stori za zama za kale sana kabla ya dunia kuwepo. Huwa nacheka tu kwamaana hadithi za kizee zisizokuwa za dini ndizo zimekuwa sahihi kwao na usahihi wa neno umekuwa ni upotofu kwao. Kuna wengine pia ukiwakuta wanajiita makanisa ya kiroho sikatai maana wao wanajiona hivyo wanategemea viongozi wao kwa kila jambo hata ambalo Mungu anatakiwa kuonekana kwa uwazi kwao wenyewe wanamsubiria mchungaji wao au nabii wao. Sipingi kuwafuata maana hata mimi nina baba zangu wa kiroho lakini hawatakiwi kuchukua nafasi  ya Mungu. Yesu alitoa uhuru kwa kila mtu kujiombea nasiyo kutegemea mtu Fulani. Ndio maana kwa biblia ikasema Bwana anazichunguza nyoyo na huvijaribu viuno. Sasa wewe na huyo kiongozi hamjui kuwa mnamtenda Mungu dhambi. Je mmesahau kuwa amelaaniwa mtu yule amtegemeeaye mwanadam??. Wengine pia kuna roho kiburi na roho uhuru wamewaingia hao hata ukiwahubiria vipi hawaelewi kitu. Tena chunga unaweza kuambulia matusi yanguvu kweli au ukaishiwa kutengwa na kanisa lako. Huwa naukumbuka sana wimbo wa MUNISHI unaitwa “WANAMWABUDU NANI?”. 
      Wengine wamejazwa roho wakajihisi watamuona Mungu wakati biblia imeagiza kujazwa ROHO tena siyo ROHO tu bali awe mtakatifu ambaye anakuja kwako kwa kazi zifuatazo:-
     ➤KUKUFUNDISHA 
     KUKUONYA
     KUKUELEKEZAKUKUJULISHA MAMBO YAJAYO
     ➤KUKUFUMBULIA MAFUMBO MAKUU YA MUNGU
     ➤KUKUPA AMANI
     KUSHUHUDIA PAMOJA NA NAFSI YAKO KUWA WEWE NI MWANA WA MUNGU
     KUKUOMBEA
     KUKUONGOZA
     KUKUPA HUDUMA KWAAJILI YA UFALME
       Unapomkataa Roho mtakatifu inamaana umekataa vyote hivyo. Inakuwa ni ngumu sana kwa wewe kujua mipango ya Mungu juu yako kwa wakati huo. Pia chamaana Zaidi ya hivyo vyote soma nami warumi 8:14{Kwa kuwa wote wanaoongozwa na Roho wa Mungu, hao ndio wana wa Mungu}. Kuwa MKRISTO kwamaana nyingine ni kuwa mwana wa MUNGU kuwa au kuwa chini ya miliki ya Mungu mwenyewe au kuonesha kuwa Mungu yupo katikati ya wanadam. Kuonesha mfano wa watu watakaoingia mbinguni na kustarehe kwa Mungu baba. Mtu hapokei Roho wa Mungu akabaki na matendo au tabia ya asili ya dhambi 1wakorintho 2:14 kwamaana mtu wa matendo ya asili bado amepotea.
        Yohana 14:16-18 {Nami nitamwomba Baba, naye atawapa Msaidizi mwingine, ili akae nanyi hata milele;ndiye Roho wa kweli; ambaye ulimwengu hauwezi kumpokea, kwa kuwa haumwoni wala haumtambui; bali ninyi mnamtambua, maana anakaa kwenu, naye atakuwa ndani yenu.Sitawaacha ninyi yatima; naja kwenu}. Roho siyo maamuzi ya dini Fulani tu bali ni agizo la kutobaki yatima kama Yesu mwenyewe alivyoagiza kwa wanafunzi wake. Ukimpata Roho mtakatifu unaanza kukamilishwa sasa katika ukristo wako na siyo dini ile ndio wanajazwa Roho mtakatifu au watu wa jinsi hii ile pekee ndio wanatakiwa kuwa na Roho mtakatifu. Kwamaaana wote waliompokea aliwapa uweza wa kuwa wana wa Mungu hapa haijasema na lazima uwe msabato au mlokole au mkatoliki au lutherani bali ni kule kuwa Mkristo na ukampokea Roho wa Mungu basi wewe umekuwa mwana wake kweli. Kwamaana Roho wa Mungu hakai sehem chafu bali hukaa sehem safi tu. Unaweza anza jiuliza napokea Roho wa Mungu kwasasa hapa nilipo, nakutoa wasiwasi kwamba kumpokea ni rahisi sana fanya yafuatayo:-
○ Jichunguze njia zako je ni kipi ambacho unafanya lakini hakipo sawa kabisaa kibiblia anza kukiacha hicho maana huwezi kujazwa ukiwa bado unatenda dhambi, kama dhehebu lako halizingatii ubatizo wa Roho basi hamia dhehebu jingine ambalo linasisitiza kuacha dhambi na kujazwa Roho mtakatifu. Tubu dhambi zako zote kwa kumaanishan jutia dhambi zako zote ulizotenda wakati bado unahangaika kwenye dhambi na usitamani kurudi huko tena. Elewa kitu kimoja unaweza kumdanganya BASA lakini huwezi kumdaganya Mungu kwamaana yeye huichunguza mioyo ya wote wamwendeao kwa kumtaka YEYE na kama bado unawaza maovu hawezi kukusikia hata kama ukeshe unaomba na kufunga juu. BADILISHA NJIA ZAKO
○ Uwe na njaa ya kujazwa Roho mtakatifu, tamani kuwa na Roho mtakatifu toka moyoni mwako omba kwa Mungu kila siku kuwa naye. Usiache kuomba hata baada ya kujazwa kwasababu kumpata siyo kinga ya YEYE kutoondoka kwako. Kwahiyo omba kila siku aje kwako uzidi kuzama zaidi ndani yake upate mafunuo kupitia Roho mtakatifu. TAMANI KUWA NAYE KILA SIKU
○ Mtumie kila siku ili adhihirike kwa wingi zaidi kwa maana kadri unavyomtumia ndivyo unavyozidi kuimarika kiroho. Kuzama kwako kutakupa kujua zaidi alama na tafsiri za kiroho na pia ndio utaanza kufurahia kumfuata KRISTO. 
         Baada ya kujazwa Roho mtakatifu furahia kuwa ndani yake wala usiruhusu akakuondolea uwepo wake ndani yako. Kuna watu walipokea na wao wakampoteza na kipimo cha Roho mtakatifu siyo kunena kwa lugha bali ni udhihirisho wake kwako kwa matunda yake tisa ambayo ni upendo, furaha, amani, uvumilivu, utu wema, fadhili, uaminifu, upole, kiasi; ukiona mtu anayo matunda ya Roho mtakatifu huyo ndio mwana kweli wa Mungu na amejazwa Roho wake kweli. Ukisoma hayo matunda hayajasema dini fulani bali yanamtaka mtu ambaye anataka kuwa mfuasi kweli wa KRISTO awe nayo. Kwamaana huyo msaidizi mwingine ndiye humtengeneza mtu kuwa hivyoo. Tunda la Roho mtakatifu inatakiwa lionekane kwa nje na siyo wewe kujitangaza kama BASA anadharau watu wengine haijalishi nitakuwa dhehebu gani wala kanisa la mchungaji nani na awe na upako kiasi gani?. Lakini bado nitakuwa sina Roho mtakatifu na siku ya mwisho makao yangu ni kwenye ziwa liwakalo moto. Basi ndugu yangu nakusihi kwa upole wake KRISTO YESU hebu tafuta ahadi yake ya Roho uwe na uzima wa milele ndani yako. Barikiwa sana

Mwandishi MICHAEL BASA 0765279698/ +255789799199

Jumatatu, 30 Oktoba 2017

NDANI YA DINI YANGU---3

AMEMKIRI KRISTO NA KUBATIZWA KWA MAJI MENGI {bofya kwa utangulizi}
Soma marko 16:15-17 Akawaambia, Enendeni ulimwenguni mwote, mkaihubiri Injili kwa kila kiumbe.Aaminiye na kubatizwa ataokoka; asiyeamini, atahukumiwa. Na pia warumi 10:9-10 {Kwa sababu, ukimkiri Yesu kwa kinywa chako ya kuwa ni Bwana, na kuamini moyoni mwako ya kuwa Mungu alimfufua katika wafu, utaokoka.Kwa maana kwa moyo mtu huamini hata kupata haki, na kwa kinywa hukiri hata kupata wokovu.}. kukiri kwa kinywa chako mwenyewe hii ndio hatua ya kwanza kabisa ya kuingia kwenye dini ya UKRISTO na siyo kwa kujikuta tu ndani ya ukristo. Kuna watu wamezaliwa babazao ni wachungaji au baba zao ni wazee wa kanisa Fulani wakaona kuwa kwasababu wamekulia kwenye mafundisho basi wao niwa KRISTO. Hapana mwajidanganya tu bure nafsi zenu inatakiwa umkiri KRISTO kwa kinywa chako mwenyewe tena mbele ya watu wengine kwamba mimi nitatembea na huyu KRISTO. Ukishamkiri unamkaribisha kuwa kiongozi wa Maisha yako kwa mda wote wa kuishi kwako. Kukiri kwa kinywa kwa maana ndogo ni kwamba unakubali kuwa kuanzia sasa mimi ni mtumwa wa YESU KRISTO katika mambo yote nakubali kuwa chini yake na nitajifunza magotini pake. Mungu wake ndio Mungu wangu Roho wake ndio Roho wangu na Maisha yake ndio Maisha yangu. Hapo ndipo unasema mimi ni mkristo. Baada ya hicho kitendo kinachofuata ni kubatizwa kwa maji mengi subiri niseme kidogo hapa kwamba kubatzwa siyo ishara bali ni ukamilisho kwa mtu yeyote aliyekubali kumfuata Yesu. Mathayo  3:13-15 soma vizuri hiyo mistari utaona kuwa kwenye msitari wa 15 Yesu mwenyewe anakiri kuwa ni haki na imetupasa wote kuitimiza. Nakuonya ndungu yangu sina ugomvi na mafundisho yenu wala dhehebu lako bali kama unataka kuwa MKRISTO hakika anza kutafuta kubatizwa kwa maji mengi na usikae tu kanisani bila kubatizwa omba kwa viongozi wako ubatizwe kwa maji mengi. Hakika usipobatizwa haki ya mbingu usipoitimiliza hauwezi kuiona mbingu hata kidogo kwa maana Yesu kaagiza kwenye mathayo 6:33{Bali utafuteni kwanza ufalme wake, na haki yake; na hayo yote mtazidishiwa.}. kumbuka ubatizo ni haki ya ufalme wa mbinguni na siyo kwa mujibu wa kanisa Fulani. Kwasbabu ni haki ya mbingu yule mwenye kazi ndio anatakiwa kuonesha mfano na siyo kwa mjibu wa dhehebu Fulani tu. Yohana 3:22-23{Baada ya hayo Yesu na wanafunzi wake walikwenda mpaka nchi ya Uyahudi; akashinda huko pamoja nao, akabatiza.Yohana naye alikuwa akibatiza huko Ainoni, karibu na Salimu, kwa sababu huko kulikuwa na maji tele; na watu wakamwendea, wakabatizwa.}. Tazama yohana aliyembatiza yesu alikuwa anabatiza kwenye maji tele. Sikia nikuambie kitu kimoja ndugu yangu katika KRISTO YESU ubatizo ulikuja kwa mkono wa Yohana ndio ambao biblia imeuagiza na sehem zote walipoagiza kubatiza au unapoona kubatizwa kwa maji ile siyo ishara tena bali ni agizo la ufalme wa mbingu. Ukitaka kujua kuwa ubatizo ulikuwa niwa aina moja muone towashi kwenye matendo 8:36-38. Hata pia wakati yesu anakuja kubatizwa yohana alikuwa anabatiza kwenye mto yordani. Basi kumbuka yesu anasisitiza kujifunza kutoka kwake kwenye mathayo 11:29-30 basi katika kujifunza kutoka kwa yesu  hakuna cha dhehebu langu limeagiza nini wala cha mchungaji wangu wala kiongozi wa dhehebu letu alikuwa na upako sana wala sijui alikuwa ni mmoja wa mitume au kaandika nyaraka zote maana hata yeye mwenyewe alifanya kubatiza kwa maji mengi pitia hata kwenye matendo ya mitume yote utaona watu wanabatizwa kwa maji tele kila sehem na hakuna sehem biblia imesema ni ishara tu. Basi ndugu achana na roho ya udini kabisaa jifunze kutoka kwa mwanzilishi wa Imani mwenyewe ambaye ni yesu KRISTO.

Mwandishi MICHAEL BASA 0765279698/+255789799199 
kama unaswali au ushauri au ombi nipigie au nitumie ujumbe mfupi{sms} kwa namba hizo utampata BASA mwenyewe na utapata vingi zaidi. Kwamaana Bwana ameniita kuwa mtumishi wako.  

Alhamisi, 26 Oktoba 2017

NDANI YA DINI YANGU ---2

 
   INAENDELEA..... {bofya hapa kusoma sehem iliyopita}
Kuna siku moja mtu mmoja aliniuliza Je BASA wewe kweli umeokoka? Nikamjibu HAPANA  unajua kwanini nilimjibu hivyo kwasababu sijafikia kwenye viwango vya wokovu ninavyovitaka na ambavyo biblia imeagiza mtu angalau kuvifikia tu kwa mawazo ya fikra yake. Kuwa mfuasi wa dini Fulani haishii kwenye jina wala kushiriki ibaada zao tu au kuhudum kwenye baadhi ya mikusanyiko ya dini hiyo. Kama hushiki sheria za dini yako hakika wewe siyo mfuasi wa hiyo dini bali ni mtu kama wasio wafuasi {KAFIRI}.
    Elewa kitu kimoja kwamba kuishi Maisha halisi ya dini yako kwa kufuata sheria za dini yako na miiko yake yote huko ndiko kuwa mwana dini wa hiyo dini yako. Ukiwa ni mwisilam hakikisha masharti ya uisilam unayafuata kwa kila kitu na kuitwa HAMIS siyo sifa ya wewe kuwa mwisilam kabisaa. Kuitwa LUKA haikufanyi wewe kuwa mfuasi wa KRISTO katika Maisha yako bali kuishi kwa mjibu wa maandiko ya kitabu chako au miongozo ya viongozi wa dini yako. Kwa mkristo Kuna madhara ya kuwa Mkrisito halafu humfuati kristo. Swali lako linaweza kuwa nitajijuaje kuwa namfuata Kristo na bado nipo kwenye njia sahihi ya kumfuta Kristo?. Kwamaana kuna watu ni wa Kristo kwa majina na madhehebu yao tu lakini kwa matendo Yesu hawajui watu hao. Kuna sifa za mtu anayemfuata Kristo kweli na siyo kwa maigizo kama watu wengi wanayofanya sasa kwamaana wameacha kazi ya msalaba na kujivika udini ambao Yesu hajaagiza hata kidogo. Hakuna Roho mtakatifu ambaye atashudia ndani yako akasema wewe niwa PENTEKOSTE au wewe niwa KATOLIKI au KKKT kama umefikia hapo wewe unajidanganya nafsi yako tu bure hakika humfuati Kristo bali umevaa roho ya udini. 
    Kama ukiweza kusema mimi niwa Kristo na matendo yako yakakiri kuwa wewe ni waKristo huyo ndio mtu ambaye ndani yake anadini ya UKRISTO. Kuna watu unawambia wewe hivyo unavyotenda ni kinyume na maadili ya dini. Anakujibu mimi si dini yako au mimi siyo dhehebu lako je hujui kuwa wizi ni dhambi je huji kuwa uongo ni dhambi?. Je ni dini gani iliyoagiza watu wasipendane au wasichukuliane katika makosa yao. Kuna watu wengine vinywa vyao vimejaa matusi na chuki wanatukana dini za wengine mara hivi mara vile. Lakini je dini yako inasemaje kuhusu kumfanya mwingine aawe dini moja nawe au kanisa moja dhehebu moja nawe?. Pia siyo kazi nyepesi kumfanya mtu mmoja atoke dini yake ya mda mrefu aje kwenye dini yako. Kuna sifa za MKRISTO aliye mfuasi wa KRISTO kweli nazo ni:-
  1. AMEMKIRI KRISTO NA KUBATIZWA KWA MAJI MENGI {bofya hapa kuisoma}
  2. AMEJAZWA ROHO MTAKATIFU{bofya hapa kuisoma}
  3. AMEJIKANA KATIKA KUMFUATA KRISTO
  4. ANASHIKA SHERIA ZOTE PAMOJA NA SABATO ZOTE ZA BWANA
  5. ANADUMU NA KWELI SIKU ZOTE
  6. MATENDO YAKE HUMTANGAZA KRISTO{bofya hapa kuisoma }
  7. ULIMI WAKE UMEJAA UZIMA
  8. ANAIJUA KWELI NA HIYO KWELI IMEMUWEKA HURU
  9. HUCHUKIA DHAMBI KWA MATENDO YAKE 
Tutaaanza kujadili sifa moja baada ya nyingine kadiri BWANA atakavyotupa uzima na mda pia.

MWANDISHI MICHAEL BASA 0765279698/+255789799199

Jumapili, 22 Oktoba 2017

NDANI YA DINI YANGU

Watu wengi tuna dini zetu au kwa maana nyingine tuna mfumo wetu wa Maisha wenye miiko na sheria pia. Dini yako inaweza kuwa tofauti na ya mwingine au zikawa sawa. Kumbuka miiko ndio inayoifanya dini yako iweke watu waufanano mmoja pamoja kwa lengo moja. Ndani ya miiko yako ndipo lengo kuu huandaliwa kwaajili ya watu wote walio kwenye dini yako kutoa mda wao kwa nguvu zote ili kulifikia. Sheria ndani ya dini yako zipo kukufanya ubaki kwenye njia sahihi wakati unaenda kutimiza lengo la ndani ya dini yako. Swali siyo usahihi wa dini swali ni je bado upo kwenye njia sahihi ya kulifikia lengo la dini yako??. 
            Nataka nielezee lakini nitatumia Zaidi maandiko ya kwenye biblia maana ndiko niliko na maarifa mengi na mifano mingi. Ukisoma yakobo 1:26 Mtu akidhani ya kuwa anayo dini, wala hauzuii ulimi wake kwa hatamu, hali akijidanganya moyo wake, dini yake mtu huyo haifai. Hapa tatizo siyo mtu kuwa na dini tatizo je hiyo dini yake ndio misingi ya Maisha yake?. Je ulimi wake unaua au unaponya? Soma mithali 21:23 na mithali26:28. Utagundua kuwa kama mtu ana dini yake anatakiwa ajifunze kuwa wa haki kwenye hiyo misingi na sheria za dini yake. Kuna watu wamekuwa wakijidanganya kuwa mimi ni dini Fulani wala siyo dini ile lakini matendo yake hayatupi picha ya ile dini anayoisema. Mtu anaweza kusema mimi ni mwisilam wakati hata sura moja hajui kusoma kwa picha sasa unajiuliza huyu dini yake kwa mawazo yake ni uislam lakini kwa matendo anakataa. Mwingine anaenda mbali Zaidi kwa kusema sisi tumezaliwa kwenye uislam lakini kuswali ni ijumaa mpaka ijumaa. Je ndivyo dini yako inavyoagiza?. 
            Mwingine ni mkristo kwamaana nyingine ni mfuasi wa KRISTO swali je wewe umejifunza kwa kristo kweli mbona haujabeba msalaba wako mwenyewe?. Kama wewe una dini kweli mbona hutuambii mwisho au Taraji ya dini yako kwa matendo tujue u katika safari kweli ya kufika kwenye Taraji ya dini yako. Mtu na akasema mimi niwa Paulo na mwingine mimi niwa Petro na wote wakabaki ni wanadam tu. Je wajua unayemuabudu anataka uweje? Soma sheria zake na usizipindishe hata moja ndipo utajua kuwa mungu wa dini yako anataka nini kwako. Leo hii mtu akisimama kuonya kuna watu wanasema sisi na wewe ni dini moja lakini madhehebu tofauti. Sikiliza nikuambie kila dini iko kwenye Imani ya ibada na ya uwepo wa Mungu. Sasa je kwa mwenendo wa ulimi na matendo yako vinamwabudu bado au umekuwa unaidanganya nafsi yako kila mara?. Sikia nikuambie ndugu kusema wewe ni dini fulani halafu ukaacha baadhi ya sharia na ukaamua kufuata baadhi tu kwasababu wewe umeona ni njema machoni pako mwenyewe. 
            Ama zinakupa uhuru wakutii mambo yaliyo kinyume na hicho unachokiamini. Nasema hivi kwasababu kuna watu wako dhehebu Fulani kwasababu tu hawapendi kuambiwa uzinzi ni dhambi au mavazi yao niya kikahaba. Kwa wakristo Hakuna wokovu pasi na kumpenda YESU na kama ukimpenda Yesu inatakiwa ujikane na ushike sheria zake na uzifuate. Kwahiyo kuwa mkirsto siyo kazi ya lelemama inahitaji kujitoa kwa gharama zote kumfuata yesu. Kuna siku moja mtu mmoja aliniuliza Je BASA wewe kweli umeokoka? Nikamjibu HAPANA  unajua kwanini nilimjibu hivyo???

................................inaendelea bofya hapa kusoma...........


Mwandishi MICHAEL BASA  0765279698

Jumapili, 1 Oktoba 2017

HUYU MUNGU NI BABA

Bwana wewe ni nguvu na ngome kwangu ahadi zako ni za milele kwangu umeniinua juu ya mataifa nawe umekuwa mji wa nguvu moyoni mwangu mataifa sikieni nanyi mkaweke ushuhuda mioyoni mwenu “Heri walio kamili njia zao, Waendao katika sheria ya Bwana”. Tena ni “Heri wazitiio shuhuda zake, Wamtafutao kwa moyo wote.Naam, hawakutenda ubatili, Wamekwenda katika njia zake”. Bwana Mungu wangu anawapenda watu hao nao kamwe hawatakuwa makapi mbele za adui zao maana Bwana yeye atawashindia vita na wao milele watakuwa washindi. Je wachamungu wametaabika mioyoni mwao na nyongeza zimeteka ufahamu wao sikieni leo niwakumbushe fadhili za Bwana zilizo za milele tena aliahidi hatakuacha enyi mtangao je hamkusoma imeandikwa “Msisumbuke, basi, mkisema, Tule nini? Au Tunywe nini? Au Tuvae nini?. Kwa maana hayo yote Mataifa huyatafuta; kwa sababu Baba yenu wa mbinguni anajua ya kuwa mnahitaji hayo yote. Bali utafuteni kwanza ufalme wake, na haki yake; na hayo yote mtazidishiwa.”. Je hamkuamini kwa neno la injili nalo ni hili yeye aketiye mahali palipoinuka ametuamru kuyashika mausia yake Ili sisi tuyatii sana. Neno langu naomba kibali mbele zako Bwana nalo ni hili “Ningependa njia zangu ziwe thabiti, Nizitii amri zako.Ndipo mimi sitaaibika, Nikiyaangalia maagizo yako yote.Nitakushukuru kwa unyofu wa moyo, Nikiisha kujifunza hukumu za haki yako”. Kwa maana Hakuna mtu aliyeacha nyumba, au ndugu waume, au ndugu wake, au mama, au baba, au watoto, au mashamba, kwa ajili ya Injili, akapata hasara bali atapewa mara mia sasa wakati huu, nyumba, na ndugu waume, na ndugu wake, na mama, na watoto, na mashamba, pamoja na udhia; na katika ulimwengu ujao uzima wa milele.

Jumatatu, 28 Agosti 2017

BASA VISION


 Moja ya mijadala au maswali magum kwa kipindi hiki au kwa wakristo wote ni kwanini shetani anawasumbua?. Nami katika njozi ya usiku wa kuamkia tarehe 28 Aug 2017 Bwana alinionesha. Kwanza siku mbili kabla moyo wangu ulikuwa na kiu ya kitu ambacho sikijui nikaona labda tamaa ya kumtumikia Bwana imekuwa kubwa kuliko jinsi ambavyo naweza kuhimili. Nikaendelea na mienendo yangu ya kawaida ya kila siku huku nikijichunga nisije mtenda Bwana dhambi. Jumapili ya tarehe 27/8/2017 nilipokuwa kanisani nikawa kama amani inaisha kwa kuwa nilihitaji kujua kitu ambacho sijui ni nin?{yaani unaahisi unahitaji kuwa na maarifa fulani ambayo huna lakini mtu akikuuliza maarifa gani huwezi kusema maana hata akili yako haijui moyo unataka nini?}. Amani ikaendelea kupungua mpaka nikawa natamani kuondoka kanisani kuacha ibada nikawa mtu wa mawazo. Nikaamua kuingia kwenye maombi nikanena kwa lugha sikujua hata naomba nini?.Roho alininyima maana yake baada ya mda kule kukosa amani kukapungua kidogo nikaendelea na ibada mpaka mwisho.
   Usiku ndipo Bwana akanionesha katika maono nilikuwa natembea sehem ambayo kuna kisima na bwawa upande mwingine namimi nilikuwa napita katikati yake huku nikiwaza jinsi ya kumtumikia Bwana kwa uaminifu huko niendako?. Kwamaana Bwana alikuwa amenituma lakini sehem siijui, nilipokuwa katika mawazo yale mara mbingu zikafunguka nikamuona Roho mtakatifu akishuka kwa mfano wa hua.  Yesu akasema na mimi akaniambia kuna kanisa hapa nataka ukafundishe ndipo uendelee na safari. Nikakubali nikafunguliwa macho nikaona kanisa ndani ya Yesu mwenyewe nililokuwa natakiwa kwenda kulifundisha nalo lilikuwa na watu wengi sana. 
   Walikuwa wakisifu mbele za Bwana hakika walipendeza sana. Nilipokubali ndani ya moyo wangu mda ule ule Roho alinichukua nikajiona naiacha ardhi na kuingia ndani ya lile kanisa madhabahuni. Waumini wakakaa kimya kila mtu mahali pake ndipo nikafungua biblia nifundishe moja ya masomo ninayoyafaham. Nilipoanza tu kufundisha Roho akaniambia siyo somo hilo tazama huku uwaelezee yote utakayoyaona nami nitakuwa nawewe. Nikaona tazama binti mmoja mlokole aliyekuwa na njaa ya kumtumkia sana Mungu na Mungu akambariki kwa KARAMA ya ualim na huduma ya uimbaji watu wote wakampenda sana kwa jinsi alivyojitoa kwa Bwana. Shetani alijaribu maranyingi sana kumtoa kwa Yesu kwa kumzuia kuimba akashindwa, kwa kumtenga na marafiki, kumkosanisha kanisani hata hakujali walipomkataa kanisani yeye alihudumia wa nje ya kanisa. Watu wakampenda sana kwa nyimbo zake na mafundisho yake mazuri hata Yesu alimpenda pia. Kikao kikafanyika kuzimu kuhusu ufalme wao kutetereka sana kupitia kwa huyu binti wa Yesu. Shetani akaja na mpango mpya ambao angetumia miaka miwili kufikia kumuangusha kabisa na kumtoa nje ya Yesu. Nao mpango ulikuwa katika hatua zifuatazo:-

1. Kuanza kucheza na mawazo yake ya kila siku kuhakikisha  mawazo yake yanaanza kuwa na chembe za uovu kwa mbali kwa vitu vifuatavyo:
  • MWILI WAKE MWENYEWE:- atakapofikria kuhusu nguo za kuvaa kwaajili ya huduma cha kwanza kabisaa ni kumpa wazo la kwamba hizo nguo ni za zamani pia hazimpendezi kwasasa na atakapojiuliza avae nguo gani?. Picha ya kwanza kumletea ni zile za watu waliopotea na bado wanafanya huduma au bado wako kanisani.
  • MARAFIKI:-kuwasogeza marafiki wengi waliopotea kwake wakanisani na wasio wakanisani karibu yake ili pindi akiwaza uovu wao ndio wamshauri uovu ule kwamba hauna madhara kwake kwa maana hata wao bado wanatumiwa na Roho au wanasfari ya kwenda mbinguni
  • MAVAZI:- kuanza kumpa mawazo ya kuvaa nusu uchi na kwa nia ya kupendeza maana huduma siyo ma nguo marefu au mapana sana lakini ni kupendeza kwanza kisha huduma itavutia watu wengi.
  • AKILI YAKE:- ipunguze kuwaza kuhusu Mungu sana au ikiwaza isiwe katika uzito ule wa mwanzo kwa kumpa kitu mbadala cha kuwaza kila anapotaka kufikria kuhusu Mungu.
2. Baada ya hivyo kufanikiwa kinachofuta ni kumpa roho ya kukosa mda kwa maana atapunguza maombi na tamaa ya kuhudumia kwa bidii au kupanda viwango iondoke. 

3. Wazo la mume limjie kwa kasi ya ajabu ambayo mwili wake na akili zake zishindwe kuhimili.. Ambapo iwe rahisi kumpa mtu ambaye atashindwa kufanya jukum la Bwana au kufikia viwango pia iwe rahisi kuingilia ndoa na kila kitu cha ndani ya ndoa. 

4. Kumuacha ahudum huku akiona kila kitu kipo sawa hata asipopotea yeye lakini kazi za ufalme wa giza zitaendelea kuwepo na kukua na kushamiri sana duniani kote.

Baada ya kile kikao nikaona kundi kubwa likimvamia la pepo wachafu kila pepo alitoa wazo ambalo anahisi linaweza kufanikiwa. Baada ya mda mrefu sana hatimae yule binti akaweka mguu mmoja nje ya msitari wa wokovu na nguvu za giza hata bega lake kushoto lilikuwa na alama ya uovu. Mwili wake uliosalia ulikuwa ndani ya Yesu ukipokea baraka zote na kila kitu lakini kuenea kwa ufalme wa Mungu kupitia yeye ilikuwa tayari imekuwa ngumu.

 MICHAEL BASA +255765 279 698 

Alhamisi, 24 Agosti 2017

NUHU WA KIZAZI HIKI

   Ukisoma kitabu cha mwanzo 5:29 mpaka mwanzo 10:32 utakuta habari za mtu mmoja anaitwa NUHU. Huyu mwanaume aliishi katika kizazi kilichokuwa katika hali ya uovu wakupindukia. Watu walilala na wanyama, walikula nyama za watu, walikuwa ni watu wakaidi wasiotii, wasiosamehe,wauaji. Watu walipoona uovu kuwa ni kitu cha kawaida Nuhu alipata kibali machoni pa Bwana. Kama wewe unampenda Mungu kweli utajiuliza ilikuwaje Mungu akamhifadhi katika uovu kiasi kile?. Je unamkumbuka Lutu aliyepata amani machoni pa Bwana pindi moto uliposhuka na kuangamiza sodoma na gomora?. Uovu ulipozoeleka machoni pa wanadam na kuonekana kitu cha kawaida yeye moyo wake ulimwelekea Bwana. 
   Walipoonekana hawana akili na kuitwa wajinga au wasio enenda na wakati kwa wakati huo lakini mioyoni mwao cha kwanza kilikuwa ni kumpendeza Bwana. Unaweza usinielewe haraka kiasi hiki twende pamoja kwenye kitabu cha mathayo 24:36-39 {Walakini habari ya siku ile na saa ile hakuna aijuaye, hata malaika walio mbinguni, wala Mwana, ila Baba peke yake.Kwa maana kama vile ilivyokuwa siku za Nuhu, ndivyo kutakavyokuwa kuja kwake Mwana wa Adamu. Kwa kuwa kama vile siku zile zilizokuwa kabla ya Gharika watu walivyokuwa wakila, na kunywa, wakioa na kuolewa, hata siku ile aliyoingia Nuhu katika safina, wasitambue, hata Gharika ikaja, ikawachukua wote, ndivyo kutakavyokuwa kuja kwake Mwana wa Adamu.}. Hata kuja kwake mwana wa adam kwa mara ya pili maisha yatakuwa yanaendelea tu kama kawaida. Kanisa litaendelea kama kawaida, manbii wauongo nao watakuwepo kama kawaida, wachagua wokovu nao watakuwepo, wang'ang'ania kanisa kuliko Yesu nao wataongezeka maana ndiko ukristo unakoelekea. Yesu hajaleta ulokole, usabato, uroma n.k. Lakini alileta uzima wa milele{Yohana 17:3 Na uzima wa milele ndio huu, Wakujue wewe, Mungu wa pekee wa kweli, na Yesu Kristo uliyemtuma.}. Tazama leo kuna wokovu wa aina mbili mmoja wa zamani na mwingine wakisasa. Wengine wameanza kuchagua maandiko ya kwenye wokovu wakisasa. 
   Ukimkemea anajenga chuki nawewe hata anaweza kutengeneza somo kwaajili yako tu je huyo Roho anayewapa amani ni kweli ndiyo huyu ninayemtumikia mimi?. Kwamaana kuna wengine mioyo yao ndio waalim wao hata wamemzimisha Roho mtakatifu kasome tena Yeremia 17:9, Yakobo 1:22b na 1Wathesalonike 5:19. Kuna kanisa moja Mungu aliniweka niabudu hapo nikakuta ibada zao ni kusemana baada ya kukosekana nikaazimu moyoni mwangu kulihama ili nikatafute kanisa jingine. Bwana akaniambia hapo ndipo nilipokupangia uabudu. Ikawa ni mtihani kwangu katika wokovu wakuanza kuwatoa watu huko kwenye mafundisho yakusemana na kuja kwenye mafundisho yakutiana moyo na kujengana katika mwili wa Kristo pia msamaha mioyoni mwao. 
   Nilikuwa naongea na mmoja mmoja kisha nikaongea na kundi zima kama Bwana alivyonipa neema na kibali pia. Lakini pia kuna mtu Roho alinishuhudia nikamwambie kuhusu mavazi yake ayabadilishe ili roho{nguvu} ya uasherati isimsumbue tena au imuache. Alikuwa ameokoka akaniambia kuwa hicho ninachomwambia ni wokovu wa zamani sana. Lakini baada ya mazungumzo marefu na kujitahidi kujibu maswali yake akaniambia baadaye atafikria kuhusu kubadili mavazi yake. Lakini haijalishi kuwa kuna wokovu wa zamani na wakisasa lakini sikia nikuambie kuwa {HAIJALISHI DHAMBI WANAFANYA WENGI KIASI GANI?, AU IMEZOELEKA KIASI GANI?, AU WANAFANYA WATU UNAOWAAMINI KIASI GANI LAKINI DHAMBI ITABAKI DHAMBI  SIKU ZOTE NA ITAKUFANYA USIENDE MBINGUNI?}. Mungu wetu ni mtakatifu na mtakatifu pekee ndio atamuona yeye na ndie atakayepata ruhusa ya kuingia kwenye makazi yake. 
itaendelea........
MICHAEL BASA 0765279698

Ijumaa, 18 Agosti 2017

JE NI MIMI au NI BWANA??.

Kuna kipindi mkanganyiko hutokea sana pindi tu linapokuja suala la mipaka ya Bwana kutenda na wewe mwenyewe kutenda. Kuna mtu mmoja aliwahi kusema nanukuu " usiufiche uzembe au uvivu wako kwenye maombi ukahisi utafanikiwa bali fanya kazi kwa bidii Bwana atakutana nawewe huko huko kazini". Pia kuna mwingine aliwahi kusema kwa kiingereza "hard work beats talent when talent doesn't work hard". Lakini biblia inaseema "Msijisumbue kwa neno lo lote; bali katika kila neno kwa kusali na kuomba, pamoja na kushukuru, haja zenu na zijulikane na Mungu." katika wafilipi 4:6. Swali la kujiuliza je kuna mipaka ipi ya kimwili na kiMungu katika utendaji wangu yaani ya kimwili na Roho katika uenendaji wangu wa kila siku?. Kabla ya kujibu hili swali tuangalie kwanza andiko moja nalo ni kutoka wagalatia 5:25 "Tukiishi kwa Roho, na tuenende kwa Roho.". Kuna vitu vifuatavyo katika kuishi katika mwili huku ukifanya ya rohoni navyo ni:-

  1. Katika mtazamo wa kwenda mbinguni au kuingia Yerusalem mpya inatakiwa uwe kwanza akilini mwako kila mahali unapotembea au kukaa au hata kulala. Kwamaana mshitaki yuko kila mda anaandaa hati yako ya mashitaka nawewe uwe katika hali ya kuvunja shitaka shitaka lolote litakaloletwa{1ptero 5:8}. Hapo cha kwanza ni kujazwa ROHO mtakatifu na kumsikiliza yeye tu kama mwalim, msahuri, mwelekezi wako, mtoa dira wako, mpangaji wa mambo yako yote, msemaji wa mwisho juu yako na rafiki bora kwako.warumi 8:9 pia yoha 14:26.
  2. Jizoeze kuwa mkazi wa mbinguni kwa kujifunza mambo ya ufalme na kujizoeza katika mambo ya ufalme kila mara.  1Petero 2:11 "Wapenzi, nawasihi kama wapitaji na wasafiri, ziepukeni tamaa za mwili zipiganazo na roho.". Wewe ni msafiri tu usitake kuupata ulimwengu kwanza bali tunza kwanza taji ufunuo 3:11, marko 8:36. Safari ya mbinguni iwe ni ya uhakika maishani mwako mwote.
  3. Acha kuishi kwa mazoea kila siku Mungu anataka kusema na wewe kwa jinsi nyingine na tofauti sana kutoka ile ya jana. Usimzoee Mungu kwa maana ukiona umemzoea sana Mungu jua tu umeshaanguka. Kwamaana mda si mrefu ulishapingana na Roho mtakatifu. Kuna watu wamekariri jinsi moja tu ya kusema na Mungu jua kwamba safari yako haina uhakika sana kwa maana hata shetani anaweza kutumia na akakupoteza na Mungu akatumia njia nyingine ukashindwa kumuelewa kuwa ni YEYE anayesema nawewe. Penda kuona Mungu akijifunua kivingine kila siku katika maisha yako ya kila siku.
  4. Penda sana kujihoji uhusiano wako wa siku kati yako na ROHO kwa maana unaweza kutana na ishu ngumu au hali ambayo akili yako ikashindwa kutafasiri kwa jinsi ambavyo Mungu anapenda au anataka uelewe. Ukijihoji atakuambia na kukuelekeza kisha unatubu mambo yanakuwa sawia kabisaa.
Baada ya kuanza kutenda hivyo vinne utakuja kugundua kwamba roho yako inaanza kuwa na nguvu sana kuliko mwili wako. Hapo ndipo unakuwa na uwezo wa kuongea na Mungu bila wasiwasi na kuishi kwa imani unakuwa mtu wa mfano  kwa jamii yote katika imani. Ukiwa mtu huyo hauhitaji unabii wala nabii akuambie Mungu anasema nini juu yako kwamaana kabla hujaja hapo ulipo tayari kashasema nawewe. Kama ndivyo hivyoo basi mtendaji ni wewe na Muongozaji{mwamuzi} ni Bwana na nyie wawili mnakuwa umoja kwamaana mnaishi ndani ya jumba moja ambalo ni mwili huo ulio nao na nyie  mmenakuwa mmoja. Na hapo  ndipo kila ufanyalo litafanikiwa kwamaana Mungu anakuwa anataka akutumie sana. Kwahiyo hawezi kuruhusu upoteze mda kwenye mambo yasiyokuwa ya ufalme wake. Kila utakapofanya swali kubwa litakuwa JE NI MIMI au NI BWANA?. Jibu ni Bwana ndani yako kwa nje unaonekana wewe kwa ndani anaonekana Bwana. Ndipo hata mtu akikushukuru haujitukuzi kwamaana ile shukrani ikiingia ndani inamkuta Bwana kila sehem na Yeye ndiye anayeipokea. 
   Mungu akubariki sana mtumishi  kwa kusoma mpaka mwisho tumia namba yangu hapo chini kunipa mrejesho na pia kutoa maoni yako. Pia nataka nisikie kutoka kwako na kwa facebook page usiache ku LIKE 

By MICHAEL BASA +255 765 279 698

Jumanne, 15 Agosti 2017

NANI ASIMAME AKEMEE ???.


 Nami nimeuona uovu juu ya madhabahu maana dhambi ya kipindi kanisa linakuja kwasasa haikemewi tena. Nani kasema kuwa Yesu kabadilika au sheria zimetanguka, kama mwanzo tulikemea kunyoa DENGE na tukaamini kuwa ni uhuni na pia haufai kanisani leo kimetokea nini isiwe dhambi tena?. Soma walawi 19:27 {You shall not round the corners of the hair of your heads nor trim the corners of your beard [as some idolaters do] kutoka kwenye AMP}.  Hiyo style ya kunyoa ya denge ilikuwa inatumiwa na waabudu sanam na pia tatuu inatumiwa na waabudu sanam kama alama ya kujisogeza kwnye ibada.Mfano kwenye makanisa ya sasa tunatumia nyimbo za kuabudu ili kujiweka tayari mbele za Mungu. Sasa wewe unayenyoa au unayetamani ujichore tatuu je unajua kwamba mawazo yako yameanza kukutoa kwenye kumwabudu au kumtumikia Mungu wa kweli nakuanza kuielekea miungu ambayo haitakupeleka mbinguni bali kuzimu. 
     Tazama tena kwa mabinti zetu nguo walizovaa makahaba miaka 1970 leo ndio zinavaliwa na waimbaji wa makanisa yetu . Mtoto wa mchungaji akifanya dhambi ni nani wa kukemea huo uasi. Sikia mbinguni hatuingii kwa vyeo vyetu ndani ya kanisa wala huduma zetu ndani ya kanisa hakika nakuambia BASA MINISTRY haitanipeleka mbinguni bali UTAKATIFU ndio utanipa kibali cha kukutana na Bwana wangu. Waumini wameanza kuchagua mafundisho ya kushika wakati biblia ni moja wewe usiye na akili ni nani aliye kuroga wainjilisti wamesema wazi na kukemea wazi mbele zako nawewe ukainua kimdomo chako kumsema vibaya pole sana. Kwamaana wafanya vita na Bwana mwenyewe nawe hutaokoka kwa mawazo yako maovu wala kujihesabia haki kwako. 
   Ni nani kati ya mabinti zetu aliyetaka kununua kimini akaammua kufunga na kuomba kwaajili ya kupata maono na ruhusa ya Roho mtakatifu na baada ya kupata jibu akashirikisha mwingine zaidi kwenye kuomba maono kuwa Roho analionaje hilo vazi?. Vijana wa kanisa nao hawako nyuma kwa msemo wa modo zao nguo inabana kila sehem. Mwanzo wanawake walivaa kuamsha hisia{lust} za wanaume je kijana wa kiume unaamsha hisia za nani?. Je unajua madhara ya kutumika kwenye kitu ambacho mwanzilishi{author} wake siyo Mungu?. 
    Nakuambia acha kuiga iga vitu ovyo tamani kwanza kujazwa Roho mtakatifu kisha ipeleke injili kwa jinsi ulivyoitwa tamaa za mwili huwezi kuzikamilisha milele mpenzi wangu nikupendaye na pia shetani ni mdanganyifu sana wewe jisifu kwa Amani yenye mapengo mapengo na roho yako mwenyewe imechoka na haiwezi kumuona MUNGU. 

By MICHAEL BASA 0765 279 698

Jumapili, 13 Agosti 2017

UNAWAZA NINI??

unawaza nini
basa jpg
    Kabla ya kitu chochote kudhihirika kwenye ulimwengu wa mwili kiutendaji huanza kama wazo ndani ya moyo au akili ya mtu mwenyewe. Kwa wazo lako  unaweza kuanzisha vita ya kiroho au kujisogeza karibu zaidi na MUNGU wako. Mwanzo 4:7 inasema ........dhambi iko, inakuotea mlangoni, nayo inakutamani wewe, walakini yapasa uishinde. Angalia kwenye hayo maandishi mekundu utajua kitu tofauti kidogo. Dhambi iko inakuotea mlangoni???? jiulize tena kivipi dhambi ikuvizie mlangoni kwako. Lakini pia inakutamani!!!! kivipi haya yanawezekana kutoka kinywani mwa MUNGU mwenyewe. Kama wewe ni mchunguzaji wa maandiko huenda na wewe ilikutatiza sana au kiasi chake.
       Twende zaburi 36:1{Kuasi kwake yule mwovu hunena moyoni mwake, Hakuna hofu ya Mungu mbele ya macho yake.}au Ezekieli 38:10. Kumbe kabla ya mtu kutenda uovu machoni  pake huja na wazo moyoni mwake likipita ndilo hulitenda bila kuwa na hofu ya Mungu kabisaa. Basi kumbe dhambi haiwi dhambi mpaka ipate kibali moyoni mwako. Usipoipa kibali kamwe wewe hauwezi kutenda dhambi kabisaa katika maisha yako yote. Jikune kichwa kidogo kisha jiulize asilimia kubwa ya mawazo unayowaza je niya ufalme upi??. 
      Soma tena zaburi 66:18 {Kama ningaliwaza maovu moyoni mwangu, Bwana asingesikia}. Swali la kujiuliza je ni Bwana hawasikii watu gani?    Yeremia11:11-17 hapa ndipo utagundua kuwa walioasi au kuiacha sharia ya Mungu ndio ambao Bwana hawasikii. Daudi anaposema Bwana asingesikia basi kwa namna moja au nyingine anakukumbusha kuwa dhambi huanzia moyoni mwa mtu. Huhesabiwa kuwa ni dhambi baada ya kupata kibali moyoni mwako mwenyewe ndio maana katika Yakobo 4:1. Imeelezea kabisa kuw vita tunavyopigana mara nyingi kwa kushindana na miili au viungo vyetu zimetokana na mawazo yetu yasiyo na kibali machoni pa Bwana. 
          Ndio maana YESU akatuonya mapema kwa kutuelekeza kuyatafakri yaliyo juu yapitayo faham zetu. Leo pia nakukumbusha usikomee kuwaza tu mazingira yako hayo yatakukatisha tamaa MUNGU haangalii mazingira wala jamii ya watu waliokuzunguka. Kwamaana hata hao hawajui Mungu anakuwazia nini? bali watasema yajazayo mioyo yao kama  mawazo yao ni maovu . Basi hata mioyo yao huwa imejaa maneno na shuhuda za kutomtukuza Bwana wala kuonesha ukuu wake hata zikikiri kuwa ni muweza wa yote lakini bado huwategemea wanadam maana mioyo yao huwa imeielekea zaidi dunia na siyo ufalme wa Mungu. Yeremia29:11 na akaambiwa asijisumbue wanasema nini juu yake kwa maana hawajui Bwana aliwazalo wala alipangalo juu yako pia  MIKA4:12. 

By Michael Basa 0765 279 698

Alhamisi, 3 Agosti 2017

KANISA LILILOPOTEA--2

      Kuna jinsi mbili za ambazo shetani hututmia kumtawala mtu mosi ni njia ya moja kwa moja. Katika hii njia mtu anakuwa anajuwa kuwa mimi ni washetani na hata sasa nikifa mimi nitaenda kuzimu lakini kwa sababu ya mambo fulani fulani siwezi kutoka huku mfano waabudu sanamu, wachawi n.k. Pili ni njia isiyo ya moja kwa moja hili kundi limegawanyika sehem mbili ya kwanza ni ile ambayo haiombi kabisa kwa MUNGU. na ya pili ni ile ambayo inaomba kwa MUNGU. Makundi yote unakuta yanamilikiwa na shetani pasipo na wao wahusika kujua. Watu katika kundi hili unaweza kuta mpaka ni viongozi wa kanisa lakini bado matendo ya mwili ni dhahiri kwao. Je hujawahi kukuta shehe kalawiti mtoto?.
         Je RC nayo amabayo watu wanaipigia kelele rome kila siku watoto wanaingiliwa kinyume na maumbile. Monoroviani ambao nao katika nchi za UK wameruhusu mashoga kufunga ndoa tena wanatumia biblia??. Je unafuu uko wapi PENTEKOSTE nako ambako ndoa zinafungwa huku binti tayari anamimba??. EAGT na TAG ambako mzee wa kanisa anakimada ndani ya kanisa lile lile?. Wamama wa makanisani nao wamejaa maseng'enyo unaachaje kusema hili ni kundi ambalo baya zaidi kuliko lile la kwanza. kwamaana hili ni kundi linaloodhifisha na kupoteza kanisa kuliko la wachawi na waabudu sanamu wala wajenzi huru.
          Kwamaana watu wengi wanashindwa kumfuata YESU katika ROHO na kweli kwasababu yenu ninyi viongozi na wachungaji vipofu. Injili zenu zimebaki kukemea wenzenu wa mafundisho fulani au waaina fulani tu. Mfano mzuri ni huu msitari waefeso 2:20{Mmejengwa juu ya msingi wa mitume na manabii, naye Kristo Yesu mwenyewe ni jiwe kuu la pembeni.}. Msingi wa kanisa lako umejengwa juu ya akina nani kama mafundisho yako wewe ni juu ya manabii tu na siyo kufundisha jinsi ya  kutofautisha nabii wa uongo na nabii wa ukweli?.
          Kuna mchungaji unamkuta mafundisho yake yote yanaongelea mafundhisha ya manabii wa uongo tu basi hebu anza kuliangalia hili andiko pia 1yohana 4:1{Wapenzi, msiiamini kila roho, bali zijaribuni hizo roho, kwamba zimetokana na Mungu; kwa sababu manabii wa uongo wengi wametokea duniani.}. Hebu anza kufundisha kanisa lako kutembea katika Roho uone kama atapotea hata mmoja kweli kwa maana umewafanya kila waumin wako kila siku kuwa ni watoto wadogo wakati kwenye kanisa lako ambalo halizidi hata huduma tatu. Na umekaa kimya tu na kuridhika kabisa je huduma zingine za ndani ya kanisa umeziweka wapi kama siyo kwamba umezikataa mwenyewe tu??.
        Naomba kwako leo ewe Mchungaji au Padri hebu jaribu kufufua karama zote na wafanye watu watembee katika Roho ndipo utaona ni kwanini watu wanahitaji kweli tu uongo utajitenga wenyewe. Pia naomba nieleweke kuwa sijakataa kuwa manabii wa uongo hawapo bali na makristo wa uongo wapo tena wengi kuliko hata manabii. Je kuna nyimbo ngapi za injili hazina utukufu katika uchezaji wake au uimbaji wake na hazimjengi mtu katika imani?. Basi kasome tena utakutwa imeandikwa katika 2wakorintho 1:21 {kuna mtia mafuta mmoja ambaye ni MUNGU} kisha kasome 1Yohana2:20-28 utajua ni kwanini natamani ujae ROHO Mtakatifu hata hutasumbuka na kuchukia mafundisho wala wafundishao bali utajua kusudi lako ni nini juu yao. Pia kuna roho ya ibilisi imekaribia kuanza kuingia makanisani na itakuwa na nguvu sana nayo ni KUJICHORA{TATTOO} nakuonya mapema anza kuikemea sasa na kufundisha kuwa kujichora ni dhambi na mtu akijichora atengwe kabisaa bila kujali cheo chake wala karama yake usije, nimekuonya mapema wewe na kundi lako.
     by MICHAEL BASA 0765 279 698
Inaendeshwa na Blogger.