Jumatatu, 21 Desemba 2015

KITOKEACHO MTU AKIZINI



Ni vitu gani humpata mtu anapozini? 
Kwanini hadi Mungu atofautishe kati ya uzinzi na dhambi nyingine? Hadi Mungu anasema “Kila dhambi aitendayo mwanadamu ni nje ya mwili wake; ila yeye afanyaye zinaa hutenda dhambi juu ya mwili wake mwenyewe” (1kor 6:18).  

Kunanini hasa?

Kwanza; unapoenda kuzini unaenda kupokea mapepo yote yaliyo kwa huyo mtu unaezini naye. Na kwakuwa tendo hilo ni agano la Damu; mwili wako na wa huyo unaezini naye inaunganishwa na kuwa mwili mmoja. Hivyo mapepo yanakuwa na haki kukaa kwa wote wawili.
Kwahiyo kama mtu ana pepo la ukahaba, nawe ukizini nae unajikuta nawewe unafanya ukahaba hata kama huendi sehemu za kujiuza. Ndio hao watu walio wengi sana wanaobadilisha mahusiano kila baada siku au miezi kadhaa. Ndio maana imeandikwa “Au hamjui ya kuwa yeye aliyeungwa na kahaba ni mwili mmoja naye?” (1kor 6:16). Kama huyo unaezini nae anayo matatizo kama kutokuoa/kutokuolewa, kutofanikiwa, na nuksi; nawe hayo yote unayapokea kama yalivyo
Watu wengi wanapozini siku ya kwanza kabisa, huwa wanajichukia sana na kukasirika na kujutia sana. Na moiyoni mwao hujiona wamepoteza kitu cha thamani sana. Hadi unajiapiza moyoni unasema “sitarudia tena kufanya jambo hili”. Lakini baada ya siku au mwezi mmoja tu hujikuta unatamani sana kufanya uzinzi… na tena unajikuta sasa huwezi kabisa kujizuia.. hii ni kwasababu ya hayo mapepo uliyoyapata siku ile ya kwanza ulipozini… ndio hao watu ambao wakijua kama rafiki yao hajawahi kufanya mapenzi humuuliza “unaishije”?... Hii ni kutokana na wao sasa kumilikiwa na nguvu za mapepo ndani yao kiasi kwamba wao haiwezekani kuishi bila kuzini.
Unapoenda kuzini ni kwamba unajaribu kuvunja agano la damu ya Yesu kwa kufanya agano lingine la Damu na Shetani kwa njia ya Uzinzi. Sasa imeandikwa “Mwaonaje? Haikumpasa adhabu iliyo kubwa zaidi mtu yule aliyemkanyaga Mwana wa Mungu, na kuihesabu damu ya agano aliyotakaswa kwayo kuwa ni kitu ovyo, na kumfanyia jeuri Roho wa neema? (ebr.10:29)
Nakumbuka mimi na rafiki yangu mmoja tukiwa form six wote tulikwa mabikira… mimi nikaja SUA na kabla sijazini Mungu alinirehemu, akaniwahi, na Yesu akaniokoka nikawa nimeokoka. Lakini mwenzangu yeye alienda Chuo kingine, hakuokoka, na huko akafanya uzinzi… siku moja akaweka picha yake facebook na nilipoiona ile picha nikahisi uharibifu wa nafsi yake. Na baadae bila kumuuliza kwavile alikuwa rafiki yangu akaniambia kwamba alishazini…
Unapozini, nafsi yako pia huharibiwa; Baada ya mtu kuzini kwa mara ya kwanza, nafsi yake huwa twisted na hivyo huwa na tabia au sifa fulani ambazo sio zake kabisa. Uzinzi huharibu personality yako na ku-corrupt true identity ya nafsi yako… kama ilivyoandikwa “Mtu aziniye na mwanamke hana akili kabisa; Afanya jambo litakalomwangamiza nafsi yake” (mithali.6:32).
Uzinzi huambatana na kupoteza kabisa hali ya uthamani wa utu wako wa ndani. Hapa wadada wengi sana (kasoro wachache sana), huanza kuvaa nguo za kikahaba na suruali zinachora maungo yao baada ya kupoteza bikira zao. Hawana aibu tena wala hawaoni haja ya kujitunza, kuisitiri na kuiheshimu miili yao tena, maana tayari wameshapoteza thamani ya utu na wasifu wao wa ndani.
Kibaya ni kwamba huwezi kuitibu nafsi yako au kijitoa kwenye hayo maagano ya damu na nguvu za mapepo Kirahisi. Dawa yake ni moja tu; Umpokee Yesu ili kuyavunja hayo maagano kwa Damu ya Yesu kwa kumpokea Kristo awe Bwana na Mwokozi wako. Kuokoka sio Dini wala kuhama Dhehebu. Kuokoka ni Kuzaliwa mara ya pili yaani born again (yoh.3:3-6), ni kupokea ondoleo la Dambi na kuwa kiumbe kipya (Tit 3:4-6). 

Merry Christmass.

Mwandishi; Nzunda Ibrahim (0754 210 627 / 0785 360 577)

Download Mafundisho haya Hapa!

MTOTO KAZALIWA KWETU

Wengi wamekuwa wakisherehekea sikukuu ya christmass kama ukumbusho wa kuzaliwa kwa mwokozi wa ulimwengu huu ambaye ni YESU Kristo. Lakini wengi wao huwa wanafurahia siku tu kwa kunywa na kula kwa tamaa zao wenyewe. Kaa hata dakika moja ujiulize “kwanini YESU alizaliwa”? 

Na je baada ya kuzaliwa aliagiza nini? Na je unayashika? Hii sherehe ya kukumbuka ni ya siku moja tu, lakini kuna siku ambazo unatakiwa ushike maagizo na kuyatenda . Basi leo hebu jikumbushe kabla ya hiyo siku ili uwe ni mwenye kufahamu kivipi unaweza kusherehekea kwenye kusudi la MUGU na kudumu katika hilo.
 

Tunaona kwenye isaya 9:6 mtoto mwanamume kuzaliwa ambaye ni utambulisho wa MUNGU kuwa pamoja nasi . Hili ni pendo ambalo MUNGU analitoa kwaajili ya binadamu wote kama ilivyo katika yohana 3:16. Kwa hiyo kuzaliwa kwa YESU hapa duniani ni kitambulisho cha kuja kwa wokovu kwa wanadamu wote bila kubagua rangi wala kabila.
 

Kwahiyo kuna mitume na manabii wengi wamekuja, lakini Duniani kuna Mwokozi mmoja tu na ndiye Bwana wa wote yaani YESU. 

Kama ilivyoandikwa “Wala hakuna wokovu katika mwingine awaye yote, kwa maana hapana jina jingine chini ya mbingu walilopewa wanadamu litupasalo sisi kuokolewa kwalo.” (Mdo.4:12)
 

YESU anajieleza kuja kwake duniani ni kwa ajili ya kuleta uzima wa milele na pia wanadamu wawe nao tele. Leo tunapokumbuka kuzaliwa kwa YESU, je tunakumbuka pia ni kwanini alizaliwa? Je, tunakumbuka hata kwa siku hiyo moja tu kujiuliza “uzima wa milele ni nini”? je YESU aliuleta ili ufanye nini kwetu?
 

Pia tusiishie hapo tu; hebu fikria siku ya kumbukumbu ya kuzaliwa kwake unapotoka kuzini au unapotenda machukizo mbele za BWANA . je ile thamani hasa ya MUNGU kumtoa mwanawe wa pekee aje duniani inakuingia akilini?. Basi ndugu kwa neema na rehema zake MUNGU nakuomba kama bado hujajua ni kwanini YESU alizaliwa hebu badilika sasa ufuate kusudi la MUNGU la kuja kukaa na wewe duniani ili akuokoe kutoka kwenye moto wa milele.
 

Kumbuka,
“Kutomchagua YESU, ni automatically kumchagua Shetani, kutochagua uzima wa milele ni kuchagua moto wa milele. Kutochagua mbingu ni kuchagua kuzimu”. Hivyo ndugu usijidanganye kwa kutofanya maamuzi sasa ukizani uko salama. Hakikisha Jina lako linaandikwa kwenye kitabu cha uzima. kwani imeandikwa “iwapo mtu ye yote hakuonekana ameandikwa katika kitabu cha uzima, alitupwa katika lile ziwa la moto” (ufu.20:15). Sikuukuu Njema sana.

GOD WANTS YOU TO BE SAVED!

You will be amazed that the greatest desire of our lovely God is to see us saved. He longs to see us totally free from sins,burdens,bondages,addictions and all dark forces.You will also be amazed that despite all the wrong deeds that we are doing He is and always for us.This means that no matter what you did in the past or you are doing now,still God is not against you,HE IS ALWAYS FOR YOU
.
( For I know the thoughts that I think toward you, saith Jehovah, thoughts of peace, and not of evil, to give you hope in your latter end.Jeremiah 29:11)

What you need to understand is that God wants you to be saved,Yes He does.Just accept Him today by believing Jesus that He is the savior and trust Him for the forgiveness of your sins.It doesn’t matter what kind of sins you did,even the size or number of your mistakes does not matter.What matters is your decision to re-establish your relationship with God and that you want to be saved and delivered .Your religion,tribe,status or gender do not matter as well.Just Make up your mind to start a new life of intimacy with God and humbly ask Him,You will…..I tell you.

I can help you to reach this decision if you wish anyway, Just call this numbers . (0766770422,0713360853)

DO NOT FORGET THIS VERY IMPORTANT TRUTH WHICH IN FACT IS THE DESIRE OF GOD FOR YOU.
GOD WANTS YOU TO BE SAVED..!! YOU ARE WELCOME…!!
Inaendeshwa na Blogger.